Habari waungwana,
Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali(CAG) anawasilisha ripoti yake kwa wanahabari leo. Fuatana nami kujua atachosema.
======
Mkaguzi anasema ripoti inaonyesha fedha nyingi zaidi zilitumika katika matumizi ya kwaida kuliko matumizi ya maendeleo. Ukusanyaji ni mdogo wa maduhuri katika kusimamia bajeti. Bila kutumia mikopo, serikali ingeweza kugharamia asilimia 62 pekee ya bajeti yake.
Assad: Deni la Taifa limefikia trilioni 41 Juni 2016 kulinganisha na trilioni 33 2015 na kiasi hiko hakijajumuisha trilioni nane ambalo ni deni katika hifadhi za jamii, serikali iliadi kutoa non cash bond na haijatimiza.
Deni la taifa linakuwa kwa kasi, zaidi ya 20% ikimaanisha baada ya miaka mitano litakuwa mara mbili. Sio vizuri deni kukua kwa namna hii.
Serikali haikuwasilisha michango kwa mifuko ya hifadhi ya jamii ya bilioni 400, si busara serikali kuchelewesha kwani hata wastaafu watacheleweshewa.
Malipo ya mishahara ya bilioni 9.8 yaliyofanyika kwa wafanyakazi waliofariki, watu wamelipwa na kodi zimekatwa, serikali ifanye juhudi kuhakikisha database yao iko updated.
Mishahara kwa kawaida isipochokuliwa benki inaitwa unclaimed salaries na inatakiwa kurejeshwa hazina lakini tumefatilia hairejeshwi na mabenki.
Pia Assad kazungumzia baadhi ya taasisi kukosa hati za malipo na kusema anazitaka kwani sheria inamruhusu kuzidai. Magari 2172 yametelekezwa ikiwa ni ongezeko la 88% kutoka mwaka 2015, amesema magari yaliyofikia ukomo wa matumizi bora kuuza kama ipo busara ya kuuza au kuzipa taasisi nyingine ambazo zinaweza kuyatumia.
Bilioni 24 imetumika bila kushindanisha tenda, serikali inatakiwa kufuata sheria ya manunuzi.
Vyama vya siasa tumeshindwa kufanya ukaguzi kwa sababu havifati sheria na vitatu havina hata akaunti benki.
Benki ya wanawake mtaji umekuwa eroded kwani sheria ya benki kuu ni lazima mtaji ufike bilioni tano na yenyewe haina hivyo haitakiwi kuendelea.
Twiga benki japo imechukuliwa na benki kuu lakini ilifikia hasi ya bilioni 19, walikuwa wapi wahusika mpaka kufika hapo.
TANESCO inapata hasara kwa sababu muundo wake hauko sahihi hasa kwenye kununua umeme wa dharura na mpango huo hauna tija katika nchi hii, tunaishauri kufanya uwekezaji kuachana na mpango wa dharura.
Kuna mradi uko chini ya Rubada na tunafikiri hana uwezo.
Mifuko ya pensheni ishuka uwekezaji umeshuka kutokana na kutokuwepo ufanisi wa kusimamia mikopo.
Kampuni zote za madini hazijawahi kulipa kodi kutokana na faida, inawezekana vipi kuendesha biashara kwa miaka 10 bila faida? Lazima tuangalia muda wa allowances tunazotoa kwa kampuni za madini. Nchi nyingine hazifanyi kama tunazofanya sisi. Anatolea mfano wa Botswana ambayo inatumia kipimo cha madini yanayotoka na sio muda, ambapo kipimo kikifika wanagawana nusu kwa nusu na serikali.
=======
Majibu ya Maswali
Assad: Bajeti ya mwaka uliopita haikutosha lakini mwaka huu tumepewa bajeti.
Assad: Kuna watu wanapoteza nafasi zao na wengine wanateuliwa, mwisho wa kukaimu ni miezi sita. Watu wanatakiwa kukumbusha mamlaka ya uteuzi kuteua nafasi, sisi hatuwezi kupokea hesabu za watu waliosaini kwa niaba baada ya miezi sita.
Assad: NSSF Kigamboni nakumbuka malipo yanatokana na uuzaji wa nyumba na mbia hajaendeleza hivyo hakuna nyumba za kuuza.
Assad: Pale ambapo mtu atashindwa kutimiza mapendekezo aliyokubali yeye mwenyewe, tutaomba mamlaka ya uteuzi impe kazi nyingine.
Assad: TANESCO itaendelea kula hasara kwa sababu sehemu pekee ni kupunguza gharama, bei zinadhibitiwa hivyo wanatakiwa kupunguza gharama na kwa maoni yangu wawekeze katika uzalishaji wa umeme.
Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali(CAG) anawasilisha ripoti yake kwa wanahabari leo. Fuatana nami kujua atachosema.
======
Mkaguzi anasema ripoti inaonyesha fedha nyingi zaidi zilitumika katika matumizi ya kwaida kuliko matumizi ya maendeleo. Ukusanyaji ni mdogo wa maduhuri katika kusimamia bajeti. Bila kutumia mikopo, serikali ingeweza kugharamia asilimia 62 pekee ya bajeti yake.
Assad: Deni la Taifa limefikia trilioni 41 Juni 2016 kulinganisha na trilioni 33 2015 na kiasi hiko hakijajumuisha trilioni nane ambalo ni deni katika hifadhi za jamii, serikali iliadi kutoa non cash bond na haijatimiza.
Deni la taifa linakuwa kwa kasi, zaidi ya 20% ikimaanisha baada ya miaka mitano litakuwa mara mbili. Sio vizuri deni kukua kwa namna hii.
Serikali haikuwasilisha michango kwa mifuko ya hifadhi ya jamii ya bilioni 400, si busara serikali kuchelewesha kwani hata wastaafu watacheleweshewa.
Malipo ya mishahara ya bilioni 9.8 yaliyofanyika kwa wafanyakazi waliofariki, watu wamelipwa na kodi zimekatwa, serikali ifanye juhudi kuhakikisha database yao iko updated.
Mishahara kwa kawaida isipochokuliwa benki inaitwa unclaimed salaries na inatakiwa kurejeshwa hazina lakini tumefatilia hairejeshwi na mabenki.
Pia Assad kazungumzia baadhi ya taasisi kukosa hati za malipo na kusema anazitaka kwani sheria inamruhusu kuzidai. Magari 2172 yametelekezwa ikiwa ni ongezeko la 88% kutoka mwaka 2015, amesema magari yaliyofikia ukomo wa matumizi bora kuuza kama ipo busara ya kuuza au kuzipa taasisi nyingine ambazo zinaweza kuyatumia.
Bilioni 24 imetumika bila kushindanisha tenda, serikali inatakiwa kufuata sheria ya manunuzi.
Vyama vya siasa tumeshindwa kufanya ukaguzi kwa sababu havifati sheria na vitatu havina hata akaunti benki.
Benki ya wanawake mtaji umekuwa eroded kwani sheria ya benki kuu ni lazima mtaji ufike bilioni tano na yenyewe haina hivyo haitakiwi kuendelea.
Twiga benki japo imechukuliwa na benki kuu lakini ilifikia hasi ya bilioni 19, walikuwa wapi wahusika mpaka kufika hapo.
TANESCO inapata hasara kwa sababu muundo wake hauko sahihi hasa kwenye kununua umeme wa dharura na mpango huo hauna tija katika nchi hii, tunaishauri kufanya uwekezaji kuachana na mpango wa dharura.
Kuna mradi uko chini ya Rubada na tunafikiri hana uwezo.
Mifuko ya pensheni ishuka uwekezaji umeshuka kutokana na kutokuwepo ufanisi wa kusimamia mikopo.
Kampuni zote za madini hazijawahi kulipa kodi kutokana na faida, inawezekana vipi kuendesha biashara kwa miaka 10 bila faida? Lazima tuangalia muda wa allowances tunazotoa kwa kampuni za madini. Nchi nyingine hazifanyi kama tunazofanya sisi. Anatolea mfano wa Botswana ambayo inatumia kipimo cha madini yanayotoka na sio muda, ambapo kipimo kikifika wanagawana nusu kwa nusu na serikali.
=======
Majibu ya Maswali
Assad: Bajeti ya mwaka uliopita haikutosha lakini mwaka huu tumepewa bajeti.
Assad: Kuna watu wanapoteza nafasi zao na wengine wanateuliwa, mwisho wa kukaimu ni miezi sita. Watu wanatakiwa kukumbusha mamlaka ya uteuzi kuteua nafasi, sisi hatuwezi kupokea hesabu za watu waliosaini kwa niaba baada ya miezi sita.
Assad: NSSF Kigamboni nakumbuka malipo yanatokana na uuzaji wa nyumba na mbia hajaendeleza hivyo hakuna nyumba za kuuza.
Assad: Pale ambapo mtu atashindwa kutimiza mapendekezo aliyokubali yeye mwenyewe, tutaomba mamlaka ya uteuzi impe kazi nyingine.
Assad: TANESCO itaendelea kula hasara kwa sababu sehemu pekee ni kupunguza gharama, bei zinadhibitiwa hivyo wanatakiwa kupunguza gharama na kwa maoni yangu wawekeze katika uzalishaji wa umeme.