Tabia za wazazi kwa mtoto wao mpendwa

101 East

JF-Expert Member
Feb 25, 2015
1,040
2,117
Habari wakuu,

Mimi kama Kijana wa kitanzania nina mengi ya kusema kuhusu familia zetu.

Wengi wetu katika familia hizi zetu za kiafrica tumekuwa wahanga wa mahaba ya wazazi kuelemea upande mmoja Kwa Baadhi ya Ndugu zetu.

Wazazi wengi wameshindwa kubalance mahaba kwa watoto ndani ya familia na kupelekea Ndugu wa familia moja kufarakana na kugombana.

Wazazi wengi wamekuwa hawaamini kama kweli wanamahaba kwa mtoto wao fulani ila hili hujitokeza pindi anapofanya makosa

1. Huwa hawaamini kama kweli kafanya hilo kosa
2. Wanaona hamumpendi
3. Mnamuonea
4. Hamjampa nafasi

Ikitokea hajafanikiwa kimaisha yule kipenzi chao basi utasikia
1. Hamumpendi Ndugu yenu
2. Mnamroga
3. Mmemtenga
4. Mimi nikifa mtamuua
5. Hata kama anamakosa ndio Ndugu yenu

Wazee wetu wakiwa watu wazima na wamezeeka hata uwafanyie jambo kubwa kiasi gani hawahisi kama umefanya chochote, lakini Yule kipenzi chao akiwapa hela hata Elfu 5 au kuja kuwaona atahadithia siku nzima.

Jambo hili la mahaba ya wazazi kuelemea upande mmoja limeperekea kuharibu umoja wa familia nyingi
Wito wangu kwa vijana wenzangu.

Sisi ni wazazi mda si mrefu tutakuwa na familia zetu na wengine tunafamilia tayari tujitahidi kuzijenga familia zetu katika upendo Sawa Kwa wote tufiche mahaba yetu kwa mtoto mmoja ili kujenga familia imara.

Karibuni tumwage shuhuda zetu.

Asanteni
 
Nashukuru kwetu hatuna hili tatizo, ila nimesikia malalamiko ya baadhi ya watu kwa wazazi wao.
 
Tumezaliwa wa4 sijawahi hisi nani anapendwa zaidi ya mwingine.
 
Habari wakuu,

Mimi kama Kijana wa kitanzania nina mengi ya kusema kuhusu familia zetu.

Wengi wetu katika familia hizi zetu za kiafrica tumekuwa wahanga wa mahaba ya wazazi kuelemea upande mmoja Kwa Baadhi ya Ndugu zetu.

Wazazi wengi wameshindwa kubalance mahaba kwa watoto ndani ya familia na kupelekea Ndugu wa familia moja kufarakana na kugombana.

Wazazi wengi wamekuwa hawaamini kama kweli wanamahaba kwa mtoto wao fulani ila hili hujitokeza pindi anapofanya makosa

1. Huwa hawaamini kama kweli kafanya hilo kosa
2. Wanaona hamumpendi
3. Mnamuonea
4. Hamjampa nafasi

Ikitokea hajafanikiwa kimaisha yule kipenzi chao basi utasikia
1. Hamumpendi Ndugu yenu
2. Mnamroga
3. Mmemtenga
4. Mimi nikifa mtamuua
5. Hata kama anamakosa ndio Ndugu yenu

Wazee wetu wakiwa watu wazima na wamezeeka hata uwafanyie jambo kubwa kiasi gani hawahisi kama umefanya chochote, lakini Yule kipenzi chao akiwapa hela hata Elfu 5 au kuja kuwaona atahadithia siku nzima.

Jambo hili la mahaba ya wazazi kuelemea upande mmoja limeperekea kuharibu umoja wa familia nyingi
Wito wangu kwa vijana wenzangu.

Sisi ni wazazi mda si mrefu tutakuwa na familia zetu na wengine tunafamilia tayari tujitahidi kuzijenga familia zetu katika upendo Sawa Kwa wote tufiche mahaba yetu kwa mtoto mmoja ili kujenga familia imara.

Karibuni tumwage shuhuda zetu.

Asanteni
Mkuu,kwanza kabisa hakuna mzazi ambaye ana mahaba zaidi kwa mtoto mmoja kuliko kwa mwingine ila Watoto huwa wanashindana kutafuta attention ya Wazazi wao.Mara nyingi mzazi huonekana kumpenda sana yule mtoto ambaye huonekana kutengwa na wenzake.Kwa mafano katika kucheza,kuonewa etc.Matokeo yake inaonekana kwamba mzazi anampenda zaidi kuliko wengine kumbe alikuwa anaweka balance.

Mimi kama baba najua kabisa kwamba upendo wangu kwa watoto ni sawa ila huwa najikuta nakuwa upande wa yule ambaye naona wenzake wamemzidi katika ujanja ubabe,uwezo etc.Mzazi kama anakupa ugali,anakupa mahali pa kulala basi ujue anakupenda hayo mengine ni matatizo ya mtazamo na hisia zako tu.
 
Back
Top Bottom