Tabora: Apandishwa Kizimbani kwa kukutwa na nyara ya Serikali, mnyama Kakakuona

Influenza

JF-Expert Member
Jul 1, 2018
1,445
3,403
Mtu mmoja mkazi wa Kijiji cha Usongo ,Nkinga wilayani Igunga anayefahamika kwa jina la Thadeo Shahibu amepandishwa kizimbani hii leo katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Tabora akikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi ya kukutwa anamiliki mnyama Kakakuona kinyume cha Sheria namba tano ya uhifadhi Wanyapori ya mwaka 2009 ambaye anakadiriwa kuwa na thamani ya Dola la Kimarekani 960 ambayo ni sawa na zaidi ya shilingi milioni 2.2 fedha za kitanzania.

3FD4828F-AE72-43B7-B175-ADC13544B8FC.jpeg


Akiwa ameambatana na Mnyama huyo kakakuona,Thadeo Shahibu amefikishwa kwa mara ya kwanza katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Tabora,Mbele ya hakimu Chiganga Tengwa akikabiliwa na shitaka la uhujumu uchumi baada ya kukutwa na Mnyama huyo nyara ya Serikali.

Umati wa watu waliofika mahakamani hapa wakiwemo watumishi wa mahakama walionekana kushangazwa na mnyama huyo ambaye wengi humtafsiri kama ni mnyama wa bahati kumuona hasa katika mazingira ya mjini.

A736AE14-87E5-4B1A-A657-0627096B83D7.jpeg


Mtuhumiwa Thadeo Shahibu alikamatwa akiwa na mnyama huyo katika kijiji Cha Ziba wilayani Igunga wakati akiwa kwenye harakati za kumuuza akidaiwa kumtoa huko Mtera mkoani Iringa ambaye alisafirishwa kwa Pikipiki

Kwa mujibu wa maelezo ya Wakili upande wa Jamhuri Tito Mwakalinga,mtuhumiwa Thadeo Shahibu mnamo tarehe 15 Julai mwaka huu majira ya usiku alikutwa na mnyama huyo kinyume na kifungu cha 86 kidogo cha kwanza na cha pili cha sheria namba 5 ya uhifadhi wanyamapori.

Hata hivyo kutokana na uzito wa shauri hilo la uhujumu uchumi namba 45 la mwaka 2019,mahakama hii ya hakimu mkazi imelazimika kumsomea shitaka mtuhumiwa na hakutakiwa kujibu chochote kwakuwa mahakama hiyo haina nguvu ya kisheria ya kusikiliza shauri hilo hivyo kesi hiyo itatajwa tena August Mosi mwaka huu huku mahakama ikimpa nafasi mtuhumiwa ya kuomba dhamana,wadhamini wawili shilingi million 5,sharti ambalo hakuweza kulitimiza na hivyo kupelekwa Gereza la mahabusu.
 
......................Nchi hii jamani nchi hii!!!?huko mwanza waliokamatwa kwa rushwa tena askari police wakiwasindikiza live wahujumu uchumi na dhahabu wameachiwa huru huku aliyekamatwa na mnyama tena mzima wala hajamuua anapandishwa kizimbani na pingu juu.

Na masharti ya dhamana kapewa makubwa kaenda gerezani akiiacha familia yake mtaani ikihangaika njaa,wenye mamlaka jitazameni huto tuvyeo msiringie kuna leo na kesho oneni huruma hata kidogo.
 
Wangetoa tu elimu kwa mshtakiwa bado ingesaidia. Usikute alikuwa hata hajui ya kwamba kumiliki aina hiyo ya viumbe ni kosa kisheria.

Kesi za uhujumu uchumi zingewabana zaidi wale wahujumu kweli wa uchumi na siyo hao watanzania wanaohitaji kuelimishwa baadhi ya mambo wasiyo yajua.
 
......................Nchi hii jamani nchi hii!!!?huko mwanza waliokamatwa kwa rushwa tena askari police wakiwasindikiza live wahujumu uchumi na dhahabu wameachiwa huru huku aliyekamatwa na mnyama tena mzima wala hajamuua anapandishwa kizimbani na pingu juu.

Na masharti ya dhamana kapewa makubwa kaenda gerezani akiiacha familia yake mtaani ikihangaika njaa,wenye mamlaka jitazameni huto tuvyeo msiringie kuna leo na kesho oneni huruma hata kidogo.
Hii ndy awamu ya tano, na nimemsikia waziri wa katiba na sheria akisema kuwa nanukuu "magereza yote aliyoyatembelea kanda ya ziwa kuna mzongamano mkubwa wa wafugwa 1:3" kwa usemi wake amesahau kuwa yeye ni waziri wa nchi nzima na siyo Tanzania tu.Mfano wapo waislam (masheikhe) kutoka Zanzibar tuliambiwa ni majangili lkn mpaka leo sijui mwaka wa 3 wapo mahabusu, wapo wengine wanasema sijui wahujumu uchumi Kitily,mzee wa Heineken (wakati issue yake wapo waliochukua hela wapo mitaani) na wengine nao wapo ndani.Sasa sijui magereza yakifurika wafugwa inabidi kuwaachilia kwa mujibu wa sheria au msaada wenye wa sheria tafadhali.
Hivi na ile mahakama ya MAFISADI ilifunguliwa kwa madaha na nyimbo nyingi imefikia wapi mpaka sasa mwaka wa tatu??
 
Back
Top Bottom