X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,809
Watanzania Italy wanasikitika kutangaza kifo cha Ndugu MOHAMED ABDUL SHAKUR (PAMA) kilichotokea 5th Jan asubuhi katika hospitali ya SAN GIOVANNI DI DIO E RUGGI D'ARAGONA" SALERNO.
Mwili wa marehemu utaondoka Rome siku ya jumanne tarehe 13/1/2009 kupitia Amsterdam kwa ndege ya shirika la KLM, na unatarajiwa kuwasili nyumbani Dar kwa mazishi siku ya jumatano 14/01/2009 saa 22:40. na ndege ya shirika la KLM namba 569.
Mwenyekiti wa jumuiya ya Watanzania Italy, kwa niaba ya uongozi na watanzania wote Italy, anatoa salam za rambirambi kwa wazazi na ndugu wa marehemu nyumbani na popote walipo, zimepokewa taarifa hizi kwa masikitiko makubwa na waunaungana na wafiwa katika wakati huu mgumu wa maombolezo.
Mungu ailaze roho yake mahala pema.
Amin.
Watanzania Italy
Picha na Habari zaidi Fungua Hapa Watanzania Italy