FINDTRUEFAITH
Member
- Mar 24, 2011
- 83
- 86
Nimekuwa mfuatiliaji sana wa lugha yetu adhimu ya Kiswahili kupitia vyanzo mbali mbali.
Moja ya neno lisilopewa kipaumbele kwa kutamkwa mara kwa mara ingawa ni la muhimu ni neno "kiate."
Neno hili kwa mujibu wa wataalamu wa lugha ya Kiswahili ni; mtoto aliyefiwa na wazazi wote wawili, kwa maana ya baba na mama.
Wengi wamezoea kumuita mtoto alyefiwa na wazazi wote wawili kwamba ni yatima, jambo ambalo si kweli.
YATIMA: ni mtoto aliyefiwa na baba ila mama yake yuko hai. Kwa maana ya yule anayemtimizia mahitaji yake (a bread winner )
MKIWA: ni mtoto aliyefiwa na mama ila baba yake yu hai. Kwa maana ya yule aliyekaribu na mtoto na kumfariji kila wakati (a comforter)
Ndipo anakuja KIATE: aliyefiwa na wazazi wote wawili.
Tuna vituo vingi vya watoto yatima. Tukitumia neno hili moja tu la Yatima kuwatambulisha watoto hao, tuna maana watoto hao wamepoteza mzazi mmoja ambaye ni baba, lakini wanao mama zao, hata kama ukweli ni kwamba wamepoteza wazazi wote wawili kwa maana ya mtoa mahitaji na mfariji, ambayo hiyo ndiyo sababu ya kutafutiwa mtoa mahitaji na mfariji mwingine (social workers).
Vitabu vya dini vimetusaidia kuliongelea hili vizuri kuhusu yatima ni nani; na mkiwa ni nani.
Ndani ya Biblia katika kitabu cha Maombolezo 5:3 imeandikwa, " Tumekuwa yatima waliofiwa na baba; Mama zetu wamekuwa kama wajane."
Katika aya hii imeoneshwa kwamba yatima ni mtoto aliyefiwa na baba.
Kuhusu mkiwa, katika kitabu cha Injili ya Yesu kama Ilivyoandikwa na Mathayo, Sura ya 23: 37-38 amenukuliwa Yesu akiuelezea mji wa Yerusalemu kuachwa ukiwa, kwa sababu haukutaka kukusanywa kama vile kuku (tetea-kuku jike) anavyowakusanya vifaranga wake. Imeandikwa,
37 Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka!
38 Angalieni, nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa."
Ni kawaida nchi yoyote kuchukia sifa ya kike (she). Hapa kwa sababu Yesu alitakiwa apokelewe Yerusalemu kama mfalme wao walimkataa. Kila mfalme ana mji wake anaoutawala. Hapa anaelezea nyumba yao kuwa ukiwa yaani bila mfalme.
Maneno mawili haya; yatima na mkiwa yanafahamika sana, lakini hili la kiate halifahamiki sana, ingawa ni neno lililojitokeza kutokana na maendeleo ya kukua kwa Kiswahili. Profesa Abdallah Safari analijua vizuri neno hili.
Ninawaomba wahusika na wadau kulitangaza zaidi neno hili ili lijualikane vyema kwa watumiaji wa lugha yetu adhimu ya Kiswahili.
Jioni njema!
Moja ya neno lisilopewa kipaumbele kwa kutamkwa mara kwa mara ingawa ni la muhimu ni neno "kiate."
Neno hili kwa mujibu wa wataalamu wa lugha ya Kiswahili ni; mtoto aliyefiwa na wazazi wote wawili, kwa maana ya baba na mama.
Wengi wamezoea kumuita mtoto alyefiwa na wazazi wote wawili kwamba ni yatima, jambo ambalo si kweli.
YATIMA: ni mtoto aliyefiwa na baba ila mama yake yuko hai. Kwa maana ya yule anayemtimizia mahitaji yake (a bread winner )
MKIWA: ni mtoto aliyefiwa na mama ila baba yake yu hai. Kwa maana ya yule aliyekaribu na mtoto na kumfariji kila wakati (a comforter)
Ndipo anakuja KIATE: aliyefiwa na wazazi wote wawili.
Tuna vituo vingi vya watoto yatima. Tukitumia neno hili moja tu la Yatima kuwatambulisha watoto hao, tuna maana watoto hao wamepoteza mzazi mmoja ambaye ni baba, lakini wanao mama zao, hata kama ukweli ni kwamba wamepoteza wazazi wote wawili kwa maana ya mtoa mahitaji na mfariji, ambayo hiyo ndiyo sababu ya kutafutiwa mtoa mahitaji na mfariji mwingine (social workers).
Vitabu vya dini vimetusaidia kuliongelea hili vizuri kuhusu yatima ni nani; na mkiwa ni nani.
Ndani ya Biblia katika kitabu cha Maombolezo 5:3 imeandikwa, " Tumekuwa yatima waliofiwa na baba; Mama zetu wamekuwa kama wajane."
Katika aya hii imeoneshwa kwamba yatima ni mtoto aliyefiwa na baba.
Kuhusu mkiwa, katika kitabu cha Injili ya Yesu kama Ilivyoandikwa na Mathayo, Sura ya 23: 37-38 amenukuliwa Yesu akiuelezea mji wa Yerusalemu kuachwa ukiwa, kwa sababu haukutaka kukusanywa kama vile kuku (tetea-kuku jike) anavyowakusanya vifaranga wake. Imeandikwa,
37 Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka!
38 Angalieni, nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa."
Ni kawaida nchi yoyote kuchukia sifa ya kike (she). Hapa kwa sababu Yesu alitakiwa apokelewe Yerusalemu kama mfalme wao walimkataa. Kila mfalme ana mji wake anaoutawala. Hapa anaelezea nyumba yao kuwa ukiwa yaani bila mfalme.
Maneno mawili haya; yatima na mkiwa yanafahamika sana, lakini hili la kiate halifahamiki sana, ingawa ni neno lililojitokeza kutokana na maendeleo ya kukua kwa Kiswahili. Profesa Abdallah Safari analijua vizuri neno hili.
Ninawaomba wahusika na wadau kulitangaza zaidi neno hili ili lijualikane vyema kwa watumiaji wa lugha yetu adhimu ya Kiswahili.
Jioni njema!