Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,806
- 11,968
Taasisi ya Twaweza pamoja na Taasisi ya Uwezo Tanzania leo Desemba 11 zinazindua ripoti ya 'Tathmini ya Kiwango cha Kujifunza Nchini ya mwaka 2019'
Tathmini kubwa iliyofanywa na Taasisi ya Uwezo Tanzania kwa Wananchi tangu mwaka 2011 imetoa mchango madhubuti katika kuongeza uelewa wa hali ya kisomo nchini
Tathmini hizo zimesaidia kuboresha maarifa juu ya usawa ambao unaendelea katika upatikanaji wa elimu na upatikanaji wa ujuzi wa kusoma na kuhesabu
Ripoti hiyo inatarajiwa kuzinduliwa katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar kuanzia majira ya saa 3:30 asubuhi
Aidan Eyakuze - ED Twaweza
Utafiti huu uliwafikia watoto 65,000 na kaya 25,000, tumefikia wilaya 56 na tumetumia vijana 3,360 kupata matokeo haya.
Utafiti huu Haukinzani na tafiti nyingine ambazo pia zina uhalisia wake. Huu utafiti unajazia tafiti nyingine ambazo labda hazikumulika hapa.Huu mchango wetu, mchango wenu kama wadau na walaji wa hizi data.
Ripoti hii inawahamasisha wazazi kufuatilia mienendo ya watoto wao kwa ukaribu ikiwa ni pamoja na kuchukua mawasiliano ya walimu wanaowafundisha watoto.
Zaida Mgalla - Meneja wa Uwezo Tanzania
Tunaangalia mazingira ambayo yatapelekea mtoto kujifunza kama vyoo bora, chakula, maji
Tunaanga rasilimali kama je walimu wapo wa kutosha
Tunaangalia suala zima la elimu jumuishi- watoto wote wanaenda shule
Tunaangalia parental participation
Jitihada hii inapima uwezo wa wananchi ili kupima uwezo wa watoto kusoma na kuandika.Tunatengeneza majaribio yetu kwa kuzingatia mtaala wa Serikali kwa darasa la pili, Lengo ni kutoa tathmini ya uwezo wa watoto wetu ktk kujifunza
Ripoti hii ni takwimu ambazo tulizikusanya mwaka 2017. Tumefanya tathmini ya mwaka 2017 kukiwa na msisitizo mkubwa sana wa kufundisha KKK na Elimu bure kwa watoto wote.Takwimu zitatuonesha kama kweli watoto wote walikwenda shule
Uwezo ni jitihada iliyoanza 2009 katika nchi za Afrika Mashariki, Hufanyika nyumbani ili kupata watoto wote walio katika umri wa kwenda shule (miaka 6-16) ambao wako shule au la
Tunaangalia uwepo wa rasilimali watu katika shule. Je, kuna walimu wa kutosha shule. Pia tunaangalia suala la elimu jumuishi kama watoto wote wanakwenda shule hata wale wenye ulemavu pamoja na ushiriki wa wazazi katika masuala ya elimu
Kwanini #Uwezo ni muhimu? Taarifa tunazopata tunaleta mwanga mpya. Mfano katika suala la elimu jumuishi, upatikanaji wa mahitaji muhimu shuleni kama maji. Tunaamini matokeo yetu haya yanasaidia kuongeza ladha katika takwimu zinazotolewa na Serikali
Takwimu zinaonesha idadi ya kuandikisha watoto shule imeongezeka. Ktk upande wa jinsia hakukuwa na utofauti kwani watoto wote walikuwa wameandikishwa kwa uwiano ulio sawa. Kwa watoto wenye mahitaji maalumu, asilimia 28 hawakuwa wameandikishwa shule
Kwa darasa la 7 ufaulu umeshuka ila kwa darasa la 3 umefaulu umeongezeka kidogo kutoka 29% mwaka 2011 mpaka 62% mwaka 2017. Kinachochangia kwa darasa la 3 ni kutokana msisitizo wa kufundisha KKK tofauti na kwa madarasa ya juu kama darasa la 7
Bado kuna shida ya wanafunzi kusoma Kiingereza ambapo kwa takwimu takriban nusu ya darasa hawawezi kusoma Kiingereza. Hii italeta shida kubwa pale watakapokuwa wamefika madarasa la juu hasa Sekondari kwani masomo mengi yapo katika Kiingereza
Asilimia kubwa ya watoto kutoka maeneo ya mijini waliweza kujibu maswali ya jaribio la #Uwezo tofauti na wale wa vijijini,Pia watoto waliotoka familia zenye uwezo kiuchumi waliweza kujibu maswali kwa usahihi zaidi kuliko wale wa kaya masikini
23% ya shule zinatoa chakula kwa wanafunzi na kuna utofauti ktk Mikoa na Wilaya. Mfano karibu shule zote za Moshi na Ludewa wanatoa chakula kwa wanafunzi. Aidha 39% ya kaya ndizo zilibainika zinatoa chakula kwa watoto kabla ya kwenda shule asubuhi
Asilimia 50 ya wazazi waliohojiwa ndiyo walionekana kwamba wanatembelea Walimu mashulenu katika kufuatilia maendeleo ya mtoto. Asilimia 21 ya wazazi walionekana kuwa hukagua madaftari ya watoto wao watokapo shuleni
Tulichokiona ni kuwa Watoto wanaotoka kwenye kaya masikini na wale wa vijijini wana fursa ndogo sana ya kuweza kujifunza
Tunapendekeza kwamba hizi takwimu huria zipewe kipaumbele na pia ni muhimu kushughulikia suala la usawa kwa watoto kupata elimu.Tumekusanya data pia kwenye Governance and accountability
RIPOTI KWA UFUPI
Tathmini kubwa iliyofanywa na Taasisi ya Uwezo Tanzania kwa Wananchi tangu mwaka 2011 imetoa mchango madhubuti katika kuongeza uelewa wa hali ya kisomo nchini
Tathmini hizo zimesaidia kuboresha maarifa juu ya usawa ambao unaendelea katika upatikanaji wa elimu na upatikanaji wa ujuzi wa kusoma na kuhesabu
Ripoti hiyo inatarajiwa kuzinduliwa katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar kuanzia majira ya saa 3:30 asubuhi
Aidan Eyakuze - ED Twaweza
Utafiti huu uliwafikia watoto 65,000 na kaya 25,000, tumefikia wilaya 56 na tumetumia vijana 3,360 kupata matokeo haya.
Utafiti huu Haukinzani na tafiti nyingine ambazo pia zina uhalisia wake. Huu utafiti unajazia tafiti nyingine ambazo labda hazikumulika hapa.Huu mchango wetu, mchango wenu kama wadau na walaji wa hizi data.
Ripoti hii inawahamasisha wazazi kufuatilia mienendo ya watoto wao kwa ukaribu ikiwa ni pamoja na kuchukua mawasiliano ya walimu wanaowafundisha watoto.
Zaida Mgalla - Meneja wa Uwezo Tanzania
Tunaangalia mazingira ambayo yatapelekea mtoto kujifunza kama vyoo bora, chakula, maji
Tunaanga rasilimali kama je walimu wapo wa kutosha
Tunaangalia suala zima la elimu jumuishi- watoto wote wanaenda shule
Tunaangalia parental participation
Jitihada hii inapima uwezo wa wananchi ili kupima uwezo wa watoto kusoma na kuandika.Tunatengeneza majaribio yetu kwa kuzingatia mtaala wa Serikali kwa darasa la pili, Lengo ni kutoa tathmini ya uwezo wa watoto wetu ktk kujifunza
Ripoti hii ni takwimu ambazo tulizikusanya mwaka 2017. Tumefanya tathmini ya mwaka 2017 kukiwa na msisitizo mkubwa sana wa kufundisha KKK na Elimu bure kwa watoto wote.Takwimu zitatuonesha kama kweli watoto wote walikwenda shule
Uwezo ni jitihada iliyoanza 2009 katika nchi za Afrika Mashariki, Hufanyika nyumbani ili kupata watoto wote walio katika umri wa kwenda shule (miaka 6-16) ambao wako shule au la
Tunaangalia uwepo wa rasilimali watu katika shule. Je, kuna walimu wa kutosha shule. Pia tunaangalia suala la elimu jumuishi kama watoto wote wanakwenda shule hata wale wenye ulemavu pamoja na ushiriki wa wazazi katika masuala ya elimu
Kwanini #Uwezo ni muhimu? Taarifa tunazopata tunaleta mwanga mpya. Mfano katika suala la elimu jumuishi, upatikanaji wa mahitaji muhimu shuleni kama maji. Tunaamini matokeo yetu haya yanasaidia kuongeza ladha katika takwimu zinazotolewa na Serikali
Takwimu zinaonesha idadi ya kuandikisha watoto shule imeongezeka. Ktk upande wa jinsia hakukuwa na utofauti kwani watoto wote walikuwa wameandikishwa kwa uwiano ulio sawa. Kwa watoto wenye mahitaji maalumu, asilimia 28 hawakuwa wameandikishwa shule
Kwa darasa la 7 ufaulu umeshuka ila kwa darasa la 3 umefaulu umeongezeka kidogo kutoka 29% mwaka 2011 mpaka 62% mwaka 2017. Kinachochangia kwa darasa la 3 ni kutokana msisitizo wa kufundisha KKK tofauti na kwa madarasa ya juu kama darasa la 7
Bado kuna shida ya wanafunzi kusoma Kiingereza ambapo kwa takwimu takriban nusu ya darasa hawawezi kusoma Kiingereza. Hii italeta shida kubwa pale watakapokuwa wamefika madarasa la juu hasa Sekondari kwani masomo mengi yapo katika Kiingereza
Asilimia kubwa ya watoto kutoka maeneo ya mijini waliweza kujibu maswali ya jaribio la #Uwezo tofauti na wale wa vijijini,Pia watoto waliotoka familia zenye uwezo kiuchumi waliweza kujibu maswali kwa usahihi zaidi kuliko wale wa kaya masikini
23% ya shule zinatoa chakula kwa wanafunzi na kuna utofauti ktk Mikoa na Wilaya. Mfano karibu shule zote za Moshi na Ludewa wanatoa chakula kwa wanafunzi. Aidha 39% ya kaya ndizo zilibainika zinatoa chakula kwa watoto kabla ya kwenda shule asubuhi
Asilimia 50 ya wazazi waliohojiwa ndiyo walionekana kwamba wanatembelea Walimu mashulenu katika kufuatilia maendeleo ya mtoto. Asilimia 21 ya wazazi walionekana kuwa hukagua madaftari ya watoto wao watokapo shuleni
Tulichokiona ni kuwa Watoto wanaotoka kwenye kaya masikini na wale wa vijijini wana fursa ndogo sana ya kuweza kujifunza
Tunapendekeza kwamba hizi takwimu huria zipewe kipaumbele na pia ni muhimu kushughulikia suala la usawa kwa watoto kupata elimu.Tumekusanya data pia kwenye Governance and accountability
RIPOTI KWA UFUPI