Taarifa ya wazi kwa waziri magufuli, tanroads na mhe.john mnyika.

Sendeu

Member
Jun 29, 2009
59
2
Natumaini hamjambo wana JF naomba wahusika haswa Waziri wetu mpendwa wa Ujenzi Magufuli mtusaidie sisi watumiaji wa barabara ya Mbezi tank Bovu hadi Goba-Kimara.
Kuna bango la TANROADS limewekwa pale Bagamoyo Road kuwa barabara ya Goba-KImara itakarabatiwa lakini hadi sasa hakuna chochote kilichofanyika,mashimo ndo yamejaa,mvua ikinyesha hakufai usafiri unakuwa wa kero nk.
Jaman tusaidieni nasi ni walipa kodi kama wengine tumechoka.Barabara hii yaweza kuwa suluhisho la foleni zinazokera hapa jijini DSM!
Ipo pia barabara ya kutoka Makongo juu kupitia mto mbezi hadi Goba Mwisho ni barabara nzuri tu japo ni rafu ila tatizo lipo kwenye kuvuka mto mbezi hakuna daraja watu wanavuka kwa kudra za mwenyezi mungu kila siku magari yanakwama pale yani ni tabu tupu ndugu zanguni tusaidieni!!!!!
Kuna stor za kila aina kuhusu Ujenzi wa hili Daraja mara pesa zipo tayari,mara mkandarasi anatafutwa nk Mhe.Magufuli tunakuamini toa msimamo juu ya barabara hizi ili wananchi tuwe na amani!!!
Mhe.Mnyika fanya kweli kaka 2015 bado tunakuhitaji tatua hizi kero ukishirikiana na Magufuli na Manispaa husika! tunakuamini na tunakutegemea.
Shukrani!
 
Sendeu,
Hayo ndiyo maisha bora kwa kila mtunzania.
Ila nawasifu mmewapiga chini hao mafisadi ingawa inashangaza hata Shinyanga ambayo ni mwisho std 7 kitaifa ila wameamka na kuangusha mafisadi majimbo matano.

Ukitaka kujua kama hawa jamaa wamechoka kuumiza kicha kwa ajili ya maendeleo yetu ile barabara inayotoka Wazo kuja Madale kwa kawawa ilifaa ziwe TWO ways ili hizo za GOBA sijui Tangibovu zikonekti kule lakini barabara kuu ya Mwisho ni Mandele baada ya hapo hakuna hata za mtaa.
\
Yanaona Dar imeishia hapo hapo.
 
umetaja madale umenikumusha mtendaji kaniuzia mbuzi kwenye gunia ..kiwanja kimoja tumeuziwa watu wa 3
 
Back
Top Bottom