Uchaguzi 2020 Taarifa kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi itazuia Mawakala wa Vyama kuingia na simu zao katika vituo vya kupigia kura imetushtua

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,009
SUALA LA SIMU KWA MAWAKALA: TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI MSIHARIBU UCHAGUZI WA WATANZANIA!

Taarifa kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi itazuia Mawakala wa Vyama kuingia na simu zao katika vituo vya kupigia kura imetushtua hata sisi viongozi wa Kanisa! Simu ina mambo mengi sana katika ulimwengu wa sasa ikiwemo kutunza kumbukumbu kwa njia mbalimbali.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi haiwezi kuwafanya mawakala kama 'tabula rasa' yaani watu wasioweza kuhifadhi kumbukumbu yo yote na hata kushindwa kuwasiliana. Mawakala wakiwa na simu wanaweza kupiga picha matokeo halisi ili kudhibiti wizi wa kura! Kitendo cha Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuzuia Mawakala kuingia na simu katika chumba cha kupigia kura ni sawa na kuandaa usiri utakaopelekea mazingira ya kuibiwa au kuchakachuliwa kwa kura!

Tunaitahadharisha Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuacha kutoa maelekezo au kutunga kanuni kwa lengo la kufanya Matokeo ya Uchaguzi Mkuu yasiheshimike na wananchi! Ili kuleta afya ni vizuri maelekezo na kanuni za Tume zikubaliwe na vyama vyote. Tume iepuke kutoa kanuni na maelekezo katika kipindi hiki kwa lengo la kuubeba upande mmoja na kuunyonga upande mwingine!

Sisi tumekwisha kutimiza wajibu wetu (Ezekieli 33:1-20).

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula - Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki na Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Makanisa ya Moravian ya Uamsho Duniani
 
Sasa Askofu kila mtu akipiga picha, then tuanze kutafuta picha ya nani ndio sahihi? Tume ina lengo zuri kwamba taarifa za matokeo ziwe na channel moja, sio kila mtu na matokeo yake itakuja kuleta taharuki na hatimae vurugu.Endelea kuchunga kondoo wa Bwana mambo mengine haya kuhusu. Usichanganye siasa na dini
 
Hahaha..Ikifika Novemba nitakuwa nawapa pole tu. Mnatumia nguvu nyingi, akili chache.
 
Rais anawapongeza team iliyowezesha mkataba mpya wa madini akiwamo professor P Kabudi . Amewaomba viongozi wa dini wawaombee sana

Maendeleo hayana vyama
 
Sasa Askofu kila mtu akipiga picha, then tuanze kutafuta picha ya nani ndio sahihi? Tume ina lengo zuri kwamba taarifa za matokeo ziwe na channel moja, sio kila mtu na matokeo yake itakuja kuleta taharuki na hatimae vurugu.Endelea kuchunga kondoo wa Bwana mambo mengine haya kuhusu. Usichanganye siasa na dini
Ngese sana wewe.. Sasa hizo za kila mtu na picha yake zinatoka wapi ilihali fomu za uchaguzi ni uniform
 
Sasa Askofu kila mtu akipiga picha, then tuanze kutafuta picha ya nani ndio sahihi? Tume ina lengo zuri kwamba taarifa za matokeo ziwe na channel moja, sio kila mtu na matokeo yake itakuja kuleta taharuki na hatimae vurugu.Endelea kuchunga kondoo wa Bwana mambo mengine haya kuhusu. Usichanganye siasa na dini
Boyaa wewe ,hayo maneno yako ungeyatamka kwa Gwajima!
 
Magufuli kakaya pumzi tume inataka kumbeba miaka yite amawakala wameingia na simu mwaka huu mr zero Magufuli wanataka kugeuza kila mtu mwendawazimu yaani watu wkubali kuibiwa asubuhi mchana peupe harafu wakubali hao CCM kweli wenda wazimu
 
SUALA LA SIMU KWA MAWAKALA: TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI MSIHARIBU UCHAGUZI WA WATANZANIA!

Taarifa kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi itazuia Mawakala wa Vyama kuingia na simu zao katika vituo vya kupigia kura imetushtua hata sisi viongozi wa Kanisa! Simu ina mambo mengi sana katika ulimwengu wa sasa ikiwemo kutunza kumbukumbu kwa njia mbalimbali.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi haiwezi kuwafanya mawakala kama 'tabula rasa' yaani watu wasioweza kuhifadhi kumbukumbu yo yote na hata kushindwa kuwasiliana. Mawakala wakiwa na simu wanaweza kupiga picha matokeo halisi ili kudhibiti wizi wa kura! Kitendo cha Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuzuia Mawakala kuingia na simu katika chumba cha kupigia kura ni sawa na kuandaa usiri utakaopelekea mazingira ya kuibiwa au kuchakachuliwa kwa kura!

Tunaitahadharisha Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuacha kutoa maelekezo au kutunga kanuni kwa lengo la kufanya Matokeo ya Uchaguzi Mkuu yasiheshimike na wananchi! Ili kuleta afya ni vizuri maelekezo na kanuni za Tume zikubaliwe na vyama vyote. Tume iepuke kutoa kanuni na maelekezo katika kipindi hiki kwa lengo la kuubeba upande mmoja na kuunyonga upande mwingine!

Sisi tumekwisha kutimiza wajibu wetu (Ezekieli 33:1-20).

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula - Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki na Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Makanisa ya Moravian ya Uamsho Duniani
Hawa maaskofu wengine wa aina hii sijui wanapatikana kwa vigezo gani imagine huyo anayesema hayo ni askofu anaetegemea kuongoza kondoo zake katika njia ya kwenda mbinguni sijui anawaza nini manake kwenye kituo Kuna mawakala na hata wagombea wanaweza kuwepo Sasa suala la. Kusema mawakala wapige picha matokea sijui haoni impact yake badae kuwa kila wakala anaweza kuwa na version yake ya kura kwa kweli viongozi wetu wa dini kuweni makini kwa dhamana mlio nayo ni kubwa Sana msitake sasa waumini tuanze kugawanyika kwa kuonyesha dhahiri mna ushabiki wa kisiasa ni vyema mkahubiri amani na kuombea uchaguzi uishe salama msiwe vyanzo vya vurugu manake hata nyie mtakua wahanga
 
Sasa Askofu kila mtu akipiga picha, then tuanze kutafuta picha ya nani ndio sahihi? Tume ina lengo zuri kwamba taarifa za matokeo ziwe na channel moja, sio kila mtu na matokeo yake itakuja kuleta taharuki na hatimae vurugu.Endelea kuchunga kondoo wa Bwana mambo mengine haya kuhusu. Usichanganye siasa na dini
Miaka yote simu zimetumika na hakukuwa na shida iweje mwaka huu Magfuli deadly drown out of the race atatijiju hakuna raisi
 
SUALA LA SIMU KWA MAWAKALA: TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI MSIHARIBU UCHAGUZI WA WATANZANIA!

Taarifa kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi itazuia Mawakala wa Vyama kuingia na simu zao katika vituo vya kupigia kura imetushtua hata sisi viongozi wa Kanisa! Simu ina mambo mengi sana katika ulimwengu wa sasa ikiwemo kutunza kumbukumbu kwa njia mbalimbali.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi haiwezi kuwafanya mawakala kama 'tabula rasa' yaani watu wasioweza kuhifadhi kumbukumbu yo yote na hata kushindwa kuwasiliana. Mawakala wakiwa na simu wanaweza kupiga picha matokeo halisi ili kudhibiti wizi wa kura! Kitendo cha Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuzuia Mawakala kuingia na simu katika chumba cha kupigia kura ni sawa na kuandaa usiri utakaopelekea mazingira ya kuibiwa au kuchakachuliwa kwa kura!

Tunaitahadharisha Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuacha kutoa maelekezo au kutunga kanuni kwa lengo la kufanya Matokeo ya Uchaguzi Mkuu yasiheshimike na wananchi! Ili kuleta afya ni vizuri maelekezo na kanuni za Tume zikubaliwe na vyama vyote. Tume iepuke kutoa kanuni na maelekezo katika kipindi hiki kwa lengo la kuubeba upande mmoja na kuunyonga upande mwingine!

Sisi tumekwisha kutimiza wajibu wetu (Ezekieli 33:1-20).

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Mkuu Emmaus Bandekile Mwamakula - Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki na Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Makanisa ya Moravian ya Uamsho Duniani
wanataka kuwanyima nakala maana simu ni njia mbadala ya mawasiliano hawataki uchaguzi uwe wa haki
 
Hawa maaskofu wengine wa aina hii sijui wanapatikana kwa vigezo gani imagine huyo anayesema hayo ni askofu anaetegemea kuongoza kondoo zake katika njia ya kwenda mbinguni sijui anawaza nini manake kwenye kituo Kuna mawakala na hata wagombea wanaweza kuwepo Sasa suala la. Kusema mawakala wapige picha matokea sijui haoni impact yake badae kuwa kila wakala anaweza kuwa na version yake ya kura kwa kweli viongozi wetu wa dini kuweni makini kwa dhamana mlio nayo ni kubwa Sana msitake sasa waumini tuanze kugawanyika kwa kuonyesha dhahiri mna ushabiki wa kisiasa ni vyema mkahubiri amani na kuombea uchaguzi uishe salama msiwe vyanzo vya vurugu manake hata nyie mtakua wahanga
Anasema ukweli maana hataki kuruhusu Magufiri aingize nchi kwenye lindi la damu kwa uroho wake wa madaraka
 
Back
Top Bottom