Taarifa za kuonekana kwa Ben, na hekaya za "kikaratasi" ofisi za MwanaHALISI

Malisa Godlisten

JF-Expert Member
Jan 20, 2010
201
1,534
Mwanahalisi waliweka kidokezo wiki iliyopita kuwa Ben anaonekana mtaani na kwenye vijiwe vya kahawa. Kisha wakamnukuu mjumbe mmoja wa kamati kuu aliyedai kuwa "Ben kajificha ili kujitafutia umaarufu wa kisiasa"

Wakaahidi kwamba toleo la jumatatu ya leo Januaru 02, 2017 wangekuja na taarifa kamili. Kabla ya taarifa hiyo nilihoji mambo machache kuhusu kidokezo hicho cha habari. Nikahoji Ben ameonekana mtaa gani (vijiwe gani vya kahawa)? Lini? Akiwa na nani? Aliyemuona ni nani? Na mjumbe wa kamati kuu aliyesema Ben kajificha ni nani?

Baada ya kuhoji nikapokea maoni tofauti. Baadhi wakisema MwanaHalisi hawajui Ben alipo ila habari hiyo ni "kick" ya kuuza gazeti, na wengine wakasema tusihukumu kabla habari yenyewe kutoka. Tusubiri habari kamili ili tuweze kuhoji tukiwa na taarifa za kutosha.

Mhe.Kubenea alinitafuta kwa simu na tukaongea kwa kirefu kuhusu habari hiyo. Moja ya mambo aliyoniambia Kubenea ni kwamba, Kwanini sikusubiri habari hiyo itoke ndipo nitoe maoni? Nawezaje kutoa maoni kwenye kidokezo cha habari badala ya kusubiri habari kamili.

Hatimaye leo nimesoma habari kamili kwenye gazeti la MwanaHalisi kama ilivyokua ikisubiriwa na wengi. Kama ambavyo wengi tukitegemea gazeti la leo lingejibu maswali yote muhimu niliyouliza wiki jana. Yani Ben ameonekana mtaa gani? Lini? Alionwa na nani? Kwanini aliyemuona hakutoa taarifa polisi? Kwanini Ben ajifiche mtaani na kuiweka familia yake, chama chake na marafiki zake kwenye taharuki? Ben analindwa na intelijensia gani kiasi kwamba anaweza kujificha na Polisi wakashindwa kumpata?

Maswali haya nilitegemea yajibiwe kwa ufasaha kupitia MwanaHalisi ya leo. Lakini MwanaHalisi wameshindwa kujibu hata swali moja kati ya hayo. Yani wameongeza maswali badala ya kujibu maswali. Inaonekana ilikua mbinu ya kuuza gazeti.

MwanaHalisi wanadai taarifa za Ben kuonekana mtaani wamezipata kwenye andiko la mkono (kikaratasi) lilioachwa ofisini kwao mtaa wa Kasaba, Kinondoni na mtu asiyejulikana. Yani kuna mtu asiyejulikana alienda na kikaratasi akakiweka chini ya mlango ofisi za MwanaHalisi.

Kikaratasi hicho kinasomeka "Hamumfahamu Saanane. Sisi tunajua alipo. Wala hatuoni anayetishia maisha yake. Kuna wanaodai kauawa, ni waongo. Kuna kitu wanaandaa, kaa chonjo."

Kwahiyo eti wakatumia kikaratasi hicho kama source ya habari yao. Kikaratasi kilichowekwa na mtu asiyejulikana kinageuka kuwa credible source ya gazeti. Haya ni Maajabu.!

Yani gazeti kubwa lenye heshima kubwa kama MwanaHalisi linaacha kuamini vyanzo vya uhakika linakimbilia kuamini vikaratasi vilivyowekwa na mtu asiyejulikana? Hii ni aibu.

Mhe.Mbowe akiwa mkoani Mbeya alisema Ben ametekwa na hapendi kuongelea sana suala hilo ili watekaji wasije kumdhuru. Inaonekana MwanaHalisi hawakuamini taarifa hiyo ya Mbowe.

Lissu katika mkutano wake na wanahabari akasema inawezekana Ben anashikiliwa na dola kutokana na maandiko yake ya kukosoa serikali hasa elimu ya JPM. Lissu akafika mbali na kueleza kuwa anajua maeneo jijini Dar yanayotumika kutesa wakosoaji wa serikali, na akahofia huenda Ben yumo humo. Inavyoonekana MwanaHalisi pia hawakuamini taarifa za Lissu.

Waziri Mwigulu Nchemba nae akatoa tamko kuhusu Ben akidai ni rafiki yake, akisema anasikitishwa na taarifa za kupotea kwake na kwamba serikali inafanya uchunguzi. Lakini inaonekana MwanaHalisi hawakuziamini pia taarifa hizi.

Jeshi la Polisi makao makuu, kupitia kwa Kamishna Robert Boaz, December 21 mwaka huu lilitoa taarifa kuwa wanafanya uchunguzi juu ya taarifa za kupotea kwa Ben. Sikusikia MwanaHalisi wakisema kitu kuhusu hili.

Lakini cha ajabu wamekuja kuamini kikaratasi kilichowekwa na mtu asiyejukikana. Yani hawakuamini taarifa ya Mbowe, hawakuamini maelezo ya Lissu, hawakuamini taarifa ya jeshi la polisi, hawakuamini taarifa ya Mhe.Mwigulu, lakini wamekuja kuamini kikaratasi kilichowekwa ofisini kwao na mtu asiyejulikana. Ridiculous.!!

Yani taarifa ya kikaratasi zimepewa uzito kuliko taarifa iliyotolewa na Mhe.Mbowe, Mhe.Mwigulu, Jeshi la Polisi na Mhe.Lissu.?? Haya ni Maajabu ya kikaratasi. Kwanini MwanaHalisi waamini zaidi taarifa za kikaratasi kilichoandikwa na watu wasiojulikana kuliko kuamini taarifa rasmi zilizotolewa na vyombo vinavyoshughulikia suala hilo? Hivi kati ya kikaratasi kilichookotwa ofisi na Lissu nani anapaswa kuaminiwa?

Kikaratasi ambacho MwanaHalisi wamekitumia kama source ya habari yao kimeongeza maswali badala ya kujibu maswali ya awali. Kwanini kikaratasi hicho kipelekwe Mwanahalisi tu na sio media house nyingine kama Mwananchi, Majira etc? Kwanini waliokiweka wafiche identity zao? Kama kweli walimuona Ben mtaani kwanini hawakutaja hiyo mitaa?

Kama ofisi za Mwanahalisi zina walinzi usiku na mchana, iweje mtu aje na kikaratasi akiweke chini ya mlango bila kujulikana? Nadhani MwanaHalisi wanahitaji kujieleza vzr kuhusu ukweli wa kikaratasi hicho. Otherwise tutaamini kimeandikwa na watu wa humohumo ndani ili kupenyeza agenda yao kuhusu Ben, kisha kujifanya hawajui kilipotoka.

Nashauri Polisi wachunguze vizuri juu ya ukweli wa kikaratasi hicho. Huenda kuna mengi sana nyuma ya pazia kuhusu hicho kikaratasi.

Kwa ujumla habari ya leo kwenye MwanaHalisi kuhusu Ben imekua na impacts mbili kubwa.

[HASHTAG]#Mosi[/HASHTAG]: imepunguza heshima ya gazeti mbele ya jamii. Wapo watu wameanza kulipuuza gazeti hili baada ya kusoma habari ya leo. Baada ya gazeti kutoa tuhuma kwamba Ben yupo mtaani, wengi walitegemea leo wapate majibu yko wapi, kwahiyo kitendo cha gazeti hilo kushindwa kudhibitisha madai yake, na badala yake wakaja na hekaya za kikaratasi na kujifanya kimetoka kwa watu wasiojulikana. Heshima ya gazeti imepungua.

[HASHTAG]#Pili[/HASHTAG]; habari ya leo imefanya watu wahisi imeandikwa kwa msukumo wa chuki kutokana na tofauti ambazo zimewahi kuwepo kati ya Ben na Kubenea ambaye ni mkurugenzi wa gazeti hilo. Hii ni kwa sababu badala ya gazeti hilo kueleza Ben alipo, limeeleza mambo mengi negative kuhusu Ben ambayo hayakua na ulazima wa kuandikwa leo. Kwa mfano katika aya ya 8 &9 mwandishi ameeleza kuwa Ben aliwahi kumrekodi Dr.Slaa, na kutaka kumpa sumu Zitto Kabwe. Tuhuma hizi za miaka 8 iliyopita hazikua na sababu ya kuandikwa leo.

Kama agenda kuu ni kujua Ben alipo, kwanini wamechomekea mambo yasiyohusiana na agenda hiyo? Mara Ben alitaka kumuwekea sumu Zitto, mara Ben alimrekodi Dr.Slaa, so what?? Hayo yanahusiana nini na kupotea kwa Ben? Hivi watu wakisema habari hii imeandikwa kwa msukumo wa chuki binafsi MwanaHalisi watabisha?

Nashauri menejimenti ya MwanaHalisi ijitafari upya kuhusu siala hili. Tunalijua MwanaHalisi kama gazeti bingwa la habari za uchunguzi, sio MwanaHalisi ya udaku kama ya leo.

Tulitegemea habari ya leo ihitimishe mjadala wa Ben. Tulitegemea kupitia gazeti la leo umma wa watanzania ujue Ben amejificha wapi, kwanini ajifiche? Alionekana lini? Sio kutuletea hekaya za "kikaratasi" kilichoandikwa na watu wasiojulikana. Hii ni aibu.

Gazeti kubwa la uchunguzi lenye heshima kama MwanaHalisi kutegemea source ya vikaratasi kutoka kwa watu wasiojulikana, ni aibu kubwa. By the way kama mnakiri kikaratasi kimewekwa na watu wasiojulikana it means mmeshindwa kujua aliyeandika hicho kikaratasi hicho. Sasa je mtawezaje kumjua aliyemficha Ben, kama mmeshindwa kumjua mwandishi wa kikaratasi? Jitafakarini upya. Mmeanza kupoteza heshima yenu kubwa mliyoijenga kwa jamii kwa muda mrefu. Jisahihisheni. Acheni chuki kwenye mambo yanayohusu uhai wa mtu. Bado mna nafasi ya kujisahihisha, itz not too late yet.!

[HASHTAG]#BringBackBenAlive[/HASHTAG].!

Malisa GJ
 
Malisa asubuhi niliandika hivi:
"Kubenea be serious, unajishushia heshima mbele ya jamii. Wewe ni Mbunge! Una dhamana, usiwe kama Lumpen,"
This is a very sensitive issue sikutegemea mtu kuandika mambo ya "vikaratasi", shame upon him! Mtu mzima na taaluma yote unaleta utani, kama mwandishi wa vijiweni!
Nyie mlio karibu naye mwambie, msimwonee aibu!
 
Wote wauni Si Kubenea,Mbowe,Mwigulu....

Hakuna aliyetoa majibu ya kuridhisha ...........

Tanzania imegeuka nchi ya propaganda na kutafuta publicity......

Si watawala si wapinzani wote wana play foolish politics..............

Kubenea nilimtoa toka Gazeti lake lilipomsafisha Lowassa..............
 
Malisa asubuhi niliandika hivi:
"Kubenea be serious, unajishushia heshima mbele ya jamii. Wewe ni Mbunge! Una dhamana, usiwe kama Lumpen,"
This is a very sensitive issue sikutegemea mtu kuandika mambo ya "vikaratasi", shame upon him! Mtu mzima na taaluma yote unaleta utani, kama mwandishi wa vijiweni!
Nyie mlio karibu naye mwambie, msimwonee aibu!
Namwonea huruma Malisa maana katika hili sakata ndiye atageuka mhanga kuliko hata Ben mwenyewe. Malisa kupitia UTG ndo alianza kuichafua serikali kwa habari ambayo hakuwa na uhakika nayo. Kwa kitendo hicho anakabiliwa na kosa la kuchapisha habari za uongo zenye kupotosha umma.

Kwa upande wa pili, Malisa sasa anagombana na Kubenea. Kitendo hicho kinampa hatari mbili. Hatari ya kwanza, Malisa atachukiwa na viongozi wa juu wa chadema waliomruhusu Mwanahalisi atoe hii habari. Kitendo hicho watamuona kuwa mkaidi hivyo asitegemee kuifaidi chadema labda siku za idd. Hatari ya pili, malisa ategemee mvua ya matusi kupitia mwanahalisi.

All the Odds of Malisa gonna be uncovered. Image ya malisa inaenda kuharibika kuliko ya Ben mwenyewe. Hakika Malisa atakuwa mhanga wa hili jambo kuliko Ben mwenyewe.
 
kwa kifupi bongo hatuna waandishi wa habari. tuna makanjanja tu. [HASHTAG]#WaandishiWaHabariUchwala[/HASHTAG]
 
Back
Top Bottom