Tabia mbaya kumi zinazofanya ushindwe kuwa na akiba "savings"

Daaah! Umepiga za chembe Mkuu, lazima wengi tukae kusikilizia maumivu. Nice kick kiongozi and salute.
 
Wenye masikio tumesikia na wenye macho tumeona ,ujumbe huu unafaa kwa kila mwenye pumzi
 
Nimeelimika na naomba nimpongeze mleta mada


Ni elimu ambayo tunapaswa kuizingatia wadau lakn kuna challenge ya ndugu hapo wadau.Unajua wengi wetu tunabahatika kupata maisha lakn ukiangalia familia zetu ni duni.

Sasa kinachotokea ni kwamba umeanza kazi na basic ya la 1.5 lakn una wadogo zako shule wawili au watatu,nyumba umepanga,bili ya maji na umeme,mtoto yupo english medium na baba na mama kule kijijini wanakutegemea unajikuta unashindwa mkuu.
 
TABIA MBAYA
1.Unanunua nguo bila mpangilio..
Kuna watu wana nguo kama duka.
Plz Kuwa na nguo chache Tu
huwezi kushindana na fashion.
2.unanunua Viatu bila mpango.
Viatu pia vinameza savings zetu.
Nunua pea chache zenye ubora ili
zidumu.
3.unatoa ofa bar bila mpango.
Nenda bar kwa bajeti mahususi.
Hakuna atakae kusifia kwa kutoa
ofa hovyo. Kila mbuzi ale kwa
urefu Wa kamba yake. Jifunze
ubepari.
4.unatumia hela nyingi kwenye
simu ambazo sio productive.
Unaweka vifurushi vya week vya
sh 7000 au 1000 ili uchati na
marafiki Fb au wasaap Huo ni
ujinga. Badilika.
5.unakopa hela banki na kununua
vitu kama simu ya milioni na gari
ambazo sio productive. Unakosa
hela hata ya mafuta, gari la nini
kwanini usingewekeza sehemu ili
kuwe na mradi Wa kuzalisha ndio
ununue gari?
6.una marafiki wengi ambao ni
mizigo kwako au hamuendani
kivipato hivyo unajikuta
unalazimika kutumia zaidi ya
kipato chako ili uwa-impress.
Meneja Wa TRA na mwalimu Wa
sec unatarajia utoe offer mpaka
umfurahishe meneja? Utabaki na
sh ngapi toka kwenye salary
yako?? Zinduka.
7.huna timetable ya kudumu ya
maisha yako, unajikuta
unaburuzwa Tu na maradiki zako
kwa kwenda sehemu mbalimbali
za matumizi.
Kuwa na ratiba za maisha yako na
zisimamie kikamilifu, usiburuzwe!
8.una michepuko inayokutegemea
we we kwa kila kitu. Wanakuita
ATM we we unakenua Tu
huzinduki. Badilika.
9.una huruma sana kuliko kipato
chako. Yaani kila ukiombwa
unatoa hata kama muombaji hana
genuine need. Usiwe mkristo
kuliko Yesu. Fanya hivyo kama ni
lazima. Ila sio kila anaekupiga
mzinga unapigika.
10.unatembea na hela nyingi
kwenye wallet au mshahara wote
kwenye wallet au nyumbani
kwako. Unapokuwa na petty cash
nyingi unatengeneza mazingira ya
kutumia hovyo. Jifunze kuweka
hela benki. Tembea na hela Tu
unayoihitaji kwa matumizi ya
lazima.
Naamini tukizingatia kanuni hizi
kumi tutaongeza savings zetu na
kuwa na mtaji Wa kufanya vitu
vikubwa endelevu.


Anza sasa...badilika...
 
Da mtu wa hayo ndio mawazo ya mwanaume wa kweli Mimi kuanzia sekunde hii nafungua m power mawazo safi sana
 
Namshukuru Mungu Hii elimu niliipata Muda nikiwa darasani saivi nakula matunda yake.
 
Michepuko ndio namba moja, mengine ziada tu. Bila kusahau kupenda kula vyakula vya bei ghali katika migahawa mikubwa.
 
We mtoa mada unaweza kabisa kuinyosha hii jamii ya kipato kidogo matumizi makubwa na kikabadilika asante
 
mkuki wa moyo kwa wengi. mm huwa nashangaa, mwanaume anajisifia kuwa na wanawake au wapenzi zaidi ya 3 nje ya ndoa,,,!! at the same time ana ndoto ya kujenga nyumba nzuri, gari ya kifahari.....
 
Japo siyo siasa LAKINI tunashukuru, haya ni mawazo ya kujenga. Jambo jingine ambalo ni muhimu kuongezea:

11. Usikimbilie kuanzisha miradi ambayo huna uhakika nayo, mara nyingi miradi ya kuiga. Fanya utafiti wa kutosha, na unaporidhika na kuamua kuanzisha mradi, wekeza pesa kiasi kidogo, ile tu ya kuuwezesha mradi usimame, na kisha pima maendeleo ya mradi wenyewe kabla hujaingiza pesa yote uliyo nayo.

12. Weka vigezo vya kukusaidia kutambua kama mradi ni viable or not. Ukiridhika kuwa mradi hauna faida, chukua maumuzi magumu ya kuufunga kabla haujakuingizia hasara kubwa lakini pia usiwe mwepesi wa kufunga mradi kama una jibu la kwa nini mradi haukutoa faida, na hicho kilichosababisha una uwezo wa kukitatua.

Na hapa ndipo watu wengi wanapoumia
 
Dah, hayo yote me siyafanyi but at the end of the day sina kitu. Hata sijui ni kwanini ingawa I'm a middle income earner!
 
mimi sehem kubwa nazimudu ila ninaposhindwa ni hapo kwenye mizinga maana nimesomeshwa na ndugu wengi na wanaponipiga mizinga lazima nipigike,
Je nifanyeje?
 
62 Reactions
Reply
Back
Top Bottom