Taarifa: Rais Kikwete aagiza bendera kupepea nusu mlingoti kwa siku tatu za maombolezo ya Kitaifa y

Huyo ameandika kitu asichojua kama ni kuomboleza waliomboleza siku nyingi zaidi ya tatu hizi,mimi nilikuwepo south africa kipindi hicho na maombolezo yalikua mpaka walipo zika Butiama.Kwa taarifa tu msiba wa Nyerere uliitikisa sana south africa na hata kabla hajafa Makanisa kote south africa ya watu weusi walikua wanafanya ibdada maalumu za kumuombea ili apone.Msemaji wa rais wakati huo alikua kila siku anatoa report kwa waandishi wa habari kuhusu mwalimu hali yake ilivyokua ikiendelea.Kulitokea malumbano makubwa sana ya vyombo vya habari wakati huo hasa vile vinavyomilikiwa na wazungu na vile vya waafrica.Wazungu walikua wakimponda na wengine wakipinga na kumuunga mkono sana.watu wengi waliokua wakimuunga mkono mwalimu walisema sera zake za uchumi zilishindwa sababu ya mbinu za nchi za Magharibi.

Kumbuka pia mwalimu ndiyo aliyekua mshauri mkubwa wa ANC wakati wa mazungumzo ya kumaliza ubaguzi wa rangi,kila hatua aliulizwa mwalimu na kuwaambia cha kufanya wakiwa ktk mazungumzo ya Kempton park.Hayo yote yalidhihilishwa na Rais Mbeki wakati wa moja ya ibada ya kumkumbuka Mwalimu siku Arobaini baada ya kifo chake ktk kanisa moja la katoliki mjini Pretoria. Mbeki alisema Mwalimu alikua anatuambia mambo ya kukubaliana na kukataa wakati wa mazungumzo na serikali ya makaburu. Lakini pia kumbuka kwamba ni Mwalimu aliyekua hata anawapa maagizo viongozi wa ANC kuja kupumzika ktk ktk mbuga za wanyama huko Arusha kuanzaia akina.

Hata mandela baada ya kuachana na winie alikuja kupumzika kisilisili mbugani huko Arusha na kuishi kama mtu wa kawaida na hakuna alie kua akijua pindi alipokua akitembea vijiji vya karibu.

Mbeki pia akiwa makamu wa Rais Mandela amewahi kumwambia aje kupumzika Tanzania baada ya kuomuona amefanya kazi kupumzika muda mrefu na alifanya hivyo.

Uhusiano wa Tanzania na South Africa ni mkubwa sana kama watu wengi wasivyojua vizuri.

mkuu umemaliza kila kitu
 
I bid farewell to our role
model and hero MADIBA tunafurahia maisha yako ya upiganaji na ushujaa
dunia na Binguni unaenda kuketi kwenye kiti cha enzi.

Wasio waungwana hakuna sababu ya kubeza salaam za mh Rais. Msiba wa Mzee
Mandela ni wa ulimwengu sasa nyie vichenchede mnauliza swala la
Tanzania kwenda kwenye mazishi. Unadhan huyo ni babu yako kule kijijini
amefariki anazikwa kama Ng'ombe? Serikali na nchi kwa ujumla lazima tuwe
na uwakilishi wa kutosha kwenye mazishi ya mzee MADIBA. RIP Nelson
Mandela

Hakukuwa na sababu yoyote ya kumtukana Babu yangu. He was a Great man by himself. By the way hakuzikwa kama ng'ombe. At least a handful of people who cared about him were there
 
If it werent for Winnie i would have married in Zanzibar. Nelson Mandela Amaan Stadium Zanzibar1990.
 
Hivi bendera kupepea nusu mlingoti ni ya taifa tu? Au hata bendera za vyama?
siyo bendera za vyama tu bali mpaka za yanga, mtibwa, wekundu wa bondeni na hata waganga wa kienyeji lazima ziwe nusu mlingoti.
 
R.V.P MY FARMER . Umepigana vita vilivyo vikali mwendo umeumaliza, imani umeilinda.nitaendelea kuenzi na kuiamini na kuisimamia kauli yako uliyowah kusema;(KURUDISHA MAPAMBANO NYUMA NI KOSA AMBALO KIZAZI KIJACHO HAKITA TUSAMEHE)

R.V.P ndo nini mkuu? Au ni yule wa Man U?
 
Alisema Kuwa Haamini Kama Nyerere Ameondoka, Na Kwa Kuwa Haamini Hawezi Kuja. Akadai Kuwa Iwapo Ataiona Maiti Ya Myerere Nayeye Ni Lazima Angekufa Papo Hapo Na Kusababisha Msiba Usio Tamkika. Nafikiri Hakikosea Mkuu!

Pia wakati ule alikuwa dhofle hali sana. Mpaka aliliona kombe la dunia, siku amini.
 
Pia hata sisi wananchi wa KIVULE DAR TZ tunaungana na wananchi wa south africa ktk wakati huu mgumu wa kuondokewa na MZEE WETU MZEE NELSON MADIBA MANDELA mungu ailaze roho ya marehemu mahala pena peponi AMENI
 
Hatujikombi kwa MTU but we use utu chungeni fikra zetu mnapocoment msiwe kama mapaka ya bar jmn aaaah
 
NCHI ZOTE TAJIRI DUNIANI ZIMEPEPERUSHA BENDERA NUSU MLINGOTI. magazeti yote ya Newsweek na Time yameisha toa toleo maalum la mandela na maisha yake. television zote muhimu duniani zinamtangaza mandela masaa 24. kipindi hiki makampuni makubwa yote yanatengeneza kitu kiitwacho, survenir( vitu kama vikombe vyenye picha ya mndera, handcachif, viberiti vya gesi, bendera ndogo NK). watu kwa jina la mndela wanatengeneza hivi sasa mabilion ya pesa kutokana na umaarufu wa Nelson Mandela.

Usimlinganishe Nyerere na mandela katika nani mwenye jina kubwa duniani. Nyerere, mao, Stalin, Lumumba, Lenin, Che, samora na Kim IL Sung, hawa watu wako katika group makuhani wa ukomunisti. Hawa viongozi wote niliowataja, walikuwa wanawakamata watu wasiokuwa na ajira na kuwafunga jela badala ya kuwatafutia kazi za kulipwa mishahara. nanai mtu awaheshimu hapa duniani? nani mjinga apepee bendera nusu mlingoti kwa kuomboleza vifo vyao?
hivi wewe hujagundua kuwa makuhani wa ukomunisti walikuwa na sera za ukandamizaji?


!
!
eeh bana eeeeeh.....hebu tiririka zaidi
 
!
!
nikumbushwe tu kama south africa walipeperusha bendera nusu mlingoti na kuomboleza kifo cha nyerere.
Hata kama hawakupeperusha siye hatuna mioyo ya korosho au jino kwa jino. tunathamini wenzetu ikizingatia jinsi tulivyokuwa mstari wa mbele kupigania ukombozi wa wasouth na uhuru wa MANDELEA. TUTAKUWA TUKIJIFANYA HATUJAGUSWA BINAFSI NIMEGUSWA NA KIGO CHAKE.

R.I.P MANDELA. POLENI WANAAFRIKA KUSINI KWA KUONDOKEWA NA BABA YENU WA TAIFA.
 
Back
Top Bottom