Tabia za Mameneja Mikopo wa benki kushinikiza 10 percent

dr Akanyonyi Ako

JF-Expert Member
Dec 31, 2012
244
86
Katika pitapita yangu, nimekutana na wateja wa Benki moja hapa Geita, wakilalamikia tabia ya Mameneja wa matawi ya benki hiyo mawilayani kuomba ten pasenti pale wanapopata mikopo.

Yaani; ni hivi ukiomba mkopo wa milioni 3, hatua za kupitisha zikafanikiwa, meneja anakupigia simu ikiwa ni pamoja na kutuma meseji za kuomba umpatie teni parcenti. Baada ya zoezi la asilimia kutolewa wateja hawa huwa wasumbufu kurejesha mikopo na hivyo kupelekea usumbufu kwa maafisa mikopo na wale wanao fuatilia marejesho katika matawi husika.

Nimeongea na walau maafisa mikopo watatu toka matawi matatu tofauti nao wamekili kuwapo kwa tatizo hili; Aidha baadhi ya wateja yaani wawili walikili kushawishiwa ama kutakiwa kutoa teni pasenti pale walipo pata mikopo.

Je wadau mmeishakumbana na tatizo hili? Walioko kanda ya ziwa hasa Geita wanaweza kusema.
 
Ha ha una hoja ila kumbuka watanzania wenzetu mkoani hawana upeo kama wewe uliyeko mjini; (exposure rate)
Dr Huyu anayetoa hana tofauti na yule mwalimu aliyeambiwa adeki na akachukua dekio akadeki. Huku akiwa hajui haki yake na maadili ya viongozi na ukomo wake
 
Ukope wewe ukishapata utoe 10%..
Hata wewe si mjinga?
Ivuga, wengi wa wanaokopa na kutoa 10% hawana vigezo vya kukopesheka! Hivyo basi, ili kulainisha njia ya kukopesheka ndipo huahidi 10% kwa maafisa mikopo ili mambo yaende kilaini. Matokeo yake maafisa mikp wa benki nyingi wameweka huu kama utaratibu rasmi wa kutoa mkopo. Matokeo yake wateja wanakuwa wasumbufu kulipa marejesho, kwa sababu sababu walizoombea mikopo ni za magumashi, na vishika uchumba vya mikopo hio ni magumashi pia. Ni ukweli mchungu.
 
Ivuga, wengi wa wanaokopa na kutoa 10% hawana vigezo vya kukopesheka! Hivyo basi, ili kulainisha njia ya kukopesheka ndipo huahidi 10% kwa maafisa mikopo ili mambo yaende kilaini. Matokeo yake maafisa mikp wa benki nyingi wameweka huu kama utaratibu rasmi wa kutoa mkopo. Matokeo yake wateja wanakuwa wasumbufu kulipa marejesho, kwa sababu sababu walizoombea mikopo ni za magumashi, na vishika uchumba vya mikopo hio ni magumashi pia. Ni ukweli mchungu.

ili linapelekea hata walio na sifa kama nilio waona kukwamishwa
 
Ivuga, wengi wa wanaokopa na kutoa 10% hawana vigezo vya kukopesheka! Hivyo basi, ili kulainisha njia ya kukopesheka ndipo huahidi 10% kwa maafisa mikopo ili mambo yaende kilaini. Matokeo yake maafisa mikp wa benki nyingi wameweka huu kama utaratibu rasmi wa kutoa mkopo. Matokeo yake wateja wanakuwa wasumbufu kulipa marejesho, kwa sababu sababu walizoombea mikopo ni za magumashi, na vishika uchumba vya mikopo hio ni magumashi pia. Ni ukweli mchungu.
Ok Mkuu good explanation.
Kama benk zina wafanyakazi wa aina hii.. Basi hapo hata mimi naweza kwenda kukopa.
Kama naweza kupeleka documents za boda boda na nikapewa mkopo wa milioni mia afu meneja hata akitaka 20 % nampa kwa sababu sina uwezo wa kurudisha hio pesa yao.
Hapo tatizo ni la benk na wafanyakazi wao
 
ili linapelekea hata walio na sifa kama nilio waona kukwamishwa
Sana tu, kwa sababu wenye vigezo vya kukopesheka hawako tayari kutoa 10%, kwa sababu mwisho wa siku hio pesa unailipa wewe bila kusaidiwa na afisa mikopo. Ni aina mpya ya unyonyaji!
 
Ni kweli. Staff mwenzangu aliomba mkopo benki, hela zilipoingia akaanza kusumbuliwa na Afisa Mikopo aliyemuhudumia akiomba ampe mil 1. Hakumpa na alipochoka kuiomba akapotezea.
 
Back
Top Bottom