Syria: Waasi wauwa wanajeshi 40 wa serikali jimboni Idlib

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,007
9,873
Wizara ya ulinzi ya Urusi imesema waasi nchini Syria wamewauwa wanajeshi 40 wa serikali na kuwajeruhi wengine zaidi ya 80, katika mashambulizi waliyoyafanya katika jimbo la Idlib.

Shirika la habari la Urusi, Interfax limenukuu tangazo la wizara hiyo, lililosema kuwa waasi walizikamata kambi mbili katika shambulio mojawapo. Shirika la habari la Syria, SANA limearifu kuwa waasi walitumia miripuko ya kutegwa ndani ya magari na silaha nzito nzito katika mashambulizi hayo ya Idlib mapema leo, na kuongeza kuwa jeshi la serikali limepeleka vikosi vya msaada katika jimbo hilo.

Idlib ni jimbo la mwisho linalodhibitiwa na waasi nchini Syria, na mamia kwa maelfu ya raia wamelikimbia mnamo wiki za hivi karibuni, kuepuka mashambulizi yanayofanywa na ndege za Urusi na za serikali ya Syria dhidi ya waasi hao.
 
Hilo jimbo litakutana na kadhia kama ile ya Allepo na litarejeshwa tena chini ya himaya ya Assad, ni suala la muda tu.

Kinachoonekana ni kama vile Rais Edorgan wa Uturuki amewatosa wale waasi wa Idlib au tuseme amewatoa kafara kwa serikali ya Assad na Urusi kama gharama ya kurejesha uhusiano wake na Putin

Hivi vita vya Syria ni kama vile Assad ameshinda kijeshi ila changamoto kubwa kwake ni namna ya kujenga nchi maana imeharibika sana.
 
Hilo jimbo litakutana na kadhia kama ile ya Allepo na litarejeshwa tena chini ya himaya ya Assad, ni suala la muda tu.

Kinachoonekana ni kama vile Rais Edorgan wa Uturuki amewatosa wale waasi wa Idlib au tuseme amewatoa kafara kwa serikali ya Assad na Urusi kama gharama ya kurejesha uhusiano wake na Putin

Hivi vita vya Syria ni kama vile Assad ameshinda kijeshi ila changamoto kubwa kwake ni namna ya kujenga nchi maana imeharibika sana.
Kilichoikumba Aleppo ndo kinachoenda kutokea Idlib.Aleppo warusi walikuwa wanapiga mabomu yanafukua mkapa chini ya ardhi.yani muda sio mrefu tutaenda kununua vifusi kwenye mkoa wa Idlib

Sent from my itel S33 using JamiiForums mobile app
 
Hilo jimbo litakutana na kadhia kama ile ya Allepo na litarejeshwa tena chini ya himaya ya Assad, ni suala la muda tu.

Kinachoonekana ni kama vile Rais Edorgan wa Uturuki amewatosa wale waasi wa Idlib au tuseme amewatoa kafara kwa serikali ya Assad na Urusi kama gharama ya kurejesha uhusiano wake na Putin

Hivi vita vya Syria ni kama vile Assad ameshinda kijeshi ila changamoto kubwa kwake ni namna ya kujenga nchi maana imeharibika sana.
Kabisa Mzee Suala Lakuijenga Upya SYRIA Nizaidi Ya Changamoto Kwa Al Assad Na Washirika Wake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SYRIA ILISHATABIRIWA KUWA ITABAKI MAGOFU NAONA MAANDIKO YANAZIDI KUTIMIA BADO IRAN NAYO ITASAMBARATIKA HAPO MASHARIKI YA KATI
 
Back
Top Bottom