Masulupwete
JF-Expert Member
- Feb 15, 2012
- 2,366
- 2,397
(1) Unakuta mtu anaongea kwa simu kwa kupaza sauti hadi inakuwa kero kwa wengine. Sijui unataka uonekane mtu wa mipango au ndo vipi? Eti unajua kwenye ile indavyuu mimi pekee ndo nilifanya vizuri. mmxxsh hiyo intavyuu yako sisi inatuhusu nini.
(2) Gari ina AC wenzio wooooote wamefunga vioo wanakula unyunyu wewe umeacha madirisha wazi ukidai eti hupendi AC, mbona gari zisizo na AC ni nyingi kwanini usingeenda kupanda hayo?
(3) Umewekewa video au redio kwa sauti ya wastani kuruhusu hali ya utulivu ndani ya gari. Wewe unapaaza sauti kwa konda eti sauti ni ndogo iongezwe. Sio kila mtu anapenda sauti ya juu achilia mbali hiyo video au redio unayosikiliza.
(4) Kwenye hizi video hasa za action au vichekesho. Wewe unapatwa na mdadi unaanza kurukaruka au kuchekacheka hovyohovyo tena kishabiki utafikiri mwehu. Sio kila mtu anapenda makelele.
(5) Unalala kwenye siti yako hadi unakoroma kama nyau wa mwituni. Kibaya zaidi unamuegemea mtu wa siti ya jirani na kumwagia maudenda yako.
(6) Muda wote wewe unachezeachezea simu yako wakati unajua huna chaja. Matokeo yake unaanza kugongea chaja ya simu kwa wasafiri wengine.
Ukijiona unafanya hayo kuanzia sasa ujijue wewe ni mshamba na unakera wengine, jirekebishe.
(2) Gari ina AC wenzio wooooote wamefunga vioo wanakula unyunyu wewe umeacha madirisha wazi ukidai eti hupendi AC, mbona gari zisizo na AC ni nyingi kwanini usingeenda kupanda hayo?
(3) Umewekewa video au redio kwa sauti ya wastani kuruhusu hali ya utulivu ndani ya gari. Wewe unapaaza sauti kwa konda eti sauti ni ndogo iongezwe. Sio kila mtu anapenda sauti ya juu achilia mbali hiyo video au redio unayosikiliza.
(4) Kwenye hizi video hasa za action au vichekesho. Wewe unapatwa na mdadi unaanza kurukaruka au kuchekacheka hovyohovyo tena kishabiki utafikiri mwehu. Sio kila mtu anapenda makelele.
(5) Unalala kwenye siti yako hadi unakoroma kama nyau wa mwituni. Kibaya zaidi unamuegemea mtu wa siti ya jirani na kumwagia maudenda yako.
(6) Muda wote wewe unachezeachezea simu yako wakati unajua huna chaja. Matokeo yake unaanza kugongea chaja ya simu kwa wasafiri wengine.
Ukijiona unafanya hayo kuanzia sasa ujijue wewe ni mshamba na unakera wengine, jirekebishe.