Mimi ni mwana jangwani mzuri sana, toka nina umri wa miaka minne. Sasa nina miaka 36 still naipenda Yanga sana. Kuna wakati naamua kuacha kuifuatilia but unakuta nashindwa kufanya hivyo. Sasa kuna huyu mfadhili wetu Yusuph Manji toka aje ameisaidia sana Yanga hilo halina ubishi. But at the same time amehusishwa na ufisadi mwingi unaotokea TZ. Sasa inasemekana anaanzisha chombo cha habari kwa ajili ya uchaguzi wa 2015 na ameanza na gazeti letu la Yanga Imara.
Sasa sisi washabiki wa Yanga ambao tupo kwenye upande wa wapinga ufisadi inatupa shida sana kwa sababu siamini katika msemo wa "baniani mbaya kiatu chake dawa". Naomba wapenzi wa Yanga ambao ni wachambuzi wa habari za siasa wachangie katika hili.
Sasa sisi washabiki wa Yanga ambao tupo kwenye upande wa wapinga ufisadi inatupa shida sana kwa sababu siamini katika msemo wa "baniani mbaya kiatu chake dawa". Naomba wapenzi wa Yanga ambao ni wachambuzi wa habari za siasa wachangie katika hili.