Taarifa kwa Access Bank

mgulu

Member
Feb 14, 2015
74
33
Wana Jf
Siku ya Jumamosi nilipigiwa simu na mtu akajitambulisha kwa jina la Daniel (0656438***) kutoka Access Bank, akaniambia nimechaguliwa kwenda kwenye training kutokana na Maombi yangu niliyotuma ya kazi.

Katika maongezi na yule jamaa alinipa options nichague niiende kuanza training lini maana wao wana uhitaji wa maafisa kwa haraka sana, option ya kwanza alinipa tar. 18/05 na ya pili ilikuwa mwezi wa sita. Akazidi kunisisitizia watanitumia forms za medical cherk up nizitume kabla ya siku husika.

Kilichonishtua ni kutaka ela kama laki tatu au mbili maana hr anahitaji kwa kukufanyia upendeleo, nikamjibu mimi sina kabisa hata 10, labda unisaidie nikifika huko nitakulipa kama fadhira, jamaa akasema Mimi sina shida ila Mzee ndio kila kitu labda nikaongee nayo then tuone nitakusaidiaje, poa poa tukamalizia Hapo.

Baadaye nampigia simu kumuulizia anasema ooh bado sijaongea nayo nikiongea nayo ntakujilisha siku ikaisha bila call yake. Nilishtuka sana hasa nikipiga ile simu haipokelewi mpaka Leo. Nikajua ndio walewale wanaowaibia watu kwa kutofahamu.
Naomba kuwasilisha
 
Pole sana kaka!

kwanza mtu kama huyo ulitakiwa kumripoti polisi, pia shukuru Mungu hukumtumia hela lazima ingeliwa tu. Inabdi watu muwe makini sana hawa matapeli ambao wanatumia vigezo vya uhaba wa ajira kujitengenezea vipato
 
Kabla ya kuhukumu ni tapeli au laah inabidi utwambie ulituma maombi ya kazi au hukutuma? Na kama ulituma ulitumia njia ya email ay Posta?

Kama ni email weka hapa email tutajua kama domain ni ya access au matapeli, na kama ni posta weka address tutajua kama ni ya kweli au uongo.

Anaweza akawa sio tapeli ila ni mchongo from inside au akawa tapeli kama ukiweza kuanika hizo info tunaweza saidia kujua.
 
Benk yenyewe yakichovu, wanaajiri kila cku km ya poster. km uli apply then baadae ukapigiwa cm na tapeli basi wao wenyewe ndo wanapiga izo mishe.
 
Wana Jf
Siku ya Jumamosi nilipigiwa simu na mtu akajitambulisha kwa jina la Daniel (0656438***) kutoka Access Bank, akaniambia nimechaguliwa kwenda kwenye training kutokana na Maombi yangu niliyotuma ya kazi.

Katika maongezi na yule jamaa alinipa options nichague niiende kuanza training lini maana wao wana uhitaji wa maafisa kwa haraka sana, option ya kwanza alinipa tar. 18/05 na ya pili ilikuwa mwezi wa sita. Akazidi kunisisitizia watanitumia forms za medical cherk up nizitume kabla ya siku husika.

Kilichonishtua ni kutaka ela kama laki tatu au mbili maana hr anahitaji kwa kukufanyia upendeleo, nikamjibu mimi sina kabisa hata 10, labda unisaidie nikifika huko nitakulipa kama fadhira, jamaa akasema Mimi sina shida ila Mzee ndio kila kitu labda nikaongee nayo then tuone nitakusaidiaje, poa poa tukamalizia Hapo.

Baadaye nampigia simu kumuulizia anasema ooh bado sijaongea nayo nikiongea nayo ntakujilisha siku ikaisha bila call yake. Nilishtuka sana hasa nikipiga ile simu haipokelewi mpaka Leo. Nikajua ndio walewale wanaowaibia watu kwa kutofahamu.
Naomba kuwasilisha

Sasa umeongea yote halafu namba umeificha weka wazi tumpigie tumpe za uso, ni tapeli tu huyo.
 
Access ni ya manyang'au hivyo inawezekana ni mchongo toka ndani kwao kwani kwao huko Nairobi ndio zao hizo!!
 
Kwanza utuambie kama ni kweli uli appy au la. Then ndio tutajua kuwa ni tapeli au ni insider wa hiyo bank... Kwa ninavyoijua mimi, Access bank, ni bank moja wapo inayoajiri bila upendeleo. Sema tu mishahara yao ni kima cha chini sana!
 
Back
Top Bottom