ntamaholo
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 12,906
- 6,909
Kwa takwimu hizi za corona, naishauri serikali iweke kumbukukumbu sawa. Ianze kutoa taarifa za:-
1. Waliochanja
2. Waliolazwa na kama wamechanja au hawajachanja.
3. Waliofariki ieleweke wazi kama wamechanja au hawajachanja.
Iwapo jamii itaona waliochanja hawapo hospitalini kwa corona, watachanja bila kutumia ushawishi maana wataelewa umuhimu wa kuchanja.
Iwapo jamii itatambua kuwa vifo vingi vinavyotokea ni kwa watu ambao hawajachanja, hakuna atakayetumia nguvu tena kuhamasisha uchanjanji, watu watazitafta wenyewe na hata kulipia maana uhai hauna mbadala.
Usiri wa taarifa za chanjo, unaathiri zoezi la uchanjaji.
1. Waliochanja
2. Waliolazwa na kama wamechanja au hawajachanja.
3. Waliofariki ieleweke wazi kama wamechanja au hawajachanja.
Iwapo jamii itaona waliochanja hawapo hospitalini kwa corona, watachanja bila kutumia ushawishi maana wataelewa umuhimu wa kuchanja.
Iwapo jamii itatambua kuwa vifo vingi vinavyotokea ni kwa watu ambao hawajachanja, hakuna atakayetumia nguvu tena kuhamasisha uchanjanji, watu watazitafta wenyewe na hata kulipia maana uhai hauna mbadala.
Usiri wa taarifa za chanjo, unaathiri zoezi la uchanjaji.