Tabia za awali kabla ya mabadiliko zina madhara gani katika uhusiano mpya??

Stroke

JF-Expert Member
Feb 17, 2012
34,669
40,917
Habari wadau wa MMU,

Leo nimeona nilete hili jambo kwenu wataalam wa maswala ya mahusiano, hii ni baada ya tukio la siku chache zilizopita, ambapo nilikutana na vijana wawili waliopo katika mahusiano yao ambao kwa mtazamo wa haraka wanaelekea kufunga ndoa.

Kijana namfahamu na binti pia namfahamu kuliko ninavyomfahamu kijana, kilichonifanya nijiulize hili swala, ni kutokana na tabia za awali za huyu binti, ambazo kwa kweli zilikuwa si njema, katika jamii aliyokuwa akiishi yule binti hakuwa na sifa nzuri kwani hakuwa na tabia njema kwa wazazi na pia alikuwa ni mtu wa kuwa na mahusiano mengi mpaka kufikia hatua ya kuzushiwa mambo mengi mno, na kwa kipindi hicho alikuwa bado na umri mdogo tu.

Kwa jinsi ninavyomfahamu kijana nilitegemea kabisa kuwa alistahili kufanya due diligence kabla ya kujihusisha na binti, lakini naona maamuzi yake yatakuwa yamefunikwa na mahaba, kwani hata hivyo kwa historia ya huyo binti sio ajabu kabisa namna alivyofanikiwa kuishi maisha ya sasa.

Ingawa kwa kuangalia kwa haraka utaona kama binti kabadilika ( kaokoka) lakini bado na mashaka kama mabadiliko hayo ni ya kudumu, na huo ndio msingi wa bandiko kama ni kwa namna gani tabia za awali zinaweza kuathiri mahusiano mapya?

Je mtu anaweza kabisa kubadili tabia na kuwa mpya??

Baada ya kuona wanandoa hao watarajiwa nikafikia hitimisho lifuatalo;

1. Ni muhimu mno kwa vijana kuchunguzana kabla ya kuingia kwenye mahusiano ya kudumu. ( Ni muhimu sana).

2. Ni muhimu kwa vijana kuwa makini na matendo yao wakati wa ujana, kwani huko mbeleni matendo hayo huibuka na kutufuatilia, hata na kutaka kuharibu furaha tutakazokuwa nazo kwa wakati huo.

3. Ni muhimu mno kumshirikisha Mungu katika kila jambo na hasa hili la kupata mwenza kwani kuna watu ni mabingwa wa deception.

Karibuni wadau.
 
Mkuu,mtu akiokoka na kuamua kubadilika kweli anakuwa mtu mpya, tabia zake zinakuwa mpya kitu ambacho hakitaondoka ni effects za matendo yake kipindi kile hajaokoka ndio bado zinakuwepo. Mfano kama ulikuwa mwizi ukashindwa ukakatwa kidole kimoja, baadae maishani ukaja ukaokoka, utakuwa mpya kwa matendo yaani utakuwa umeacha wizi lakini kile kidole kilichokatwa hakiwezi kurudi.

Anothing ni kuwa we have to be sure kwamba huyo mwanamke kabadilika kweli au anadanganya ,and this will take time to prove, kwaio tuliache.

Ishu ni je ,tabia zake za nyuma zitaafect uhusiano wake na jamaa? Jibu ni ndio kama tu tabia zake za nyuma zilimpa effects phusically na psychology,ambazo hizo effects zinaweza hatarisha ndoa yake, kwa mfano kutokushika mimba kwa matatizo aliyojisababishia akiwa na tabia mbovu kabla hajabadilika.

So its a gamble kwa jamaa,ila sio kosa lake,until then hatuna uhakika na chochote
 
Hapo kuna mawili.....inawezekana hajaacha tabia yake ila anapretend maana amepata mtu aliyemtangazia ndoa kama unavyojua baadhi ya tabia ni ngumu kuziacha esp kama mtu alikua mzoefu so atapunguza tu ila sio kuacha kabsa

Pili inawezekana kabisa ameacha kwel na amebadilika kwa vile kampata mtu mwenye mapenzi ya dhati sababu hatujui kwann alikua muhuni kipindi cha nyuma....kuna mambo mengi sana/mazingira yanasababisha mtu awe na tabia flani isiyo nzuri ila siku akipata mtu wa kumbadilisha bas anabadilika mazima na kua mpya maana anakua kapata kama pumziko
 
Habari wadau wa MMU,

Leo nimeona nilete hili jambo kwenu wataalam wa maswala ya mahusiano, hii ni baada ya tukio la siku chache zilizopita, ambapo nilikutana na vijana wawili waliopo katika mahusiano yao ambao kwa mtazamo wa haraka wanaelekea kufunga ndoa.

Kijana namfahamu na binti pia namfahamu kuliko ninavyomfahamu kijana, kilichonifanya nijiulize hili swala, ni kutokana na tabia za awali za huyu binti, ambazo kwa kweli zilikuwa si njema, katika jamii aliyokuwa akiishi yule binti hakuwa na sifa nzuri kwani hakuwa na tabia njema kwa wazazi na pia alikuwa ni mtu wa kuwa na mahusiano mengi mpaka kufikia hatua ya kuzushiwa mambo mengi mno, na kwa kipindi hicho alikuwa bado na umri mdogo tu.

Kwa jinsi ninavyomfahamu kijana nilitegemea kabisa kuwa alistahili kufanya due diligence kabla ya kujihusisha na binti, lakini naona maamuzi yake yatakuwa yamefunikwa na mahaba, kwani hata hivyo kwa historia ya huyo binti sio ajabu kabisa namna alivyofanikiwa kuishi maisha ya sasa.

Ingawa kwa kuangalia kwa haraka utaona kama binti kabadilika ( kaokoka) lakini bado na mashaka kama mabadiliko hayo ni ya kudumu, na huo ndio msingi wa bandiko kama ni kwa namna gani tabia za awali zinaweza kuathiri mahusiano mapya?

Je mtu anaweza kabisa kubadili tabia na kuwa mpya??

Baada ya kuona wanandoa hao watarajiwa nikafikia hitimisho lifuatalo;

1. Ni muhimu mno kwa vijana kuchunguzana kabla ya kuingia kwenye mahusiano ya kudumu. ( Ni muhimu sana).

2. Ni muhimu kwa vijana kuwa makini na matendo yao wakati wa ujana, kwani huko mbeleni matendo hayo huibuka na kutufuatilia, hata na kutaka kuharibu furaha tutakazokuwa nazo kwa wakati huo.

3. Ni muhimu mno kumshirikisha Mungu katika kila jambo na hasa hili la kupata mwenza kwani kuna watu ni mabingwa wa deception.

Karibuni wadau.

ukiona visuli suli vingi kanisani kwa mama mbunge ujue kuna jambo wengi washa shindikana,ngoma ngumu,matumaini hakuna wanatafuta pakutokea
 
1. Kuna wanaobadilika totally
2. Kuna wanaojificha kwenye kivuli cha kuokoka.

Hutegemeana na chanzo cha uhuni wake wa nyuma.
 
Back
Top Bottom