Taarifa kwa Umma: Kanusho la kuzuiwa behewa za SGR Ujerumani

Tanzania Railways Corp

JF-Expert Member
Mar 23, 2018
251
595
TAARIFA KWA UMMA - KANUSHO LA KUZUIWA KWA BEHEWA ZA SGR UJERUMANI

Kanusho Behewa za SGR.jpg
 

Attachments

  • Kanusho Behewa za SGR.pdf
    367.5 KB · Views: 2
Hawa jamaa bhana...

Taarifa inasema "Kanusho la kuzuiwa kwa behewa za SGR Ujerumani", ndani ya taarifa wanasema "hatujapokea taarifa yoyote kuhusu kuzuiwa au kuuzwa"
 
TAARIFA KWA UMMA - KANUSHO LA KUZUIWA KWA BEHEWA ZA SGR UJERUMANI

View attachment 2424031
Mkuu Tanzania Railways Corp , kwanza asante kwa taarifa hii,
Nina viswali vyangu vichache kuhusu hili la vichwa na mabehewa
Ukipata muda yapitie, utujibu, ila hata ukikosa muda, kutokana na ubize na pilika pilika za mapokezi, usijali mimi ni muelewa ma nitakuelewa.

Kwenye mambo ya SGR, Watanzania tunapaswa kuambiwa ukweli wa kila kitu!, serikali yetu lazima iwe very transparent see through kwenye kila kitu including mikataba na financial maters kufuatia kuwahi kupigwa huko nyuma kwenye rada, kwenye ndege, kwenye meli na sasa kwenye reli
Maswali haya yajibiwe kikamilifu
Wanabodi,
1. Taarifa ya TRC inasema vichwa vipya na mabehewa mapya, lakini ukweli ni kuwa ni vichwa mitumba na mabehewa mitumba kama ya mwaka '1947'!.

2. Ukiyaangalia kwa ndani, haya mabehewa ni kama yana madirisha only one sided!, hiki ni kuashiria originally haya ni mabehewa ya underground trains na sio ya terestrial train!. Sisi SGR yetu ni terestrial, moja ya faida kubwa kusafiri na treni ni pamoja na kuenjoy kitu kinachoitwa scenery enjoymement, madirisha makubwa both sides abiria kuona nje, hizi behewa za madirisha ya upande mmoja, hebu mfikirie abiria wa Kigoma, seat ya upande usio na dirisha!, kuna tofauti gani na chumba cha jela?.

3. Mkataba ni wa ukarabati na kutiwa nakshi nakshi kwa vichwa na mabehewa mitumba!, na sio kuundwa kwa vichwa na mabehewa mapya!, kwanini Watanzania hatuelezwi ukweli?.
Hakuna ubaya nchi kununua vichwa mitumba na mabehewa mitumba, kitu muhimu ni Watanzania tuelezwe ukweli!.

4. Je, hivyo vichwa viliundwa lini, wapi?, jee originally vimetumika wapi na kwa muda gani kabla sisi hatujauziwa?

5. Mitumba hiyo imenunuliwa kwa bei gani, ikakarabatiwa kwa bei gani, na kusafirishwa kwa gharama gani?

6. Tufanyiwe comparative analysis, kama tungenunua vichwa vipya na mabehewa mapya, tungetumia gharama kiasi gani, compared na kununua vichwa mitumba na mabehewa mitumba, ili tujue tumeokoa fedha kiasi gani kwa kununua mitumba hiyo?

7. Japo gharama za kununua vitu vipya ni juu ila maintance cost ni ndogo, unaweza kununua mitumba kwa bei poa kumbe ni mitumba choka mbaya, hivyo maintenance cost ikawa juu.

8. Sii wengi wanajua kazi ya CAG sio kutoa tuu zile ripoti za hesabu za serikali, CAG ni Mdhibiti na Mkaguzi, ufhibiti unafanywa kabla ya manunuzi, je, kulifanyika tathmini yoyote rail worthness report ya vichwa na mabehewa hayo mitumba kabla hayajanunuliwa?. Then CAG atufanyie value for money audit, msikute mitumba hiyo tumepewa bure, huku watu wakipiga kubwa tunauziwa kwa bei ya mapya!.

9. Ukiingia mkataba wa manunuzi, kwa matengenezo, mzigo ukanunuliwa, delivery ndio ikachelewa, huwezi kuvunja mkataba huo ukabaki salama, hivyo kesi ikifunguliwa, Tanzania tunashindwa hata kabla kesi haijaanza!.

10. Tulivunja mkataba wa Dowans, tulishitakiwa, tukashindwa, tukadaiwa tukasema hatulipi!, watu wakajiapisha "over my dead body", hatulipi!.
ukweli ni kuwa tumelipa kwa siri, Watanzania hatukuambiwa!.

11. Tulipo vunja mkataba wa Dowans, Zitto akashauri tuitaifishe mitambo ile, Wabunge wetu wakagoma kuwa Tanzania hatununui mitambo chakavu, mitambo mitumba!

12 Mitambo ile ikanunuliwa na Simbion, tukaingia nao mkataba ule ule wa Dowans, watu wale wale walio ikataa dowams, ndio hao hao danced to the tune na Hilary Clinton kuzindua Simbion kwa mkataba ule ule tuliovunja!, kwa gharama zile zile!, na capacity charge ile ile!, na tukawalipa!.

13. JPM alipoingia tukavunja mkataba wa Simbion, tukashitakiwa, tukashindwa, JPM akagoma kulipa!, ila baada tuu ya JPM kuitwa kule alipoitwa huku nyuma, sisi sio tuu tumelipa!, bali pia tumeinunua ile mitambo ya Simbion kwa bei ya ajabu!, sasa mitambo ile tuliosema ni chakavu, mtumba, na serikali yetu hatununui, mivitu chakavu, sasa ndio tumeinunua!, sasa mitambo ile ya Simbion ni mitambo yetu, ni mali yetu! na malipo yote yaliisha fanyika chap chap fasta fasta!, bila bajeti yake kuombwa popote!, bila Bunge letu kuijadili, bila CAG kuidhinisha malipo hayo!, na haya yote yamefanyika bila iWatanzania kuambiwa!.

14. NB. Unapohoji vitu kama hivi, huchelewi kunyooshewa vidole vya kukosa uzalendo au kutokuwa na nia njema!, no!, wala sijasema kilichofanyika ni wrong!, no!, ninachosema hapa ni sisi
Watanzania wa sasa ni waelewa, tuwe tuu tunaambiwa ukweli,

15. Kwa vile mambo kama haya kwenye manunuzi makubwa yaliwahi kutokea kule nyuma kwenye ununuzi wa Rada mtumba toka BAE, watu wakaweka cha juu kikubwa tuu, tukalipa fasta!, Mama Mzalendo wa kizungu, Linda Chalkel akabaini, akatupigania tukarudishiwa chenji ya Rada!.

16. Ununuzi wa ndege ya rais Gulf Steeam bei ikapaishwa zaidibya mara tatu!, John Cheyo akaonyesha bei ya kiwandaji watu wakatia pamba masikioni tukalipa fasta!.

17. Kuna vifaa vya kijeshi chakavu tumeuziwa hapa!, tangu vimenunuliwa havijawahi kutumika mpaka leo!. Hivi naomba nisivizungumzie wala msiniulizie!, maana hata sisi waandishi wa habari haturuhusiwi kuzungumzia mambo ya jeshi na usalama wa taifa, ila fedha zilizotumika sio fedha za jeshi au za usalama wa taifa, ni fedha za Watanzania, kuzungumzia vifaa vya jeshi, tuliuziwa nini mitumba ni vifaa vya nini na viko wapi, hii ni no!, hatuzungumzi, lakini tulilipia fedha kiasi gani, ni haki ya Watanzania kujua!.

18. Tukanunua Boti mtumba ya MV Bagamoyo, ikafanya safari moja tuu mahali pa 30 min, ilitumia masaa 3!, Hii pia sasa ni kufaa cha kijeshi!, isizungumzwe!, ila fedha zake ni fedha za Watanzania!.

19. Hivyo kweli hivi vichwa na mabehewa haya, ni bora tukaelezana ukweli tangia mwanzo!.

20. Namalizia kwa msisitizo, hakuna ubaya kutumia vitu used!, tena vingine ni vizuri, imara, bora, madhubuti kuliko hata vipya!, na Watanzania walio wengi, kutokana na low purchasing power due to umasikini uliotopea, wengi wetu affordability yetu ni mitumba kuanzia magar
i, nguo hadi mitambo, hivyo tumezoea, tunachohitaji ni kuambiwa ukweli tuu!,
tutaelewa tuu kuliko...

Wasalaam.
Paskali.
Maswali haya yanahitaji majibu ya kina na sio blah blah!.
Kama mtu kuuliza maswali kama haya, kutapelekea kuhojiwa uzalendo wake, mimi naomba kutumia kinga ya kihabari na kanuni ya kwanza ya mwandishi wa habari no seek the truth, and write nothing but the truth!, kuna kitu ninadhamiria sio tuu kuandika bali kukitengenezea a video documentary ya safari ya SGR ya Tanzania, tulipotoka, tulipo na tunapokwenda, ili huko mbele, likija kujitokeza liji white elephant fulani hivi ambalo sijui kama ni mimi tuu naliona, angalau dhamira yangu isinisute, niliona kabla, nikasema kabla, nikaandaa documentary kabla, nikaonyesha kabla, ili angalau jamii ya Watanzania wajue kuna watu waliona kabla na walisema kabla!.

Na labda kuwasaidia Watanzania wenzangu wasio jua, kwenye ile kashfa ya rada, BAE walikiri kutoa mlungula wa kickbacks, lakini sheria yao inawaruhusu non disclosure ya waliowapa mlungula, ilo usipoteze wateja wapya wapenda mlungula, kibiashara mlungula wa 10% ni halali!, ila ikijulikana kuwa umetoa mlungula, unapaswa ama uwataje uliowapa mlungungula, wakamuliwe wautapike huo mlingula, ama uwahifadhi usiwataje, na badala yake utozwe faini kwa uliowapa mlungula, na kuurejesha ule mlungula, na hicho ndicho kilichofanywa na BAE, kuwahifadhi waliowapa mlungula, na badala yake ikakubali kulipa faini na ndipo tukarejeshewa ile chenji ya rada.

Hii maana yake, kuna viongozi wetu walikula mlungula BAE akawakingia kifua kuwahifadhi kwa kulipia faini na ule mlungula ukarudishwa nchini kama chenji ya rada, endapo BAE wasinge wakingia kifua kuwahifadhi na kuwalinda, amini usiamini, hayo majina ya waliopokea mlungula na kuzihifadhi fedha zao kule Credit Suisse, yangetoka, Watanzania msinge amini macho na masikio yenu!.

Kashfa hii iliobuka kwasababu tuu kulitokea lijinga limoja, mgao wake yeye ukauhifadhi visiwa fulani ambavyo viko chini ya milki ya Uingereza, ndipo Muingereza akabaini, lakini kama wote wange bank Swiss banks, kule fedha zao ni very secure, hata bank manager, hajui majina ya customers na clients ni secret codes tuu zinatembea, hivyo wala kashfa ya rada isinge ibuka!.

Hivyo watu tunaoulizia kuhusu haya mabenewa, naomba mtuelewe ni wazalendo wa kweli wa nchi hii!.

Paskali
 
Back
Top Bottom