Tabora: Maiko Jacobo amuua baba yake kwa shoka kisa imani za kishirikina

John Haramba

JF-Expert Member
Feb 4, 2022
365
1,373
Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora linamshikilia Maiko Jacobo mwenye umri wa miaka 25 mkazi wa Kijiji cha Upungu, Wilaya ya Nzega mkoani hapo kwa tuhuma ya kutenda kosa la kumuua baba yake mzazi mzee Jacobo Lubela mwenye umri wa miaka 88 baada ya kumvizia majira ya jioni akiwa nje ya nyumba yake na kumkata shoka kichwani, shingoni na mikono yote miwili.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora Kamishina Msaidizi wa Polisi, Richard Abwao amesema tukio hilo lilitokea Februari 28, 2022 majira ya saa 1 jioni ambapo mtuhumiwa amekuwa akisumbuliwa na tatizo la ugonjwa wa kifafa ambao amekuwa akiuhusisha kulogwa na baba yake mzazi.

“Mzee Jacobo alijeruhiwa vibaya katika tukio hilo, akakimbizwa katika Hispitali ya Misheni ya Ndala, hali yake ilikuwa mbaya na akafariki usiku wa tukio, pia mtuhumiwa alimjeruhi ndugu yake mwingine Magdalena Jacobo ambaye alipatiwa matibabu na kuruhusiwa kutoka.

“Mtuhumiwa amekiri kuhusika na mauaji hayo na alikutwa na shoka aliyoitumia. Nitoe wito kwa wakazi wa Tabora kuacha kuwa na Imani za kishirikina ambazo zinasababisha matatizo kama haya,” anasema ACP Richard Abwao.


Source: Wasafi Digital
 
Hiyo mikoa; Tabora, Shinyanga, Kigoma, Rukwa sijui lini watu wake watabadilika na kuachana na hizi imani za giza/ushirikina.

Viongozi wetu wa dini wanapaswa wafanye jitihada katika maeneo haya ili kuondoa imani hizi ambazo mwisho wake ni mauaji.
 
Hiyo mikoa; Tabora, Shinyanga, Kigoma, Rukwa sijui lini watu wake watabadilika na kuachana na hizi imani za giza/ushirikina.

Viongozi wetu wa dini wanapaswa wafanye jitihada katika maeneo haya ili kuondoa imani hizi ambazo mwisho wake ni mauaji.
Kuna tumbili watakuja hapa kukwambia hizo ndizo imani zetu za mababu waliotutangulia kuishi duniani na hatutakiwi kuziacha kamwe!

Hakika shetwani ana mawakala hadi JF, lakini kwa nguvu za Mungu tutashinda.
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora linamshikilia Maiko Jacobo mwenye umri wa miaka 25 mkazi wa Kijiji cha Upungu, Wilaya ya Nzega kwa tuhuma ya kutenda kosa la kumuua baba yake mzazi mzee Jacobo Lubela mwenye umri wa miaka 88 baada ya kumvizia majira ya jioni akiwa nje ya nyumba yake na kumkata shoka kichwani, shingoni na mikono yote miwili.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora Kamishina Msaidizi wa Polisi, Richard Abwao amesema tukio hilo lilitokea Februari 28, 2022 majira ya saa 1 jioni ambapo mtuhumiwa amekuwa akisumbuliwa na tatizo la ugonjwa wa kifafa ambao amekuwa akiuhusisha kulogwa na baba yake mzazi.

“Mzee Jacobo alijeruhiwa vibaya katika tukio hilo, akakimbizwa katika Hispitali ya Misheni ya Ndala, hali yake ilikuwa mbaya na akafariki usiku wa tukio, pia mtuhumiwa alimjeruhi ndugu yake mwingine Magdalena Jacobo ambaye alipatiwa matibabu na kuruhusiwa kutoka.

“Mtuhumiwa amekiri kuhusika na mauaji hayo na alikutwa na shoka aliyoitumia. Nitoe wito kwa wakazi wa Tabora kuacha kuwa na Imani za kishirikina ambazo zinasababisha matatizo kama haya,” anasema ACP Richard Abwao.


Source: Wasafi Digital
Du very sad.

Ila

Kati ya tukio hili na la vita ya urusi na Ukraine, wapi watu wamekufa sana. Je huo nao sio ushirikina?
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora linamshikilia Maiko Jacobo mwenye umri wa miaka 25 mkazi wa Kijiji cha Upungu, Wilaya ya Nzega mkoani hapo kwa tuhuma ya kutenda kosa la kumuua baba yake mzazi mzee Jacobo Lubela mwenye umri wa miaka 88 baada ya kumvizia majira ya jioni akiwa nje ya nyumba yake na kumkata shoka kichwani, shingoni na mikono yote miwili.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora Kamishina Msaidizi wa Polisi, Richard Abwao amesema tukio hilo lilitokea Februari 28, 2022 majira ya saa 1 jioni ambapo mtuhumiwa amekuwa akisumbuliwa na tatizo la ugonjwa wa kifafa ambao amekuwa akiuhusisha kulogwa na baba yake mzazi.

“Mzee Jacobo alijeruhiwa vibaya katika tukio hilo, akakimbizwa katika Hispitali ya Misheni ya Ndala, hali yake ilikuwa mbaya na akafariki usiku wa tukio, pia mtuhumiwa alimjeruhi ndugu yake mwingine Magdalena Jacobo ambaye alipatiwa matibabu na kuruhusiwa kutoka.

“Mtuhumiwa amekiri kuhusika na mauaji hayo na alikutwa na shoka aliyoitumia. Nitoe wito kwa wakazi wa Tabora kuacha kuwa na Imani za kishirikina ambazo zinasababisha matatizo kama haya,” anasema ACP Richard Abwao.


Source: Wasafi Digital
Baba yako akuzae mwenyewe kisha Akuroge Mwenyewe?/ Haingii akilini...
 
No matter ni Imani gani au nani anakwambia Kudhuru mwingine its a non - stater

Hivi na yule Abraham aliyekuwa tayari kumtoa Sadaka mwanae eti ana Imani kubwa tungekuwa nao hapa leo si ingekuwa tatizo !!!, Anyway natumai kuna siku mtu atatumie hii kama defense (kwamba nae aliambiwa)..., Ila mimi ningekuwa Isaac ningefunga virago au kuhamia kwa jirani....
 
Hiyo mikoa; Tabora, Shinyanga, Kigoma, Rukwa sijui lini watu wake watabadilika na kuachana na hizi imani za giza/ushirikina.

Viongozi wetu wa dini wanapaswa wafanye jitihada katika maeneo haya ili kuondoa imani hizi ambazo mwisho wake ni mauaji.
Viongozi wa dini siku hizi wanahubiri zaidi sadaka na michango
 
Hiyo mikoa; Tabora, Shinyanga, Kigoma, Rukwa sijui lini watu wake watabadilika na kuachana na hizi imani za giza/ushirikina.

Viongozi wetu wa dini wanapaswa wafanye jitihada katika maeneo haya ili kuondoa imani hizi ambazo mwisho wake ni mauaji.
Uchawi upo mzee...na watu wanafanyiwa hayo
 
Mi nikiona mtu anaamini-amini/anaogopa ushirikina, huwa namdharau na kumuepuka kabisa. Moja ya dalili kubwa ya ujinga na umaskini ni kuamini-amini ushirikina. Paka akilia usiku, au bundi akiimba kujitafutia mademu, yeye anaanza kutukana au kukemea!!
 
Hiyo mikoa; Tabora, Shinyanga, Kigoma, Rukwa sijui lini watu wake watabadilika na kuachana na hizi imani za giza/ushirikina.

Viongozi wetu wa dini wanapaswa wafanye jitihada katika maeneo haya ili kuondoa imani hizi ambazo mwisho wake ni mauaji.
Kaka huko si ndiko tunajizolea kura za kishindo? Wacha ibaki hivyo hivyo tutawale milele. Usiwashtue!
 
Back
Top Bottom