Limekuwa ni jambo la kawaida siku hizi kusikia Rais either amesitisha kazi za Waziri/Mawaziri kadhaa au amevunja baraza la Mawaziri kutokana na sababu kadha wa kadha.
Tatizo kubwa hapa ni jinsi hawa Mawaziri wanavyopatikana kwani wanateuliwa moja kwa moja na Rais bila ya kulishirikisha Bunge ndiyo sababu ya Rais kuishia kuzungukwa na Mawaziri mizigo (Washikaji).
Serikali kuhodhi sehemu kubwa ya madaraka na mamlaka ya ufanyaji maamuzi na utekelezaji mipango ya kimaendeleo imesababisha Wizara kuzidiwa na mizigo ya majukumu.Kwa kuelemewa huku na majukumu baadhi ya Mawaziri wasio na uwezo mzuri wa kiutawala wamejikuta wakilaumiwa na hata kuitwa mizigo na Wananchi waliochoshwa na uzembe wa Viongozi wetu.
Ili kuondokana na matatizo haya siku za usoni ni budi Katiba Mpya ijayo ikasimishe sehemu kubwa ya madaraka katika serikali za Mikoa ili kuipungizia lundo la majukumu serikali kuu na pia ili kupeleka maendeleo haraka Mikoani.
Pia Bunge letu lihusishwe kwa karibu katika kuwathibitisha Wateule mbalimbali wa Rais.
Tatizo kubwa hapa ni jinsi hawa Mawaziri wanavyopatikana kwani wanateuliwa moja kwa moja na Rais bila ya kulishirikisha Bunge ndiyo sababu ya Rais kuishia kuzungukwa na Mawaziri mizigo (Washikaji).
Serikali kuhodhi sehemu kubwa ya madaraka na mamlaka ya ufanyaji maamuzi na utekelezaji mipango ya kimaendeleo imesababisha Wizara kuzidiwa na mizigo ya majukumu.Kwa kuelemewa huku na majukumu baadhi ya Mawaziri wasio na uwezo mzuri wa kiutawala wamejikuta wakilaumiwa na hata kuitwa mizigo na Wananchi waliochoshwa na uzembe wa Viongozi wetu.
Ili kuondokana na matatizo haya siku za usoni ni budi Katiba Mpya ijayo ikasimishe sehemu kubwa ya madaraka katika serikali za Mikoa ili kuipungizia lundo la majukumu serikali kuu na pia ili kupeleka maendeleo haraka Mikoani.
Pia Bunge letu lihusishwe kwa karibu katika kuwathibitisha Wateule mbalimbali wa Rais.