Taarifa Juu ya Hoja za Ukaguzi kuhusu Hesabu za Fedha za ACT Wazalendo Kutokana na Taarifa ya CAG

ACT Wazalendo

JF-Expert Member
May 5, 2014
605
1,536
Taarifa Juu ya Hoja za Ukaguzi kuhusu Hesabu za Fedha za ACT Wazalendo Kutokana na Taarifa ya CAG ya mwaka unaoishia June 2016

Tumesoma Taarifa ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuhusu hoja za ukaguzi wa Chama cha ACT Wazalendo za mwaka 2014/15. Tunapenda kuwajulisha wanachama wetu kuwa hoja hizi za CAG ni za hesabu za mwaka 2014/15 na sio hoja za Sasa za 2015/16. Ukaguzi wa mwaka 2015/16 bado.

Hoja hizi zote zilizoibuliwa na CAG tulizijibu pamoja na kuwasilisha hesabu za mwaka 2015/16 kwaajili ya Ukaguzi. Kama kawaida yetu, tutaweka Taarifa hii ya 2014/15 ya ukaguzi pamoja na majibu yetu wazi kwenye tovuti ya Chama siku ya Jumatano tarehe 19 Aprili, 2017, ambao pia Kamati ya Fedha itatoa maelezo kwa wanachama wa ACT Wazalendo na Watanzania kwa ujumla juu ya Masuala kadhaa yaliyoibuliwa katika ripoti ya CAG kwa hesabu za mwaka 2014/15.

Venance Msebo
Mwenyekiti Kamati ya Fedha - ACT Wazalendo
April 15, 2017
 
Mm wao wana Mbunge mmoja TZ hata mtoto wa Darasa la nne anaweza akatoa ufafanuzi ktk Mapato na matumizi ya ACT labda kama wanafadhiliwa na nchi chonganishi
 
Mm wao wana Mbunge mmoja TZ hata mtoto wa Darasa la nne anaweza akatoa ufafanuzi ktk Mapato na matumizi ya ACT labda kama wanafadhiliwa na nchi chonganishi
Unaweza kukuta wanapata ruzuku ya laki mbili,sasa hiyo kweli mpaka waitolee ufafanuzi
 
Maswala gani ya Ufisadi yaliyoibuliwa na CAG, tusaidie tuweze kujua kwa ufupi namna Zitto anavyotafuna hela ya maskini kwa mambo yake.

Afu Venance Msebo ungemwambia Kiongozi wenu Mkuu Ayattollah Zitto ajiongeze na huku awe anajitengeneza kitaalam kama alivyodai Polisi wakitaka kumkamata hawawezi kumpata maana anatumia nguvu giza hadi wanaona Ziwa Tanganyika badala yake. Sasa Kwa nini hiyo dawa asiitumie na huku ili wakati CAG anakagua asiweze kuibua chochote ila aone karatasi ni nyeupe tu ???
 
Wanapata ruzuku ya laki unusu
Ningekuwa Mimi CAG hata ofisini kwao nisingeingia,ningekuwa nawahojia dirishani tu wenye we wakiwa ndani ya ofisi yao

Lakini Kitila Mkumbo sasa ana mshahara mkubwa,atakuwa anawasaidia,hata akipata safari za mkoani anaweza kumbeba mwana ACT akaeneze Chama

Pia tunataraji kila mkumbo atasaidia kuimarisha tawi la ACT wazalendo Dodoma
 
Hawa jamaa wanakaguliwa nini? Duu kweli hii nchi ina mambo
 
kuna maofisa wa cag wanakula allowance na wanachoma mafuta na per diem juu kwenda kukagua laki na nusu ya act wazalendo

kama ni kweli aliyeturoga kweli amekufa
 
kuna maofisa wa cag wanakula allowance na wanachoma mafuta na per diem juu kwenda kukagua laki na nusu ya act wazalendo

kama ni kweli aliyeturoga kweli amekufa
Kulipa mishahara wameshindwa mpaka serikali imeamua kuchukua afisa wao mmoja imuajiri ili ajikimu.

Laki na nusu unachoma mafuta? Bora uwaambie watume document kwa wasapu au telegramu au wampe mtu wa bodaboda azilete
 
Mbona hawajajibu kuhusu halmashauri yao ya kigoma ujiji
Ujiji wale wazee wa pale ni kiboko,wanawapiga vyombo watumishi wa pale balaa,wanajua mpaka tarehe za kufata hela benki,ukizitoa tu,utaona wazee wanaita na kugawana,chuma ulete ni shida
 
Back
Top Bottom