Mike Mushi
JF-Expert Member
- Feb 10, 2006
- 253
- 572
Tangu kuanza kwa mgomo wa madaktari nchini, wananchi katika maeneo mbalimbali ya nchi wamekuwa wakitoa rai kwa viongozi mbalimbali wa Chama Cha Demokrasia CHADEMA (CHADEMA) kuingilia kati mgogoro unaoendelea baina ya madaktari na Serikali.
Tarehe 25 Januari 2012 Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kilitoa taarifa kwa umma kueleza kwamba chama kiliguswa na mgomo uliokuwa ukiendelea nchini na kueleza masikitiko kuhusu udhaifu wa serikali katika kushughulikia kwa wakati madai ya madaktari nchini.
Katika taarifa hiyo tulieleza kwamba kwamba uzembe na ufisadi katika serikali kwenye sekta ya afya unaligharimu taifa na maisha ya wananchi. Hivyo, CHADEMA kikaitaka serikali kukamilisha kwa haraka majadiliano na madaktari ili kuepusha madhara zaidi kwa umma.
Katika taarifa hiyo, CHADEMA iliwapa pole wananchi ambao wameathirika na migomo inayoendelea na kuzingatia kwamba mgomo huo umesababishwa na udhaifu katika serikali. Aidha, pamoja na migomo inayoendelea CHADEMA kilitoa rai kwa madaktari na watumishi wengine wa umma kuhakikisha maisha ya wagonjwa walio katika hali ya hatari yanaokolewa.
CHADEMA ilieleza kuwa iwapo serikali haitachukua hatua za haraka kutatua mgogoro unaoendelea na kushughulikia madai ya wafanyakazi wa sekta ya afya, viongozi wakuu wa CHADEMA watatoa tamko kuhusu hatua za ziada ambazo chama kitachukua ili kuhakikisha kwamba umma hauendelei kupata madhara kutokana na udhaifu wa serikali.
Pamoja na taarifa hiyo viongozi wakuu wa chama na kambi rasmi ya upinzani inayoongozwa na CHADEMA wamefanya mawasiliano kati ya tarehe 23 na 29 Januari 2012 na viongozi wa Chama Cha Madaktari Tanzania (MAT) na kamati ya mpito ya mgomo wa madaktari ili kupatiwa nakala ya madai ya madaktari na kuweza kutimiza wajibu wa chama na kambi rasmi ya upinzani bungeni katika kushughulikia vyanzo vya mgogoro huo.
Mwenyekiti wa chama Mh. Freeman Mbowe kwa nafasi yake kama kiongozi wa upinzani bungeni tarehe 27 Januari 2012 aliwasiliana na viongozi wa kamati ya mpito ya madaktari ili kupokea madai yao kuweza kulinganisha na masuala ambayo tayari kambi rasmi ya upinzani iliyawasilisha bungeni kuhusu haja ya serikali kuboresha maslahi ya watumishi wa umma katika sekta ya afya.
Katibu Mkuu Dr Wilbroad Slaa kwa niaba ya chama aliwasiliana na viongozi wa Chama Cha Madaktari (MAT) kwa ajili ya kupatiwa nakala ya nyaraka za madai husika kwa nyakati mbalimbali.
Kutokana na kusitasita kwa viongozi wa MAT na kamati ya mpito ya mgomo wa madaktari kutoa ushirikiano unaostahili ili chama na kambi rasmi ya upinzani, CHADEMA kilivuta subira ili kukamilisha mawasiliano husika kuweza kuisimamia serikali kuhusu mgogoro huu.
CHADEMA kinatoa mwito kwa TUGHE, MAT na kamati ya mgomo wa madaktari kutoa ushirikiano unaostahili kwa chama, kambi rasmi ya upinzani na wadau wengine ili kuweza kuunganisha nguvu ya pamoja katika kushughulikia madai ya msingi ya madaktari yenye kuathiri sekta ya afya nchini na maisha ya wananchi kwa ujumla.
Kwa upande mwingine, CHADEMA hakijaridhishwa na maelezo yaliyotolewa na serikali kupitia kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuhusu namna ambavyo imeshughulikia mgogoro huu na madai ya madaktari, watumishi wengine wa umma katika sekta ya afya nchini pamoja na uboreshaji wa huduma katika hospitali, zahanati na vituo vya afya nchini. Aidha, CHADEMA kinamtaka Waziri Mkuu Mizengo Pinda na serikali kwa ujumla kuacha vitisho na matumizi makubwa ya vyombo vya dola kwa madaktari na makundi mengine katika jamii yanapotumia uhuru wa kikatiba kwa kukusanyika, kujadiliana na kuhoji kuhusu uwajibikaji wa serikali na viongozi wake kwa kuzingatia ibara za 8, 18 na 20 za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
CHADEMA kinarudia kutoa rai kwa wananchi kuendelea kuunga mkono madai ya msingi ya madaktari ili kuhakikisha kwamba hospitali za umma nchini zinakuwa mahali salama kwenye huduma bora za kulinda maisha ya wananchi hususan wasio na uwezo wa kudumu gharama za matibabu katika hospitali binafsi za ndani na nje ya nchi. Pamoja na madai ya maslahi ya madaktari ambayo ni kwa maslahi ya umma, madaktari wanataka pia serikali ichukue hatua za kuboresha huduma za afya. Serikali inaingia gharama kubwa kupeleka baadhi ya watanzania wengi wao wakiwa viongozi kwenda kutibiwa nje ya nchi huduma katika hospitali za umma zinazidi kuzorota kutokana na ukosefu wa madawa, vifaa tiba na wataalamu wa kutosha katika hospitali za umma. Aidha, serikali inashindwa kuipa kipaumbele sekta ya afya kwa kisingizio cha kutokuwa na uwezo wakati ambapo inafanya matumizi mengine ya anasa kwa kiwango kikubwa kama ilivyokuwa katika maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru. Serikali inashindwa kushughulikia madai ya posho za madaktari kama nyongeza ya posho ya kulala kazini (on call allowance) na posho ya kufanya kazi katika mazingira hatarishi (risk allowance) wakati huo huo serikali hiyo hiyo inazungumzia nyongeza ya posho za vikao kwa wabunge.
Chama kimewasiliana na kimeitaka kambi rasmi ya upinzani bungeni inayoongozwa na CHADEMA kufanya uchambuzi wa kina kuhusu maelezo hayo na kutumia njia za kibunge katika kuisimamia serikali kushughulikia migogoro kati yake na madaktari, maslahi ya watumishi wa umma katika sekta ya afya pamoja na uboreshaji wa huduma katika hospitali, zahanati na sekta ya afya nchini.
Viongozi wakuu wa CHADEMA watatoa tamko kuhusu hatua za ziada ambazo chama kitachukua ili kuhakikisha kwamba umma hauendelei kupata madhara yatokanayo na udhaifu wa serikali katika sekta ya afya nchini iwapo serikali haitachukua hatua zinazostahili kuzingatia maoni yanayoendelea kutolewa na kambi ya upinzani katika nyakati mbalimbali.
CHADEMA kinarudia tena kutoa mwito kwa serikali inayoongozwa na Rais Jakaya Kikwete kurejea mapendekezo yaliyotolewa na chama kupitia tamko la Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr Wilbroad Slaa kuhusu mwelekeo wa taifa kwa mwaka 2012 kwamba Kipaumbele kikuu cha Kijamii kiwe kushughulikia vyanzo vya migogoro katika maeneo mbalimbali badala ya kukabiliana na matokeo.
Iwapo serikali ingezingatia msingi wa tamko hilo ambalo linapatikana kupitia www.chadema.or.tz; mgogoro huu kuhusu madaktari na watumishi wengine wa sekta ya afya na serikali usingefikia hatua ya kuleta madhara kwa wananchi.
Tunasisitiza umma uzingatie kwamba tangu Mwalimu Nyerere aondoke madarakani mwaka 1985, Serikali ya CCM imeongeza wingi wa majengo mbalimbali kwenye sekta ya afya hata hivyo imeshindwa kusimamia utoaji bora wa huduma za afya katika zahanati, hospitali na vituo vya afya. Kutokana na mfumo mbaya wa usimamizi wa sekta ya afya, misingi imara ya kuimarisha sekta ya afya iliyowekwa baada ya uhuru imevunjwa na kubomolewa ikiwemo katika masuala yanayohusu kujali maslahi ya watumishi wa umma katika sekta hii muhimu.
Hali hii imefanya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kuwa na nakisi ya watumishi asilimia 48% na takwimu zinaonesha kuwa 18% ya wafamasia, 15% ya madaktari, 13% ya madaktari wasaidizi waliacha vituo vyao vya kazi na kwenda kutafuta kazi kwenye mashirika ambayo yanalipa mishahara mikubwa na mizuri. Nakisi hii itaongezeka zaidi iwapo madai ya msingi ya madaktari na watumishi wengine hayatashughulikiwa na serikali itaendelea kuchelewa kushughulikia migogoro na migomo mingine inayoendelea.
Serikali ya CCM irejee ilani ya CHADEMA katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 kifungu cha 3.3 ambapo chama kimeeleza bayana namna ambavyo serikali inaweza kuongeza mishahara kwa watumishi wa sekta ya afya ili kuweza kuwavutia wataalamu kubakia nchini badala ya kwenda kugoma au kwenda kutafuta kazi nje ya nchi kutokana na malipo mazuri huko.
Aidha, katika ilani hiyo CHADEMA imeeleza bayana kwamba ipo haja ya malipo ya mazingira magumu kutolewa kwa watumishi wa afya wanaofanya kazi katika maeneo na kada maalum.
Pia, serikali izingatie maoni yaliyotolewa na kambi rasmi ya upinzani bungeni kuhusu sekta ya afya ili kuweza kuepusha migogoro na pia muendelezo wa upatikanaji wa huduma mbovu za afya katika hospitali, zahanati na vituo vya afya nchini kwa manufaa ya umma.
Imetolewa tarehe 30 Januari 2012 kwa niaba ya CHADEMA na:
John Mnyika (Mb)
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi
Tarehe 25 Januari 2012 Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kilitoa taarifa kwa umma kueleza kwamba chama kiliguswa na mgomo uliokuwa ukiendelea nchini na kueleza masikitiko kuhusu udhaifu wa serikali katika kushughulikia kwa wakati madai ya madaktari nchini.
Katika taarifa hiyo tulieleza kwamba kwamba uzembe na ufisadi katika serikali kwenye sekta ya afya unaligharimu taifa na maisha ya wananchi. Hivyo, CHADEMA kikaitaka serikali kukamilisha kwa haraka majadiliano na madaktari ili kuepusha madhara zaidi kwa umma.
Katika taarifa hiyo, CHADEMA iliwapa pole wananchi ambao wameathirika na migomo inayoendelea na kuzingatia kwamba mgomo huo umesababishwa na udhaifu katika serikali. Aidha, pamoja na migomo inayoendelea CHADEMA kilitoa rai kwa madaktari na watumishi wengine wa umma kuhakikisha maisha ya wagonjwa walio katika hali ya hatari yanaokolewa.
CHADEMA ilieleza kuwa iwapo serikali haitachukua hatua za haraka kutatua mgogoro unaoendelea na kushughulikia madai ya wafanyakazi wa sekta ya afya, viongozi wakuu wa CHADEMA watatoa tamko kuhusu hatua za ziada ambazo chama kitachukua ili kuhakikisha kwamba umma hauendelei kupata madhara kutokana na udhaifu wa serikali.
Pamoja na taarifa hiyo viongozi wakuu wa chama na kambi rasmi ya upinzani inayoongozwa na CHADEMA wamefanya mawasiliano kati ya tarehe 23 na 29 Januari 2012 na viongozi wa Chama Cha Madaktari Tanzania (MAT) na kamati ya mpito ya mgomo wa madaktari ili kupatiwa nakala ya madai ya madaktari na kuweza kutimiza wajibu wa chama na kambi rasmi ya upinzani bungeni katika kushughulikia vyanzo vya mgogoro huo.
Mwenyekiti wa chama Mh. Freeman Mbowe kwa nafasi yake kama kiongozi wa upinzani bungeni tarehe 27 Januari 2012 aliwasiliana na viongozi wa kamati ya mpito ya madaktari ili kupokea madai yao kuweza kulinganisha na masuala ambayo tayari kambi rasmi ya upinzani iliyawasilisha bungeni kuhusu haja ya serikali kuboresha maslahi ya watumishi wa umma katika sekta ya afya.
Katibu Mkuu Dr Wilbroad Slaa kwa niaba ya chama aliwasiliana na viongozi wa Chama Cha Madaktari (MAT) kwa ajili ya kupatiwa nakala ya nyaraka za madai husika kwa nyakati mbalimbali.
Kutokana na kusitasita kwa viongozi wa MAT na kamati ya mpito ya mgomo wa madaktari kutoa ushirikiano unaostahili ili chama na kambi rasmi ya upinzani, CHADEMA kilivuta subira ili kukamilisha mawasiliano husika kuweza kuisimamia serikali kuhusu mgogoro huu.
CHADEMA kinatoa mwito kwa TUGHE, MAT na kamati ya mgomo wa madaktari kutoa ushirikiano unaostahili kwa chama, kambi rasmi ya upinzani na wadau wengine ili kuweza kuunganisha nguvu ya pamoja katika kushughulikia madai ya msingi ya madaktari yenye kuathiri sekta ya afya nchini na maisha ya wananchi kwa ujumla.
Kwa upande mwingine, CHADEMA hakijaridhishwa na maelezo yaliyotolewa na serikali kupitia kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuhusu namna ambavyo imeshughulikia mgogoro huu na madai ya madaktari, watumishi wengine wa umma katika sekta ya afya nchini pamoja na uboreshaji wa huduma katika hospitali, zahanati na vituo vya afya nchini. Aidha, CHADEMA kinamtaka Waziri Mkuu Mizengo Pinda na serikali kwa ujumla kuacha vitisho na matumizi makubwa ya vyombo vya dola kwa madaktari na makundi mengine katika jamii yanapotumia uhuru wa kikatiba kwa kukusanyika, kujadiliana na kuhoji kuhusu uwajibikaji wa serikali na viongozi wake kwa kuzingatia ibara za 8, 18 na 20 za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
CHADEMA kinarudia kutoa rai kwa wananchi kuendelea kuunga mkono madai ya msingi ya madaktari ili kuhakikisha kwamba hospitali za umma nchini zinakuwa mahali salama kwenye huduma bora za kulinda maisha ya wananchi hususan wasio na uwezo wa kudumu gharama za matibabu katika hospitali binafsi za ndani na nje ya nchi. Pamoja na madai ya maslahi ya madaktari ambayo ni kwa maslahi ya umma, madaktari wanataka pia serikali ichukue hatua za kuboresha huduma za afya. Serikali inaingia gharama kubwa kupeleka baadhi ya watanzania wengi wao wakiwa viongozi kwenda kutibiwa nje ya nchi huduma katika hospitali za umma zinazidi kuzorota kutokana na ukosefu wa madawa, vifaa tiba na wataalamu wa kutosha katika hospitali za umma. Aidha, serikali inashindwa kuipa kipaumbele sekta ya afya kwa kisingizio cha kutokuwa na uwezo wakati ambapo inafanya matumizi mengine ya anasa kwa kiwango kikubwa kama ilivyokuwa katika maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru. Serikali inashindwa kushughulikia madai ya posho za madaktari kama nyongeza ya posho ya kulala kazini (on call allowance) na posho ya kufanya kazi katika mazingira hatarishi (risk allowance) wakati huo huo serikali hiyo hiyo inazungumzia nyongeza ya posho za vikao kwa wabunge.
Chama kimewasiliana na kimeitaka kambi rasmi ya upinzani bungeni inayoongozwa na CHADEMA kufanya uchambuzi wa kina kuhusu maelezo hayo na kutumia njia za kibunge katika kuisimamia serikali kushughulikia migogoro kati yake na madaktari, maslahi ya watumishi wa umma katika sekta ya afya pamoja na uboreshaji wa huduma katika hospitali, zahanati na sekta ya afya nchini.
Viongozi wakuu wa CHADEMA watatoa tamko kuhusu hatua za ziada ambazo chama kitachukua ili kuhakikisha kwamba umma hauendelei kupata madhara yatokanayo na udhaifu wa serikali katika sekta ya afya nchini iwapo serikali haitachukua hatua zinazostahili kuzingatia maoni yanayoendelea kutolewa na kambi ya upinzani katika nyakati mbalimbali.
CHADEMA kinarudia tena kutoa mwito kwa serikali inayoongozwa na Rais Jakaya Kikwete kurejea mapendekezo yaliyotolewa na chama kupitia tamko la Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr Wilbroad Slaa kuhusu mwelekeo wa taifa kwa mwaka 2012 kwamba Kipaumbele kikuu cha Kijamii kiwe kushughulikia vyanzo vya migogoro katika maeneo mbalimbali badala ya kukabiliana na matokeo.
Iwapo serikali ingezingatia msingi wa tamko hilo ambalo linapatikana kupitia www.chadema.or.tz; mgogoro huu kuhusu madaktari na watumishi wengine wa sekta ya afya na serikali usingefikia hatua ya kuleta madhara kwa wananchi.
Tunasisitiza umma uzingatie kwamba tangu Mwalimu Nyerere aondoke madarakani mwaka 1985, Serikali ya CCM imeongeza wingi wa majengo mbalimbali kwenye sekta ya afya hata hivyo imeshindwa kusimamia utoaji bora wa huduma za afya katika zahanati, hospitali na vituo vya afya. Kutokana na mfumo mbaya wa usimamizi wa sekta ya afya, misingi imara ya kuimarisha sekta ya afya iliyowekwa baada ya uhuru imevunjwa na kubomolewa ikiwemo katika masuala yanayohusu kujali maslahi ya watumishi wa umma katika sekta hii muhimu.
Hali hii imefanya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kuwa na nakisi ya watumishi asilimia 48% na takwimu zinaonesha kuwa 18% ya wafamasia, 15% ya madaktari, 13% ya madaktari wasaidizi waliacha vituo vyao vya kazi na kwenda kutafuta kazi kwenye mashirika ambayo yanalipa mishahara mikubwa na mizuri. Nakisi hii itaongezeka zaidi iwapo madai ya msingi ya madaktari na watumishi wengine hayatashughulikiwa na serikali itaendelea kuchelewa kushughulikia migogoro na migomo mingine inayoendelea.
Serikali ya CCM irejee ilani ya CHADEMA katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 kifungu cha 3.3 ambapo chama kimeeleza bayana namna ambavyo serikali inaweza kuongeza mishahara kwa watumishi wa sekta ya afya ili kuweza kuwavutia wataalamu kubakia nchini badala ya kwenda kugoma au kwenda kutafuta kazi nje ya nchi kutokana na malipo mazuri huko.
Aidha, katika ilani hiyo CHADEMA imeeleza bayana kwamba ipo haja ya malipo ya mazingira magumu kutolewa kwa watumishi wa afya wanaofanya kazi katika maeneo na kada maalum.
Pia, serikali izingatie maoni yaliyotolewa na kambi rasmi ya upinzani bungeni kuhusu sekta ya afya ili kuweza kuepusha migogoro na pia muendelezo wa upatikanaji wa huduma mbovu za afya katika hospitali, zahanati na vituo vya afya nchini kwa manufaa ya umma.
Imetolewa tarehe 30 Januari 2012 kwa niaba ya CHADEMA na:
John Mnyika (Mb)
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi