Tabia ya watanzania kulalamika/kulaumu kila jambo zuri/baya

money bag

JF-Expert Member
Jan 15, 2016
373
297
Habari za asubuhi wadau jf.

Binafsi kuna jambo nashindwa kuelewa khs tabia ya sisi wa Tanzania kujijengea tabia ya kulalamika.

Kwa mfn:- mhe. Rais anamtumbua kiongozi utashangaa utasikia watu wanalalamika oooh ameonewa, oooh tumbua haikuwa na tija amekurupuka, mradi fln mzr unaanzishwa utasikia oooh watanzania kwa kuiga, pesa zinapigwa n.k

Another hand anateuliwa mtu kushika nafasi flan serikalini au taasis flan yaani watu hata hawamjui lkn utasikia wanalalamika oooh hawa ni walewale, hana lolote, ataweza kweli?

Sasa sisi watanzania tukae kundi gani jambo zurI likifanyika tunalalamika, jambo zuri tunalalamika nini shida?

Naomba tusaidiane tukomeshe hii tabia ifike mahali kwa jambo zuri tunapongeza na kupeana moyo sio kukandia, kulalamika na kulaumu na mbaya zaidi mtu analalamika hlf hatoi way forward.
 
Kwa sababu watanzania wengi wamelelewa kwa mawazo hasi kwenye kila jambo hawana jema. Pia umaskini wa fikra, kipato na elimu na kujitambua.
 
Umetumwa wewe si bure...haya malalamiko ndo yanasaidia kufichua maovu. Watu ni wanafiki sana sio km unavofikiri
 
Unaposema malalamiko ni kwa watanzania umetumia takwimu gani? Kila uovu hulalamikiwa, huoni huko wanakopigana hayo ni matiokeo ya malalamiko, kama kuna zuri linasifiwa lazima liwepo baya nalo lilalamikiwe.
 
Unaposema malalamiko ni kwa watanzania umetumia takwimu gani? Kila uovu hulalamikiwa, huoni huko wanakopigana hayo ni matiokeo ya malalamiko, kama kuna zuri linasifiwa lazima liwepo baya nalo lilalamikiwe.
Anataka sifa za kifalme...kwa kuwa ccm inatawala kifalme hakuna kunyooshewa kidole. Mfalme juha
 
Back
Top Bottom