Taarifa: Rais Kikwete aagiza bendera kupepea nusu mlingoti kwa siku tatu za maombolezo ya Kitaifa y

Kutokana na misele mingi anayoipiga na safari nyingi za bandika bandua na sasa yupo ulaya ndani ya mwezi kuwa ulaya zaidi ya mara 3,sasa asipoeda sauzi siku chcche zijazo najinyonga,,,,
anayebisha abishe,,,,!!
 
Kwa hiyo ina maana nyie wala vumbi hamtaenda kazini kwa muda wa siku tatu au inakuwaje?
 
Tanzania imetangaza siku tatu za maombolezo kuanzia tarehe 8 hadi11 kufuatiwa kifo cha kiongozi wa kwanza mweusi wa A/kusini Nelson Mandela...R. I. P Mzee Madiba...
Source: clouds fm.

Japo Clouds is not a reliable source, lakini naafiki kuomboleza hata wiki nzima, Mandela ni Nembo ya Africa
 
Acheni pumba kama hamna cha kuandika si mnakauka tu,MODS futeni pumba hii....Rip Madiba
 
!
!
nini!?........JK asiende kwenye msiba!?.....chezea JK kwa hitima wewe?

Wanaita HİTMA....Na kwenye hitma shurti ubwabwa uwepo. Kula Ubwabwa ni sunna sheikh...Tena utapata swawabu 25 ukiusomea dua kabla hujala. Swawabu hutiririka zaidi ukila kwa mikono na shurti la kula kwa mkono ukae TAHİYATU!!
Takibiiiiiirr
 
Afadhari tusiende kazini tupige mishe mingine kwani mshahara yetu walimu ni kiduchu!!
 
Hata dakika moja simpi, tungeweka angalau dakika mbili kwa watu wanaokufa na njaa, shida, watoto wadogo, wamama... Tunaweka siku tatu kwa Mandela, sawa alifanya kitu flani ila he z 95 mbona umri umeenda mno, hizo baraka zinamtosha kabisa....
 
atakaa kule mpaka matanga yaishe chezea mbongo wewe na ataonga apangwe siti za mbele siku ya kuaga mwili
 
Kutokana na misele mingi anayoipiga na safari nyingi za bandika bandua na sasa yupo ulaya ndani ya mwezi kuwa ulaya zaidi ya mara 3,sasa asipoeda sauzi siku chcche zijazo najinyonga,,,,
anayebisha abishe,,,,!!

Kwa mahusiano ya kijamaa kindugu kirafiki na mengine mengi, JK ni LAZİMA aende
 
R.V.P MY FARMER . Umepigana vita vilivyo vikali mwendo umeumaliza, imani umeilinda.nitaendelea kuenzi na kuiamini na kuisimamia kauli yako uliyowah kusema;(KURUDISHA MAPAMBANO NYUMA NI KOSA AMBALO KIZAZI KIJACHO HAKITA TUSAMEHE)
 
Mandela mwenyewe hakuhudhuria msiba wa Nyerere, sisi tunatangaza siku 3 za maombolezo!

Sioni sababu...


tunajikomba sana....sijui tukoje mitanzania..pamoja na kuisaidia SA na ANC kudai ukombozi na kukatwa mishahara kwa watu wetu kujenga kambi za wapigania uhuru wa SA..Pamoja na kujaza mimba dada zetu pale mazimbu (dark city) bado Mandela hakuja kumzika Nyerere....
 
Mandela mwenyewe hakuhudhuria msiba wa Nyerere, sisi tunatangaza siku 3 za maombolezo!

Sioni sababu...

Hapana, ilikuwa ahudhurie ila kwasababu ya maradhi ya Moyo alishauliwa asihudhurie. Ila nakumbuka hata SA bendera ilishushwa nusu mlingoti.
 
Back
Top Bottom