Taarifa ya BAVICHA kuhusu Mikutano ya CCM Dodoma

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,898
Ndugu waandishi wa habari kwanza tunawashukuru kwa kazi kubwa mliyoifanya kwa kuwaeleza Watanzania adhima yetu ya kwenda Dodoma, katika kuhakikisha BAVICHA tunaisimamia kauli Jeshi la Polisi na ya Mhe. Raisi, na kulisaidia jeshi la Polisi kuzuia mikutano ya kisiasa kwa vyama vyote hadi mwaka 2020 tukianza na mkutano haramu wa CCM hapo tarehe 23 July 2016.

Tunaendelea na msimamo wetu kuamini mkutano huo sio halali,kwakuwa ni Mkusanyiko wa Kisiasa ambao Mhe. Raisi na Jeshi la Polisi waliikataa vinginevyo watoke hadharani kukanusha Agizo na msimamo wao ulioathiri tayari vyama vya upinzani vikiwemo CHADEMA na ACT kwa kuzuiwa kukutana.

Sisi BAVICHA tunaheshimi kauli ya Kiongozi wetu mkuu wa chama,aliyotuomba tusiende Dodoma, kauli hii imeipa nafuu kubwa CCM kwakuwa hawakuwa na ubavu wa kutuzuia tusizuie mkutano wao.

Tulijipanga kila kona ya nchi hii,na hata jeshi la Polisi lisingeweza kutuzuia katika kutekeleza azima yetu,ya kutaka haki na usawa wa Kidemokrasia katika nchi hii ya Kidemokrasia.

Sasa basi,baada ya M/kiti kutuomba vijana wake tusiende Dodoma, sasa tunaamua kuja na plan B,ambapo hatutaenda Dodoma lakini hatutaruhusu mkutano wa CCM ufanyike mpaka pale Serikali itakapotoa kauli ya haki sawa za Kidemokrasia kwa kila chama,kufanya siasa maana hivi tunavyoongea CCM wao wanafanya mikutano ya hadahara na wengine wanazuiwa.

Tunayo taarifa ya Baadhi ya mawaziri na wabunge wa CCM wao wanafanya mikutano ya hadhara katika majimbo mbali mbali,na picha za matukio hayo tunazo kwa ushahidi hivyo tukashitaki wapi?

Tunazo taarifa za Wakuu wa wilaya wakifanya mikutano ya hadhara na wanachi,hivi kati ya mkuu wa wilaya na vyama vya siasa nani mwenye mamlaka ya kufanya siasa!??

Tunaomba Watanzania waone na wapaze sauiti jinsi nchi yao inavyoongozwa Kidikteta,na kukosa usawa.Leo Dodoma kumepelekwa Polisi kutoka katika mikoa ya Morogoro, Singida,Dar es salaam na Iringa wakiwa na kila aina ya Vifaa vya kivita.

Kwa Mara ya kwanza katika historia ya nchi hii Polisi wengi wasio na Idadi wakiwa na silaha nzito za kivita wanaenda kulinda mkutano wa Kisiasa,hii haijawahi kutokea.

Mtakumbuka Polisi wamewahi kuzuia mikutano mingi sana ya CHADEMA kwa kigezo kutokea machafuko na hali ya usalama ni ndogo,lakini hii imekuwa tofauti sana kwa upande wa Ccm wao usalama ni mdogo sana kupita maelezo katika mkutano wao wa tarehe 23 July,lakini vimepelekwa mpaka vifaru vya jeshi kuimarisha usalama.

Hii ni double standard ya hali ya juu,inayooneshwa na jeshi la Polisi kwa vyama vya siasa na huwa mara nyingine tunasema Polisi wanatumika na Ccm na huu ni ushahidi wa kwanza mkubwa kabisa.

Polisi wa nchi hii wako radhi wao wafe lakini Ccm isiguswe na wapo radhi hata kuua wapinzani ili Ccm iendelee kuwa madarakani,uko wapi usawa wa Kidemokrasia??? Uko wapi weledi wa kiutendaji wa jeshi letu la Polisi?.

UNYANYASAJI WA HAKI ZA BINADAMU.

Tokea BAVICHA tumatangaza kwenda Dodoma, majeshi yaliyopelekwa Dodoma kuisaidia Ccm yamekuwa yakifanya unyanyasaji mkubwa kwa raia,wamekuwa wakikamata wananchi hivyo na kuwaweka ndani bila kuwafungulia kesi,na jina la mtu aliyekamatwa tokea siku ya jumatano mpaka Leo hajafunguliwa kesi,wala kufikishwa Mahakamani na hata mawakili wanapoenda kujua hatima yake wanafukuzwa na Polisi.

Polisi wanaingia katika Nyumba vya kulala wageni usiku,kufanya ukaguzi,kinadada wanadhalilika kwakuwa wengine wanakutwa uchi wa mnyama na Polisi wa kiume,huu ni unyanyasaji mkubwa unaofanywa na jeshi la polisi Dodoma.


Sasa tunawaomba vijana wetu wote nchi nzima watulie na wasubirie maamuzi ya kikao kikubwa cha kamati ya Utendaji,kitakachokaa siku ya jumatano ya tarehe 20.07.2016 Kukutana na M/kiti wetu tukiwa tayari na Plan B ya kuipigania Demokrasia ya Taifa letu.

Imetolewa July 16

M/kiti BAVICHA Taifa
 

Attachments

  • IMG-20160716-WA0035.jpg
    IMG-20160716-WA0035.jpg
    66.1 KB · Views: 78
Bavicha mmekua kama mtoto wa kambo, kila siku mnaonewa nyie. Hamjiulizi labda kuna kitu mnafanya sivyo kinachosababisha hiyo hali.
Unanitafutia BAN.

Hoja za msingi zimewekwa hapo, jinsi ambavyo chama A kinapata haki ile ile ambayo chama B kinanyimwa. hayo yoooote hukuyaona, umekuja kucomment utumbo. Kwa kifupi unawadhalilisha wanawake wa nchi hii, unajenga taswira mbaya.
 
Unanitafutia BAN.

Hoja za msingi zimewekwa hapo, jinsi ambavyo chama A kinapata haki ile ile ambayo chama B kinanyimwa. hayo yoooote hukuyaona, umekuja kucomment utumbo. Kwa kifupi unawadhalilisha wanawake wa nchi hii, unajenga taswira mbaya.

Freedom of speech, that is my opinion and I am entitled to it like you are entitled to yours.

Siwezi kukubaliana na kila unachoamimi kwa vile tu wewe unaamini hivyo. Si vizuri kufuata rai ya mtu kibubusa na sifuati rai kwenye hiyo taarifa kibubusa.

I am keeping in mind that even freedom has limits.
 
Ndugu waandishi wa habari kwanza tunawashukuru kwa kazi kubwa mliyoifanya kwa kuwaeleza Watanzania adhima yetu ya kwenda Dodoma, katika kuhakikisha BAVICHA tunaisimamia kauli Jeshi la Polisi na ya Mhe. Raisi, na kulisaidia jeshi la Polisi kuzuia mikutano ya kisiasa kwa vyama vyote hadi mwaka 2020 tukianza na mkutano haramu wa CCM hapo tarehe 23 July 2016.

Tunaendelea na msimamo wetu kuamini mkutano huo sio halali,kwakuwa ni Mkusanyiko wa Kisiasa ambao Mhe. Raisi na Jeshi la Polisi waliikataa vinginevyo watoke hadharani kukanusha Agizo na msimamo wao ulioathiri tayari vyama vya upinzani vikiwemo CHADEMA na ACT kwa kuzuiwa kukutana.

Sisi BAVICHA tunaheshimi kauli ya Kiongozi wetu mkuu wa chama,aliyotuomba tusiende Dodoma, kauli hii imeipa nafuu kubwa CCM kwakuwa hawakuwa na ubavu wa kutuzuia tusizuie mkutano wao.

Tulijipanga kila kona ya nchi hii,na hata jeshi la Polisi lisingeweza kutuzuia katika kutekeleza azima yetu,ya kutaka haki na usawa wa Kidemokrasia katika nchi hii ya Kidemokrasia.

Sasa basi,baada ya M/kiti kutuomba vijana wake tusiende Dodoma, sasa tunaamua kuja na plan B,ambapo hatutaenda Dodoma lakini hatutaruhusu mkutano wa CCM ufanyike mpaka pale Serikali itakapotoa kauli ya haki sawa za Kidemokrasia kwa kila chama,kufanya siasa maana hivi tunavyoongea CCM wao wanafanya mikutano ya hadahara na wengine wanazuiwa.

Tunayo taarifa ya Baadhi ya mawaziri na wabunge wa CCM wao wanafanya mikutano ya hadhara katika majimbo mbali mbali,na picha za matukio hayo tunazo kwa ushahidi hivyo tukashitaki wapi?

Tunazo taarifa za Wakuu wa wilaya wakifanya mikutano ya hadhara na wanachi,hivi kati ya mkuu wa wilaya na vyama vya siasa nani mwenye mamlaka ya kufanya siasa!??

Tunaomba Watanzania waone na wapaze sauiti jinsi nchi yao inavyoongozwa Kidikteta,na kukosa usawa.Leo Dodoma kumepelekwa Polisi kutoka katika mikoa ya Morogoro, Singida,Dar es salaam na Iringa wakiwa na kila aina ya Vifaa vya kivita.

Kwa Mara ya kwanza katika historia ya nchi hii Polisi wengi wasio na Idadi wakiwa na silaha nzito za kivita wanaenda kulinda mkutano wa Kisiasa,hii haijawahi kutokea.

Mtakumbuka Polisi wamewahi kuzuia mikutano mingi sana ya CHADEMA kwa kigezo kutokea machafuko na hali ya usalama ni ndogo,lakini hii imekuwa tofauti sana kwa upande wa Ccm wao usalama ni mdogo sana kupita maelezo katika mkutano wao wa tarehe 23 July,lakini vimepelekwa mpaka vifaru vya jeshi kuimarisha usalama.

Hii ni double standard ya hali ya juu,inayooneshwa na jeshi la Polisi kwa vyama vya siasa na huwa mara nyingine tunasema Polisi wanatumika na Ccm na huu ni ushahidi wa kwanza mkubwa kabisa.

Polisi wa nchi hii wako radhi wao wafe lakini Ccm isiguswe na wapo radhi hata kuua wapinzani ili Ccm iendelee kuwa madarakani,uko wapi usawa wa Kidemokrasia??? Uko wapi weledi wa kiutendaji wa jeshi letu la Polisi?.

UNYANYASAJI WA HAKI ZA BINADAMU.

Tokea BAVICHA tumatangaza kwenda Dodoma, majeshi yaliyopelekwa Dodoma kuisaidia Ccm yamekuwa yakifanya unyanyasaji mkubwa kwa raia,wamekuwa wakikamata wananchi hivyo na kuwaweka ndani bila kuwafungulia kesi,na jina la mtu aliyekamatwa tokea siku ya jumatano mpaka Leo hajafunguliwa kesi,wala kufikishwa Mahakamani na hata mawakili wanapoenda kujua hatima yake wanafukuzwa na Polisi.

Polisi wanaingia katika Nyumba vya kulala wageni usiku,kufanya ukaguzi,kinadada wanadhalilika kwakuwa wengine wanakutwa uchi wa mnyama na Polisi wa kiume,huu ni unyanyasaji mkubwa unaofanywa na jeshi la polisi Dodoma.


Sasa tunawaomba vijana wetu wote nchi nzima watulie na wasubirie maamuzi ya kikao kikubwa cha kamati ya Utendaji,kitakachokaa siku ya jumatano ya tarehe 20.07.2016 Kukutana na M/kiti wetu tukiwa tayari na Plan B ya kuipigania Demokrasia ya Taifa letu.

Imetolewa July 16

M/kiti BAVICHA Taifa
tamko feki. kiongozi mkuu wa chama na msaidizi wake wameshapiga marufuku uanaharakati. chama kime graduate tayari. nashangaa mnataka kutupotezea muda bure. nashauri muende kufuata ushauri na maagizo kutoka kwa Lowasa kwanza kabla hamjaja kwenye mitandao kuropoka ropoka. kuweni na adabu nyie watoto
 
tamko feki. kiongozi mkuu wa chama na msaidizi wake wameshapiga marufuku uanaharakati. chama kime graduate tayari. nashangaa mnataka kutupotezea muda bure. nashauri muende kufuata ushauri na maagizo kutoka kwa Lowasa kwanza kabla hamjaja kwenye mitandao kuropoka ropoka. kuweni na adabu nyie watoto

Kweli nifake
 
tamko feki. kiongozi mkuu wa chama na msaidizi wake wameshapiga marufuku uanaharakati. chama kime graduate tayari. nashangaa mnataka kutupotezea muda bure. nashauri muende kufuata ushauri na maagizo kutoka kwa Lowasa kwanza kabla hamjaja kwenye mitandao kuropoka ropoka. kuweni na adabu nyie watoto

naona umeandika utumbo.
 
Imeishasemekana cdm sio wanaharakati tena ni chama cha siasa, ni ccm B. Nyie Ba-vichaa hamjaelewa bado? Mentor wa chama ni EL aliyelelewa na kukuzwa ccm. Mbowe kamwelewa, ninyi hamtaki kumwelewa, mnajifanya ba-vichaa. Kwa tabia hii ya ukambale naiona cdm ikipasuka vipande vipande.
 
Freedom of speech, that is my opinion and I am entitled to it like you are entitled to yours.

Siwezi kukubaliana na kila unachoamimi kwa vile tu wewe unaamini hivyo. Si vizuri kufuata rai ya mtu kibubusa na sifuati rai kwenye hiyo taarifa kibubusa.

I am keeping in mind that even freedom has limits.
Limit hiyo inaishia wapi? Kuna alive juu ya Katiba, ili yy tu aongee atakacho na wengine tukae kimya?
 
Bavicha bhana!!! Wanakaa kimyaaaa siku wakiibuka utasikia operation, maandamano oh kupambana Na polisi. I wish ningepata fursa ya kutafiti IQ ya vijana 5000 waliosemekana kuwa tayari kwenda Dodoma .
 
Freedom of speech, that is my opinion and I am entitled to it like you are entitled to yours.

Siwezi kukubaliana na kila unachoamimi kwa vile tu wewe unaamini hivyo. Si vizuri kufuata rai ya mtu kibubusa na sifuati rai kwenye hiyo taarifa kibubusa.

I am keeping in mind that even freedom has limits.
Upumbavu ni upumbavu tu...usemwe hata kwa Kigiriki...lugha ya Aristotle na Plato.

Ulikuwa wa kwanza kuwashutumu UKAWA kuwa walalamishi kama watoto wa kambo, hapa povu linakutoka kwa kuwa nimekukosoa. Huu mchezo mamaangu, hauhitaji hasira...ungeyasemea nyumbani kwako chumbani yasingekosolewa na mtu.

That is my opinion...ulichoandika ni pumba. Kama unafikiri nimeandika pumba, feel free to say so. Karibu sana!
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom