Tabia yangu ya kutojipendekeza, kusujudia maboss na kutokuwa mfitini inanisotesha mtaani

Kategele

JF-Expert Member
Oct 7, 2017
968
2,230
Kama kawaida baada ya kumaliza chuo nikaingia mtaani kusota na maisha bahati nzuri nikapata intern kwenye moja ya taasisi za serikali zinazolipa vizuri.​

Changamoto ikawa kumbe kwenye taasisi hizi za serikali inatakiwa ufanye kazi kwa bidii bila kusahau kujipendekeza kwa boss.​
Kwa jinsi nilivyo tabia yangu ya kutopenda kujipendekeza wala kufitini wafanyakazi wenzagu mimi nikawa natimiza Majukumu kama kawaida.​

Kumbe ilitakiwa niwe naenda hata kumuona boss personly angalau mara moja kwa wiki kumsalimia tu ambavyo wengine hufanya sasa mimi nawaza nikamuone manager nimweleze nini cha zaidi wakati meeting za Kila wiki tunakutana na kila mtu anawasilisha ripoti yake?.​

Basi bwana boss akaanza kulalamika ooh sina msaada kwenye office ikabidi nifuatilie kujua ninakwama wapi bassi wadau wakanitonya jipendekeze nenda hata mara moja peleka umbea wowote ule atakukubali tu.​

Asikwambie mtu hakuna kazi ngumu Kama kuwa mmbeya eneo la kazi Kama hauna tabia hiyo.​

Mimi nikasema potelea mbali ilimradi natimiza Majukumu yangu na nipo qualified siwezi kujipendekeza kwenye ofsi hii nitapata kazi hata kwingine.​

Mkataba wa intern ukaisha boss Kama kawaida akaaniambia nitafute kazi sehemu nyingine.​

Mwamba nikaona siyo kesi nikaingia mtaani nikapata kazi kampuni nyingine ya kibongo aisee kule ndio ikawa balaa bila kuwa mbeya humalizi mwezi unatimuliwa boss anataka kila siku mpishane na wafanyakazi ili apate taarifa mara huyu kapeleka fulani mwizi kaiba mafuta, kifusi.​

Daah nikaona pia isiwe kesi nikaacha kazi.​
Sasa Nina mwaka nasota mtaani nimezunguka kinoma hamna kazi kila Kona patupu wadau wanashauri tafuta hata viongozi wa kisiasa ujipendekeze kazi siku hizi kujuana mimi naona wananisumbua tu.​

Natafuta kazi nikiamini qualifications zangu zitanibeba lakini patupu nimeapply sehemu nyingi hata kuitwa hakuna.​

Nikatafuta mpaka sehemu za vibarua patupu. Sasa nawaza hii tabia ya kutojipendekeza nitaachaa vipi maana kubadili tabia ni ngumu kama kubadili ngozi.​
 
Ona sasa....when in rome you do as the romans do.
Hii kauli muhimu sana.

Wakati naanza kazi Unyamwezini, kuna ofisi nilikuwa nafanya, bosi mtu poa sana nilimuona. Yuko focused kiaina, lakini very approachable.

Sasa siku moja nikaamua kumtembelea ofisini kwake, a sort of "management by walking around",maana kuna watu wengine wanaweza kuwa na issue hawakufuati, lakini ukiwafuata, wanakueleza issues zao.

He, basi nilivyomfuata ofisini kwake, tena wala si kwa nia ya kujipendekeza-I have too much pride for that- ila kumsalimia tu, jamaa alinibadilikia mpaka leo siwezi kusahau.

Aliniangalia akaniuliza, umekuja kufanya nini hapa? Nikasema nimekuja kukusalimia tu. Akasema niko busy saa hizi. Nikasema OOOOK.

Needless to say, miezi michache baadaye nilitafuta sehemu nyingine nikajikata.

Sehemu nyingine hata ukitaka kusalimia watu ni kwa appointment, ama sivyo unaonekana unapotezea watu muda.
 
Usiogope na usijali. Kaa ukijua wema na uaminifu unalipa sana. Pia kumbuka giza na nuru haviishi sehemu moja lazima nuru italiangamiza giza.

Brother, utapata kazi nzuri sana ambayo hukuwahi kuiwaza kabisa maana ni aina ya kazi ambayo ndio ndoto ya watu wengi.

Mungu akusimamie katika kila jambo.
 
Kitu pekee ntakua mdogo na mnyenyekevu kuliko maelezo ni pale nimekamatwa na mke wa mtu..vinginevyo kwenye mambo ya kazi hapana kabisa kuendekeza kujipendekeza.

Mtu umeacha kazi zako na kwa nia njema umeenda kusabahi tu, anashindwa hata kuthamini akatumia lugha ya staha kukufukuza badala ya kuwa muungwana?

Niliwahi kuacha kazi sehem kwa mambo haya haya.
 
Kitu pekee ntakua mdogo na myenyekevu kuliko maelezo ni pale nimekamatwa na mke wa mtu..vinginevyo kwenye mambo ya kazi haoana kabisa kuendekeza kujipendekeza.

Mtu umeacha kazi zako na kwa nia njema umeenda kusabahi tu, anashindwa hata kuthamini akatumia ligha ya staha kukufukuza badala ya kuwa muungwana?

Niliwahi kuacha kazi sehem kwa mambo haya haya.
Yule jamaa inawezekana nilimkuta yupo katikati ya stress za madeni.

Jamaa alikuwa eccentric Professor fulani hivi kawa frustrated na maisha, rafiki zake aliosoma nao wote wametoboa maisha, mmoja alikuwa rais Europe. Yeye alikuwa anajiona kalosti.

Mimi nilivyousoma mchezo tu na kuona hapa hamna respect nilijikata zangu.

Tatizo jamaa ni bonge la passive aggressive. Leo kakuzodoa hivyo, kesho anakupa offer vizuri akununulie lunch kama bosi poa tu.

Nikasema hapa hapanifai.

I had the exact opposite problem, ofisi ile ukijipendekeza ndiyo unaleta tatizo, watu hawana muda wa kuendekeza kujipendekeza.
 
Basi utakuwa na nyota ya umbea, nakushauri ukianza kazi popote fanya kazi Kama vile upo mwenyewe, wafanya kazi wengine akiwemo boss wako mpe heshima yake halafu tembea mbele. Find your style of working, mimi nimefanya kazi hadi nimeamua kujiajiri ni mtu ninayeheshimika sehemu zote nilizofanya field, kazi kibarua na sijawahi kujipendekeza kwa boss, Kuna wapambe wa Boss na wanaojiweka karibu na maboss achana nao kiaina, wapigie story za uongo ikiwezekana .

Nasisitiza inawezekana kufauata Mambo yako na ukaish fresh kazini kwa raha zako, hata mawe yatakutetea pale kila mtu anapokuwa kinyume na wewe, nimefanya field serikalini, nimajiriwa kampuni binafsi kubwa mbili, kampuni ndogo mbili ya pili ndio mkataba ulipoisha niliomba kusitisha kwa sababu walikuwa wanakula muda wangu Sana, sijawahi kubebwa na mtu yoyte kazini, kuwa mbunifu ujiajiri lakini lazima ufanye kazi kidogo ujikusanyie mtaji, kwa sababu kujiajiri kuna kuzoea mzingira, Kuna kupata kahasara vichangamoto falni Kama upo serious kitakachokutesa ni hela tuu baasi ambayo ukijiwekea malengo mradi unaupanga mwaka ambao umepanga ndo wa mwisho kufanya kazi. Kila la heri.
 
Yaan kama unanisemelea Mimi

Hiki ndo kipo ofisin kwetu, usipojipendekeza unapigwa chini
Wanakupa changamoto uwe mjasiliamali na wewe uajiri watu wajipendekeze kwako.

Yani bosi hata ukivaa vibaya msela haueleweki utasikia unasifiwa tu.
Utasikia "Bosi hii ya leo umeitoa wapi, Dubai au Paris".

Wakati wewe unaona kabisa hapa hamna kitu mtu anajikomba tu.
 
Yah! Naelewa unachokisema. Yamenikuta pia,ila na mimi naona watu wa aina hii tunatakiwa kujiajiri na si kuwafanyia watu kazi zao na hayo ya ziada ndio wakuappriciate.
Ghwee bhututu ughwe
76771519_618171332255722_4684460713089957888_n.jpg
 
Back
Top Bottom