Taarifa Muhimu Toka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB)

moyafricatz

JF-Expert Member
Nov 27, 2015
2,900
4,865
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inapenda kuwataarifu waombaji wa mikopo kwa mwaka wa masomo 2018/2019 na umma kwa ujumla kwamba imetangaza orodha ya baadhi ya waombaji mikopo ambao fomu zao za maombi ya mikopo zina upungufu ili waweze kufanya marekebisho kwa njia ya mtandao https://olas.heslb.go.tz kwa siku saba (7) kuanzia Jumatatu Septemba 24 hadi Jumapili Septemba 30, 2018.

Katika kipindi hicho waombaji wote wa mikopo ambao fomu zao zina upungufu wa baadhi ya taarifa na nyaraka zao ama za wadhamimi wao, watapaswa kusoma majina yao kwenye orodha iliyowekwa kwenye tovuti ya HESLB www.heslb.go.tz na kisha kuingia kwenye mtandao wa maombi ya mikopo ili kufanya masahihisho kwa kufuata hatua zilizowekwa na baada kukamilisha, waziwasilishe ndani ya muda uliopangwa bila kutuma kwa njia ya EMS.

Nyaraka zote zinazokosekana ikiwa ni pamoja na vyeti vya kuzaliwa au vya vifo vya wazazi, kurasa za taarifa na saini za mwombaji na/au mdhamini wake zinapaswa kujazwa kwa ukamilifu, kuwa ‘scanned’ na kisha kupakiwa kwenye mtandao baada ya kuthibitishwa na mamlaka husika.

Zoezi la Uhakiki wa Taarifa za Waombaji wa mikopo
Baada kukamilika kwa muda wa kupokea maombi ya mikopo Julai 31, 2018, HESLB ilikuwa imepokea jumla ya maombi 78,833 ambapo baada ya uhakiki, HESLB ilibaini jumla ya waombaji zaidi ya 25,000 fomu zao za maombi zikiwa na upungufu wa nyaraka na uthibitisho wa kuwezesha kuendelea na hatua inayofuata ya kupangiwa mikopo katikati ya mwezi Oktoba, 2018.

Hitimisho
Kwa taarifa hii pia tunapenda kuwakumbusha waombaji wa mikopo ambao wamo katika orodha hiyo yenye upungufu wa taarifa kusoma kwa umakini na kurekebisha kasoro hizo ili waweze kupangiwa mikopo.

Aidha tunawatahadharisha dhidi ya matapeli wanaoweza kutumia taarifa hiyo kuwalaghai waombaji mikopo kuwa wanaweza kuwasaidia kupata mikopo. Tangazo maalum na mwongozo wa marekebisho vinapatikana katika tovuti ya HESLB (www.heslb.go.tz).

Iwapo wana maswali, wawasiliane nasi kupitia:
Simu: 0736665533 au 022 5507910

Taarifa hii pia inapatikana kwenye tovuti ya HESLB www.heslb.go.tz

Imetolewa na:
Mkurugenzi Mtendaji
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
 
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inapenda kuwataarifu waombaji wa mikopo kwa mwaka wa masomo 2018/2019 na umma kwa ujumla kwamba imetangaza orodha ya baadhi ya waombaji mikopo ambao fomu zao za maombi ya mikopo zina upungufu ili waweze kufanya marekebisho kwa njia ya mtandao https://olas.heslb.go.tz kwa siku saba (7) kuanzia Jumatatu Septemba 24 hadi Jumapili Septemba 30, 2018.

Katika kipindi hicho waombaji wote wa mikopo ambao fomu zao zina upungufu wa baadhi ya taarifa na nyaraka zao ama za wadhamimi wao, watapaswa kusoma majina yao kwenye orodha iliyowekwa kwenye tovuti ya HESLB www.heslb.go.tz na kisha kuingia kwenye mtandao wa maombi ya mikopo ili kufanya masahihisho kwa kufuata hatua zilizowekwa na baada kukamilisha, waziwasilishe ndani ya muda uliopangwa bila kutuma kwa njia ya EMS.

Nyaraka zote zinazokosekana ikiwa ni pamoja na vyeti vya kuzaliwa au vya vifo vya wazazi, kurasa za taarifa na saini za mwombaji na/au mdhamini wake zinapaswa kujazwa kwa ukamilifu, kuwa ‘scanned’ na kisha kupakiwa kwenye mtandao baada ya kuthibitishwa na mamlaka husika.

Zoezi la Uhakiki wa Taarifa za Waombaji wa mikopo
Baada kukamilika kwa muda wa kupokea maombi ya mikopo Julai 31, 2018, HESLB ilikuwa imepokea jumla ya maombi 78,833 ambapo baada ya uhakiki, HESLB ilibaini jumla ya waombaji zaidi ya 25,000 fomu zao za maombi zikiwa na upungufu wa nyaraka na uthibitisho wa kuwezesha kuendelea na hatua inayofuata ya kupangiwa mikopo katikati ya mwezi Oktoba, 2018.

Hitimisho
Kwa taarifa hii pia tunapenda kuwakumbusha waombaji wa mikopo ambao wamo katika orodha hiyo yenye upungufu wa taarifa kusoma kwa umakini na kurekebisha kasoro hizo ili waweze kupangiwa mikopo.

Aidha tunawatahadharisha dhidi ya matapeli wanaoweza kutumia taarifa hiyo kuwalaghai waombaji mikopo kuwa wanaweza kuwasaidia kupata mikopo. Tangazo maalum na mwongozo wa marekebisho vinapatikana katika tovuti ya HESLB (www.heslb.go.tz).

Iwapo wana maswali, wawasiliane nasi kupitia:
Simu: 0736665533 au 022 5507910

Taarifa hii pia inapatikana kwenye tovuti ya HESLB www.heslb.go.tz

Imetolewa na:
Mkurugenzi Mtendaji
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
Asante mkuu jf inahitaji watu muhimu kama wewe .
 
tatizo kubwa la bodi ni kukosa kitengo makini cha kuwasiliana na wadau moja kwa moja. simu zao ni chache na hazipokelewi. kwa sasa kwenye system yao sehemu ya submitt doccument haitokei. ukiwapigia ndo hivo simu hazipokelewi...
 
Back
Top Bottom