Sweden yamwaga mabilioni kusaidia elimu ya msingi

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Serikali ya Tanzania imepokea msaada wa Sh196 bilioni kwa ajili ya kusaidia utekelezaji wa awamu ya Pili ya Mpango wa Elimu kwa Matokeo unaohusu elimu ya Msingi (EP4R II).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Oktoba 5,2021 na kitengo cha mawasiliano cha Wizara ya Fedha na Mipango, Maktaba huo umesainiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Emmanuel Tutuba kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Balozi wa Sweden nchini Tanzania Anders Sjoberg kwa niaba ya Serikali ya Sweden.

Tutuba amesema msaada huo utasaidia utekelezaji wa mpango huo wa kuboresha elimu ya msingi kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia Julai, 2021 hadi Juni mwaka 2026.

Katika kutekeleza Mpango wa Elimu kwa Matokeo wa EP4R uliohusisha pia kuendeleza elimu ya msingi Awamu ya Kwanza, ulioanza mwaka 2014 hadi 2020, Sweden kupitia Shirika lake la Maendeleo SIDA, ilitoa kiasi cha sh208 bilioni.

Tutuba ametaja baadhi ya mafanikio ya utekelezaji wa Awamu ya Kwanza ya Mpango huo kuwa ni ujenzi wa madarasa, 10,409, mabweni 646, nyumba za walimu 91, majengo ya utawala 37, maktaba 49, maabara 29, uzio 3 na visima vya maji katika shule za msingi 16.

Mengine ni ujenzi wa ofisi 155 za udhibiti wa ubora wa shule, ujenzi wa shule mpya 44, ukarabati wa shule kongwe 86, ununuzi wa magari 347 kwa ajili ya halmashauri zote za wilaya, ofisi za wilaya za udhibiti wa ubora wa shule, maafisa elimu wa mikoa, Baraza la Mitihani la Taifa na vyuo.

Kwa upande wake, Balozi wa Sweden nchini Anders Sjoberg amesema kuwa nchi yake inafadhili kwa mara nyingine uboreshaji wa elimu ya msingi ambapo mpango huo umelenga kuwanufaisha wanafunzi milioni 16.

Amebainusha mpango wa awali ulilenga zaidi kuwanufaisha Watoto wa kike lakini mpango huu mpya utawanufaisha wanafunzi wote wakiwemo wenye mahitaji maalum na kuwawezesha kuhitimu masomo yao kwa ajili ya manufaa yao na Taifa kwa ujumla.

Sjoberg amesema kuwa EP4R Awamu ya Kwanza imefanikisha kujenga mifumo imara ya elimu ya msingi kwa kuweka miundombinu mahsusi na maendeleo ya kimkakati itakayoisaidia nchi kuboresha elimu kwa miongo mingi ijayo.

Chanzo: Mwananchi
 
Si tuliambiwa humu, NA MAKAMANDA, kuwa nchi za Scandinavia zote zitaigeuzia kisogo Tanzania kwasababu ya kumkamata mwenyekiti wa maisha?!!!!

Ni jambo jema lililobaki ni kuzisimamia vema fedha hizo zifanye yaliyokusudiwa na siyo watu kujipigia tu kama walivyofanya kwenye EQUIP (zimepigwa sana sana huku jitihada za kuleta yale mabadiliko zikiwa ndogo mno huko vituoni; watu wakishapata maposho wanarudi vituoni na kuendelea na business as usual matarajio ya mafunzo yote wanayaacha hukohuko)

Lakini pia, mama Samia, hebu fanya hizi kesi za madarasa kuwa historia mama. Huu ni mwaka wangu wa 25 tangu niwe na akili za upembuzi na kila siku katika miaka yote hiyo sikomi kusikia habari za madarasa.......mpaka inanikera sasa!!!! Ikija misaada ya wahisani km hivyo utasikia habari za madarasa, serikali utasikia habari za madarasa, wananchi utasikia habari za kujitolea kujenga madarasa hadi leo n.k. KUNA TATIZO GANI?!!!!!
 
Kama serikali bado inapokea hii misaada kwanini wasifute zile tozo za miamala ya simu?

Huku wanaomba "mikopo nafuu", kule wanapokea misaada, hapa wanatukamua wananchi kwenye tozo, hawa watu hata siwaelewi.
Mimi naona tozo ziendelee ila iwe imetosha kwa upande wa mambo ya madarasa na badala yake sasa zielekezwe katika utatuzi wa changamoto zingine za kijamii kama mabarabara huko vijijini
 
Serikali ya Tanzania imepokea msaada wa Sh196 bilioni kwa ajili ya kusaidia utekelezaji wa awamu ya Pili ya Mpango wa Elimu kwa Matokeo unaohusu elimu ya Msingi (EP4R II)...
Usiseme Sweeden Kibwetele wew sema Mabeberu ya mwaga misaada. Halafu mkivimbiwa misaada hapo Lumumba mnaanza kuharisha mdomoni mara ooh sisi donor country, ooh Mabeberu yanatunyonya ooh hatutaki misaada ya mashoga.

Halafu pesa hizo hizo ndizo mnazo ringishia na kutishia watu kuwa hamzipeleki sehemu ambapo wananchi wenye Akili wamewachagua wapinzani mamaaaee zen.
CC jiwe bovu
 
Kuelekea uchaguzi mkuu serikali ya Tz ilipewa mkopo na WB kujenga shule za sekondari emu nionyesheni hata tofali moja lilioundwa kwa ile pesa.

Pesa yoote ilipelekwa kwenye uchaguzi wa kujaza kula kwenye maboksi.

Wapinzani waliupinga ule mkopo lakini wapiiii hata hizi nazo zikibadilishiwa matumizi siwezi shangaa
 
Serikali ya Tanzania imepokea msaada wa Sh196 bilioni kwa ajili ya kusaidia utekelezaji wa awamu ya Pili ya Mpango wa Elimu kwa Matokeo unaohusu elimu ya Msingi (EP4R II)...
sasa tunataka tuone kweli fedha hizo zinaleta mabadiliko chanya ktk Elimu yetu ya Msingi.

Wasimamizi wetu wa Elimu tunawaomba msilale, tumieni jitihada zenu zote kuhakikisha vikwazo/vhqngamoto zote ktk Elimu yetu ya msingi zinatatuliwa.
 
Misaada hii inatudumaza kifikra na kimtazamo, hivi kweli bilioni 196 kwa miaka mitano sisi wenyewe hatuwezi kuipata! Tusifurahie bali ni jambo la kuhuzunisha kwa kweli.

Spirit tuliyoianza kuhusu tozo japo wengine wanalalamika ndiyo njia sahihi kama taifa huru, maana wenzetu ni kupitia staili hizi ndio wanapata uwezo wa kutupa misaada.

Kukataa kuitwa mnyonge ni vitendo na sio mdomoni tu. Bado weupe wanatuona wanyonge na mtu anapokea msaada kwa furaha utadhani ni ushindi, dah! Kaaaz kweli kweli. Nadhani tozo ziendelee tu.
 
Kama serikali bado inapokea hii misaada kwanini wasifute zile tozo za miamala ya simu?

Huku wanaomba "mikopo nafuu", kule wanapokea misaada, hapa wanatukamua wananchi kwenye tozo, hawa watu hata siwaelewi.
Misaada hii inatokana na tozo na kodi wanazolipa wananchi wa nchi nyingine.
Hatuwezi kuishi maisha yetu yote tukitegemea misaada.
Ni vizuri nasi tujenge mazoea ya kulipa na kodi na tozo bila malalamiko.
Malalamiko yawe pale tunapobaini ufisadi wa kodi zetu.
 
Serikali ya Tanzania imepokea msaada wa Sh196 bilioni kwa ajili ya kusaidia utekelezaji wa awamu ya Pili ya Mpango wa Elimu kwa Matokeo unaohusu elimu ya Msingi (EP4R II).

Chanzo: Mwananchi
Mkuu beth, asante kwa taarifa hii, Waswidi siku zote ni wazuri kwetu. Waangalie hapa

P
 
Usiseme Sweeden Kibwetele wew sema Mabeberu ya mwaga misaada. Halafu mkivimbiwa misaada hapo Lumumba mnaanza kuharisha mdomoni mara ooh sisi donor country...
Mwmbie Lisu arudi tu maana kazi imemshinda
 
Serikali ya Tanzania imepokea msaada wa Sh196 bilioni kwa ajili ya kusaidia utekelezaji wa awamu ya Pili ya Mpango wa Elimu kwa Matokeo unaohusu elimu ya Msingi (EP4R II).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Oktoba 5,2021 na kitengo cha mawasiliano cha Wizara ya Fedha na Mipango, Maktaba huo umesainiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Emmanuel Tutuba kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Balozi wa Sweden nchini Tanzania Anders Sjoberg kwa niaba ya Serikali ya Sweden.

Tutuba amesema msaada huo utasaidia utekelezaji wa mpango huo wa kuboresha elimu ya msingi kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia Julai, 2021 hadi Juni mwaka 2026.

Katika kutekeleza Mpango wa Elimu kwa Matokeo wa EP4R uliohusisha pia kuendeleza elimu ya msingi Awamu ya Kwanza, ulioanza mwaka 2014 hadi 2020, Sweden kupitia Shirika lake la Maendeleo SIDA, ilitoa kiasi cha sh208 bilioni.

Tutuba ametaja baadhi ya mafanikio ya utekelezaji wa Awamu ya Kwanza ya Mpango huo kuwa ni ujenzi wa madarasa, 10,409, mabweni 646, nyumba za walimu 91, majengo ya utawala 37, maktaba 49, maabara 29, uzio 3 na visima vya maji katika shule za msingi 16.

Mengine ni ujenzi wa ofisi 155 za udhibiti wa ubora wa shule, ujenzi wa shule mpya 44, ukarabati wa shule kongwe 86, ununuzi wa magari 347 kwa ajili ya halmashauri zote za wilaya, ofisi za wilaya za udhibiti wa ubora wa shule, maafisa elimu wa mikoa, Baraza la Mitihani la Taifa na vyuo.

Kwa upande wake, Balozi wa Sweden nchini Anders Sjoberg amesema kuwa nchi yake inafadhili kwa mara nyingine uboreshaji wa elimu ya msingi ambapo mpango huo umelenga kuwanufaisha wanafunzi milioni 16.

Amebainusha mpango wa awali ulilenga zaidi kuwanufaisha Watoto wa kike lakini mpango huu mpya utawanufaisha wanafunzi wote wakiwemo wenye mahitaji maalum na kuwawezesha kuhitimu masomo yao kwa ajili ya manufaa yao na Taifa kwa ujumla.

Sjoberg amesema kuwa EP4R Awamu ya Kwanza imefanikisha kujenga mifumo imara ya elimu ya msingi kwa kuweka miundombinu mahsusi na maendeleo ya kimkakati itakayoisaidia nchi kuboresha elimu kwa miongo mingi ijayo.

Chanzo: Mwananchi
Ni muendelezo wao mkuu wa kufashili ujenzi wa shule..

Kale kapesa alikosema mama ndio hako sasa 😆😆

Screenshot_20211006-075909.png
 
Kuna kipindi jamaa waliomba msaada wakapelekewa mabilioni wakahamisha yote wakaiba yakarudi tena kwa Waswede🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom