Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Sitta amechemka - Wanasheria
Siku moja baada ya Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, kutoa maoni yake kuhusu hukumu ya mahakama ya kimataifa ya usuluhishi wa migogoro ya kibiashara (ICC), iliyopipa ushindi kampuni ya Dowans dhidi ya shirika lka ugavi wa umeme nchini Tanesco, baadhi ya wanasheria wamedai mwanasiasa huyo amechemka.
Hukumu hiyo iliyotolewa hivi karibuni iliamuru Tanesco kuilipa Dowans kiasi cha Sh bilioni 185 kama fidia kwa kuvunja mkataba kati yake na shirika hilo.
Katika sehemu ya maoni na ushauri wake kwa serikali kuhusiana na hukumu hiyo, pamoja na mambo mengine, Sitta, pamoja na mambo mengine, alinukuliwa na vyombo vya habari juzi akisema,
hukumu iliyotolewa dhidi ya TANESCO ni mwendelezo wa hujuma kubwa dhidi ya taifa kwa vile inaonekana wazi kwamba kuna kundi la watu maarufu ambalo ndilo chanzo cha suala hilo, na ambalo kwa namna moja au nyingine lilishiriki kuhujumu mwenendo wa kesi ili serikali ishindwe, wao walipwe pesa.
Waziri huyo pia aliishauri serikali isilipe fidia hiyo iliyoamuliwa katika hukumu hiyo.
Hata hivyo baadhi ya wanasheria nchini jana walielezea kushangazwa kwao na kauli hizo za Sitta kwa kile walichodai kuwa zinaweza kuwahamasisha au kuwashawishi wananchi kuacha kutii amri na maamuzi ya sheria za kimataifa.
Mmoja wa wanasheria wa sheria za biashara nchini, Henry Chaula, alisema Sitta alikosea sana kutoa kauli hizo kwani serikali ya Tanzania inaendeshwa kwa kufuata utawala wa sheria.
Alisema serikali ilikubali yenyewe Tanesco kwenda katika mahakama hiyo, hivyo maamuzi yoyote yaliyotolewa mahakamani hawana budi kuyapokea.
Aliongeza kwamba madai ya kesi hiyo kuingiliwa na mafisadi hayana ukweli wowote kwani ilihusisha pande mbili tu, Tanesco na Dowans.
Serikali iliridhia sheria za mahakama hiyo, hivyo hukumu iliyotolewa haina shaka na serikali ilikubali, alisema mwanasheria huyo.
Mwanasheria mwingine kwa sharti la kutotajwa jina lake alisema:
Kama n I kweli Waziri Sitta amenukuliwa na hayo magazeti, basi mimi nasema Sitta amepotoka kwani yeye ni mwanasheria hakupaswa kutoa ushauri huo
Afadhali angesema Tanesco ikate rufaa au ikae chini na Doiwans wazungumze nao ./
Habari zaidi katika Tanzania Daima ya leo.
My Take (angalizo nilipohighlight in red):
1. Hii sasa ni project ya RA/EL na inaonyesha how the two are in full swing kutaka walipwe pesa.
2. By the way, who is Henry Chaula. Mwenye CV zake etc atujuze.
3. Anasema suala zima hilo halikuingiliwa na mafisadi sijui anaishi dunia gani, hii ya Tanzania kweli? Tumuulize kalipwa ngapi na RA/EL kuwapigia tarumbeta?
4. Mahakama hiyo ya kimataifa haitambuliwi kisheria za kimataifa kwani haiko chini ya chombo kama vile UN. Ni taasisi binafsi tu ya watu walioamua kufanya biashara ya kuamua kesi zitokananzo na migogoro ya kibiashara kwa kulipwa fees. Hiyo mahakama inayo uwezo kisheria ku-enforce hukumu zake? Kama vile zilivyo mahakama za nchi zilizowekwa kikatiba (eg High Court/Court of Appeal) za hapa kwetu kwa mfano?
5. Kutokana na hilo si kweli kukataa kulipa pesa hizo kunaweza kuhamasisha wananchi kuacha kutii amri na sheria za kimataifa. Kama serikali ilishindwa kutii amri za mahakama yake yenyewe chini ya katiba yake (eg kesi ya Valambhia) tayari ilihamasisha wananchi kutotii amri na sheria zake. Hii ya kimataifa is just nonsense!
6. Kwa ujumla kwa muda mrefu nimrkuwa na wasiwasi sana na mhariri mkuu wa T. Daima linapokuja suala la Richmond/Dowans mara nyingi anaonekana kujikita upande wa EL/RA. Makala zake kadha zimekuwa zina mwelekeo huo.