Tabia ya ubishi kwenye utoaji wa nauli miongoni mwa watu wanapotumia vyombo vya usafiri.

Tychob

JF-Expert Member
Apr 29, 2013
3,646
4,611
Habari wakuu .

Naamini Mungu ametujalia afya na uzima mbali na changamoto mbali mbali za huu mwaka.

Nirudi kwenye lengo la maada yangu . Kama wewe ni msafiri ama umewahi kutumia vyombo vya usafiri vya umma kama mabasi n.k. naamini ushakutana na hili la watu kubisha kutoa nauli iliyopangwa na inayofahamika kwa maksudi kabisa.

Mfano unaweza kua unatoka mji A kwenda mji B , na kiwango cha nauli kina fahamika kwa basi kuwa ni sh 3000. Sasa tatizo linakuja kwa baadhi ya watu, baada ya kupanda gari na pasipo kuongea na" konda "

Wakati konda anapita kuchukua nauli na anapo mfikia huyu abiria anaanza kusema "mimi nina 2000 tuu" hapo mmefika karibia nusu ya safari. Ajabu huyo jamaa anaanza kuwa mkali pale konda anamgomea juu ya hicho kiwango kinachofuata utaskia huyo abiria "ooohh mnalinga na magari yenu ,tutakua hatupandi magari yenu " cha kujiuliza wewe unapanda gari na unajua kiwango cha nauli husika . Kero ni pale linapoibuka zogo baina ya konda na huyo Abiria "msumbufu" kiasi cha kuwa kero kwa sisi wengine tunaoskiliza malumbano yao pia pale huyo abiria asiye na staha kutaka abiria wengine wamsaidie katika huo ujinga wake.

Hii tabia ipo saana kwa abiria wa nje ya miji ama vijijini na wengine.

Naamini kuna watu pia ni wasumbufu na pia kuna watu hawapendezwi na hizi tabia.

Tujifunze kuheshimu taratibu na kuheshimu kazi za watu.


Karibu uchangie chochote kama kuna kisa chochote kuhusiana na hii kadhia ulishawahi kukutana nayo...
 
Habari wakuu .

Naamini Mungu ametujalia afya na uzima mbali na changamoto mbali mbali za huu mwaka.

Nirudi kwenye lengo la maada yangu . Kama wewe ni msafiri ama umewahi kutumia vyombo vya usafiri vya umma kama mabasi n.k. naamini ushakutana na hili la watu kubisha kutoa nauli iliyopangwa na inayofahamika kwa maksudi kabisa.

Mfano unaweza kua unatoka mji A kwenda mji B , na kiwango cha nauli kina fahamika kwa basi kuwa ni sh 3000. Sasa tatizo linakuja kwa baadhi ya watu, baada ya kupanda gari na pasipo kuongea na" konda "

Wakati konda anapita kuchukua nauli na anapo mfikia huyu abiria anaanza kusema "mimi nina 2000 tuu" hapo mmefika karibia nusu ya safari. Ajabu huyo jamaa anaanza kuwa mkali pale konda anamgomea juu ya hicho kiwango kinachofuata utaskia huyo abiria "ooohh mnalinga na magari yenu ,tutakua hatupandi magari yenu " cha kujiuliza wewe unapanda gari na unajua kiwango cha nauli husika . Kero ni pale linapoibuka zogo baina ya konda na huyo Abiria "msumbufu" kiasi cha kuwa kero kwa sisi wengine tunaoskiliza malumbano yao pia pale huyo abiria asiye na staha kutaka abiria wengine wamsaidie katika huo ujinga wake.

Hii tabia ipo saana kwa abiria wa nje ya miji ama vijijini na wengine.

Naamini kuna watu pia ni wasumbufu na pia kuna watu hawapendezwi na hizi tabia.

Tujifunze kuheshimu taratibu na kuheshimu kazi za watu.


Karibu uchangie chochote kama kuna kisa chochote kuhusiana na hii kadhia ulishawahi kukutana nayo...
Kuna watu hawapendi kumaliza siku hawajagombana. Waache waendelee na makondakta nao wapate changamoto kwenye kazi yao.
 
Afadhali ya hao wanaolipa pungufu ,kuna siku jamaa katulia zake ,amejaza misuli kama baunsa,konda alipomfikia kudai nauli akasema nimekupa usinisumbue ,jamaa aligoma mwanzo mwisho hadi mwisho wa safari
 
Kuna watu hawapendi kumaliza siku hawajagombana. Waache waendelee na makondakta nao wapate changamoto kwenye kazi yao.
Mkuu kuna watu wana hela kabisa ila kutoa nauli inayotakiwa hawatoi sijui kwanini?
 
Afadhali ya hao wanaolipa pungufu ,kuna siku jamaa katulia zake ,amejaza misuli kama baunsa,konda alipomfikia kudai nauli akasema nimekupa usinisumbue ,jamaa aligoma mwanzo mwisho hadi mwisho wa safari
Nilikutana na kisa kimoja hivo hivo mtu hataki kutoa nauli inayohitajika konda akamwambia dereva amshushe kituo kinachofuata , jamaa akaanza kugoma kushuka dereva akapaki akasema haendelei bila kushuka huyo jamaa. Ilibidi abiria tuingilie kati. Sasa najiuliza mtu unafanya yote haya ili iwaje?.
 
Halafu wakishaona wameshindwa wanajifanya kudai tiketi, utasikia nipe tiketi yangu konda nae anampa bila wasi. Nawaonaga washamba tu unakuja kusumbua sumbua watu wako kazini!
 
Halafu wakishaona wameshindwa wanajifanya kudai tiketi, utasikia nipe tiketi yangu konda nae anampa bila wasi. Nawaonaga washamba tu unakuja kusumbua sumbua watu wako kazini!
Anavodai tiketi sasa kama ugonvi...
 
Hii huchangiwa na magari kushusha nauli ya kipande husika muda ambao abiria si wengi hivyo kuzoesha abiria kuwa nauli ni kiasi fulani.
 
Back
Top Bottom