Taarifa Fupi kuhusu Kazi za Maendeleo Jimboni Ubungo (AMUA)

Wenzio wa Bonyokwa hawataki hata kukuona. Kiswigo humu kalalamika mpaka kakaukiwa na sauti. Mbunge wewe siyo msikivu.
 
Hoja yako nzuri ila wapo watu wanakusifia kwa kukutia ujinga. ukweli ni kwamba tatizo la maji nisugu na limatukela wengi fanya kazi shungulikia maji, pia huja fanya chochote kuhusu ajira. timiza ahadi wananchi tunataka kuona utekelezaji wa AMUA sio watusi kwa kikwete.
 
Daima amekuwa mtu wa maneno mengi na sio vitendo! Azipokee changamoto na kuzifanyia kazi 2015 sio mbali.
 
Hoja yako nzuri ila wapo watu wanakusifia kwa kukutia ujinga. ukweli ni kwamba tatizo la maji nisugu na limatukela wengi fanya kazi shungulikia maji, pia huja fanya chochote kuhusu ajira. timiza ahadi wananchi tunataka kuona utekelezaji wa AMUA sio watusi kwa kikwete.
Unataka achimbe mitaro na kuweka mabomba mapya. Kazi yake ni kushinikiza serikali na anafanya hivyo, wacha uchawi.
 
Wenzio wa Bonyokwa hawataki hata kukuona. Kiswigo humu kalalamika mpaka kakaukiwa na sauti. Mbunge wewe siyo msikivu.

Wewe unajua kazi ya Mbunge? Laumu serekali na Ccm kwa kukaa madarakani miaka 50 hukuwatu wana shea maji na wanyama
 
Napokea kwa unyenyekevu pongezi zilizotolewa na wachangiaji mbalimbali hapa JF lakini izingatiwe kuwa michango yangu bungeni ni matokeo ya heshima mliyonipa ya kuwawakilisha. Aidha yapo maoni machache ambayo yametoa tafsiri tenge kuhusu kazi ya mbunge na wengine mmetaka nieleze nimefanya kazi gani za maendeleo jimboni Ubungo.

Tarehe kama ya leo 21 Agosti 2005 nilianza mchakato wa kuwa kugombea ubunge nikiwa kwenye chakula na watoto yatima, tarehe kama hiyo mwaka 2010 nilianza kampeni za uchaguzi mitaani Ubungo, tarehe hii hii kwa mwaka huu wa 2012 naomba niitumie kutoa taarifa fupi ya utekelezaji kwa masuala ya maendeleo katika mwaka wa fedha 2011/2012 uliomalizika tarehe 30 Juni 2012;
http://mnyika.blogspot.com/2012/08/taarifa-fupi-kuhusu-kazi-za-maendeleo.html kuhusu elimu, ajira, miundombinu, maji, usalama, uwajibikaji, ardhi na afya; taarifa ya kina ya utekelezaji nitaitoa nitakapotimiza miaka miwili ya utendaji.

Hivyo, ufanisi wa ubunge wangu upimwe kwa kuzingatia msimamo huu kuhusu kazi nne za mbunge katika kuwezesha maendeleo:
http://mnyika.blogspot.com/2010/03/natangaza-rasmi-dhamira-ya-kugombea.html ambao niliwaeleza wananchi wakati wa uchaguzi hivyo nilichaguliwa ikifahamika wazi kuwa huo ndio wajibu ambao nitautekeleza katika kipindi cha miaka mitano.

Bado naendelea kuamini kwamba jimbo la Ubungo na taifa kwa ujumla tutapiga hatua ya haraka zaidi ya maendeleo kupitia mabadiliko katika mifumo yetu ya mgawanyo wa rasilimali na usimamizi wa matumizi ya fedha za umma na pia kwa kuweka mazingira bora ya kisera, kisheria na kiutendaji wa sekta binafsi.Tuliyoyafanya mpaka sasa ni sehemu tu katika mahitaji makubwa ya maendeleo kutokana na pengo la miaka 50 ukilinganisha na fursa ambazo taifa letu linazo; hata hivyo naamini miaka mitatu iliyobaki itafanya miaka mitano ya kuisimamia Serikali iliyopo madarakani hivi sasa pamoja na udhaifu wote uliokuwepo kuleta tofauti katika maendeleo majimboni.

Ni katika muktadha huo wakati mwingine tunazimika kuwakilisha na kuwasilisha matakwa ya wananchi namna hii:
http://www.youtube.com/watch?v=ES4OMOD_xME tukiamini kwamba watawala wenye dhamana kwa sasa ya kukusanya kodi watasikiliza na kuzingatia vipaumbele vya maendeleo vya wananchi.Aidha, baada ya kazi mkutano wa nane wa bunge naomba kutumia fursa mjadala utakaofuatia taarifa hii kupata maoni yenu kuhusu masuala ninayopaswa kuyapa kipaumbele katika kuwawakilisha na kuwatumikia jimboni katika kipindi cha mwezi Septemba mpaka Oktoba 2012 kabla ya kuanza kwa mkutano wa tisa wa bunge na pia kuhusu maandalizi ya mwaka 2013.

Kero nyingi zinazoendelea kuwepo kwa sasa ni neema iliyojificha (blessing in disguise) ili tuendelee kuunganisha nguvu ya umma kuendeleza wimbi la mabadiliko. Narudia tena kuwakumbusha kuwa nguvu ile ile tuliyoitumia kwenye kutafuta kura na kulinda kura ndio naiomba toka kwenu katika hatua hii ya kufanya kazi za kuwezesha maendeleo kwa kutimiza wajibu kila mmoja wetu kwa nafasi yake, kuisimamia serikali na kuunganisha rasilimali za wadau wengine; Maslahi ya Umma Kwanza.

hongera mkuu kwa juhudi zako kutatua kero jimboni kwako. napenda kukumbusha shida kubwa ya maji inayowakabili wakazi wa mbezi mjimpya, mshikamano na makabe. mheshimiwa hali ni mbaya sana gharama ya maisha iko juu sana sababu ya shida kubwa ya maji. wakazi wa maeneo tajwa hawajui sababu inayosababisha maji yasisambazwe kwa wakazi wa maeneo haya. watu wanaishi kwa maji ya kununua mwaka mzima nayo upatikanaji wake umekuwa wa shida siku hizi hivyo kusababisha bei yake kupanda. kuna mchezo mchafu unafanywa na dawasa wa kufunga bomba kubwa lililopo mbezi mwisho na kulifungua wanapojisikia hivyo kuleta mateso makubwa kwa wakazi wa mbezi. pigania viosk vya maji vilivyopo mbezi mwisho, stop over na kwa yusufu vifungwe na badala yake mabomba yasambazwe kwenda majumbani kwa watu. huu mradi wa uuzaji maji kati ya dawasa na waliomilikishwa mabomba haya ni janga kwa wakazi wa mbezi. fanyia kazi mheshimiwa!
 
kila ninapokusikia bungeni, naamini kwamba Tanzania siyo kama inavyoonekana, kuna "vichwa" sema nafasi ya kutosha haijapatikana. Tuombe mungu moto mliouanzisha, utufikishe tunakotamani!

Mimi binafsi nakuombea makubwa zaidi ya Ubunge, ikiwezekana Uwaziri Mkuu, na hata "URAIS" maana bado 'unadai'

natamani ungekuwa mbunge wangu.

Mi ni Mwananchi wa Monduli
 
kila ninapokusikia bungeni, naamini kwamba Tanzania siyo kama inavyoonekana, kuna "vichwa" sema nafasi ya kutosha haijapatikana. Tuombe mungu moto mliouanzisha, utufikishe tunakotamani!

Mimi binafsi nakuombea makubwa zaidi ya Ubunge, ikiwezekana Uwaziri Mkuu, na hata "URAIS" maana bado 'unadai'

natamani ungekuwa mbunge wangu.

Mi ni Mwananchi wa Monduli

Na huku Jang'ombe je, ni vizuri nao wakina Mariam Msabaha na Raya Ibrahim nao wakatupa taarifa zao.

Asha
 
kila ninapokusikia bungeni, naamini kwamba Tanzania siyo kama inavyoonekana, kuna "vichwa" sema nafasi ya kutosha haijapatikana. Tuombe mungu moto mliouanzisha, utufikishe tunakotamani!

Mimi binafsi nakuombea makubwa zaidi ya Ubunge, ikiwezekana Uwaziri Mkuu, na hata "URAIS" maana bado 'unadai'

natamani ungekuwa mbunge wangu.

Mi ni Mwananchi wa Monduli

Wabunge wote waungane, moto uliowashwa uendelezwe
 
Mnyika yale yote ulioahidi hujatekeleza hata moja, ila kwa kupiga domo bungeni hilo umefanikiwa, nia yetu ya wakazi wa ubungo ni kutekeleza uliyotuahidi vinginevyo 2015 ukae mguu sawa ukalime.

duh, yani wewe ktk yote hayo umeona kupiga domo bungeni tu? wameshindwa ccm for 51years ataweza mnyika kwa miaka hii miwili? unazikumbuka ahadi za jk 2010? ametimiza kwa asilimia ngapi mpk sasa?
 
Kamanda mnyika safi sana kwa kazi unayofanya,sisi wakazi wa ubungo tupo pamoja na wewe na tunakuamini sana,tulianza na Mungu na tutamaliza na Mungu,wao wana pesa na risasi sisi tunaMUNGU anayetupigania.
 
Mkuu Mnyika,kwanza nakupongeza kwa juhudi zako na endelea hivyo hivyo
Tunashukuru leo upo nasi hapa kwenye forum. Nina ombi kwako mkuu wangu. Kwa niaba ya wapigakura wako wa kimara Matosa (kimara B) kuanzia kanisa la KKT kuelekea kigango cha Matosa hatujawahi kupata maji tangia hii miundo mbinu ya kichina imewekwa lakini wanzetu wengia kuanzia Temboni wanapata maji kwa mgao mara mbili kwa wiki.Tumejaribu kufuatilia hapo Kimara DAWASCO lakini majibu yake ni kuwa tupo kilimani na maji hayawezi kufika huko mpaka wapate kibali kutoka makao makuu ya kutupagia mgao wetu wenyewe lakini tangia tumefuatilia imekuwa subirini mpaka imechosha
hii ni tangia March mpaka leo wanasema tutapangia mgao wetu

Tutashukuru kwa hilo
 
hongera mnyika.. kazi unafanya. wanaokudiss wana chuki binafsi..ni wagen tu kwao vunjo kelele wanapigia ubungo...
 
Hoja yako nzuri ila wapo watu wanakusifia kwa kukutia ujinga. ukweli ni kwamba tatizo la maji nisugu na limatukela wengi fanya kazi shungulikia maji, pia huja fanya chochote kuhusu ajira. timiza ahadi wananchi tunataka kuona utekelezaji wa AMUA sio watusi kwa kikwete.

Hv kazi za mbunge ni kukutafutia ajira?kwanini usimuulize baba rizmoko hilo swali la ajira maana yeye ndiye atakuwa na jibu sahihi sio mbunge wetu bhana.
 
Narudia tena kuwakumbusha kuwa nguvu ile ile tuliyoitumia kwenye kutafuta kura na kulinda kura ndio naiomba toka kwenu katika hatua hii ya kufanya kazi za kuwezesha maendeleo kwa kutimiza wajibu kila mmoja wetu kwa nafasi yake, kuisimamia serikali na kuunganisha rasilimali za wadau wengine; Maslahi ya Umma Kwanza.


Hongera sana Mbunge wangu na waepukeni wasaliti mapema msikae nao karibu!!
 
Kuna tofauti Kati ya wabunge Kama Mnyika na wabunge Kama Ndesamburo.... Wewe ni Mbunge wa Chadema makao makuu,msemaji wa chama na sio msemaji wa wananchi....
Nakuombea ubadilike Kwa sababu taiga bado linakuhitaji Kwa mchango wako.......
 
54 Reactions
Reply
Back
Top Bottom