Swali tamu kidogo; Je hakuna anayefikiria kumpeleka Mkurugenzi wa TANESCO mahakamani.

herzegovina

JF-Expert Member
Oct 28, 2015
3,129
4,712
Salaam,
Juzi usiku, wafanyakazi wa TANESCO wakijitambulisha kama maafisa wa jeshi la polisi, walifika nyumbani kwa mwandishi wa habari, Emmanuel Kibiki na kumpekua nje ya muda uliowekwa kisheria na kisha kuondoka naye halafu wakamkabishi polisi baada ya zaidi ya masaa kumi na mbili.

Hapa Mkurugenzi wa TANESCO amevuka mipaka. Amepata wapi mamlaka ya kuwatuma vijana wake kupekua na kukamata bila kulishirikisha jeshi la polisi?

Kama TANESCO wana malalamiko, vyombo vya kutoa haki si vinajulikana? Kwanini hawakwenda kama wamechafuliwa??

Kwa waandishi wa habari, wanaharakati na wadau wa demokrasia, je hakuna haja ya kumfikisha mahakamani huyu Mkurugenzi wa TANESCO ? Jeshi la polisi nalo, je wameridhia TANESCO kuwasaidia kupekua na kukamata??

Kwanini Jeshi la Polisi halijalaani kitendo cha wafanyakazi wa TANESCO kujitambulisha kama maafisa wa polisi?.

Wito kwa wanahabari, ukifuatwa na TANESCO kabla hujafungua ita wenzako. Kama TANESCO watataka kuondoka na wewe basi wenzako wakusindikize hadi kituoni..haya mambo ya TANESCO kukupeleka wanapojua kwanza bila hata polisi kujua ni hatari.

Ni vizuri kuanza na huyu Mkurugenzi

Nawasilisha

Mods nisaidieni kuweka alama ya kuuliza kwenye title
 
Tansesco wanafanya kazi kubwa sana kuzuia wizi wa umeme kuliko kenya.Ona wizi wa umeme kenya ulivyokubuhu
 
Tansesco wanafanya kazi kubwa sana kuzuia wizi wa umeme kuliko kenya.Ona wizi wa umeme kenya ulivyokubuhu

Huyu mtu sijui ni mwehu!!? Hivi hakuna jirani yake akamwelekeza hospitali ya vichaa pale Dodoma jamani? JF tumchangie mwenzetu apone. Kwa akili hizi kuna siku mtakuta amenyonga mtoto wake au Wa jirani yake ndo mtakumbuka kuwa ni mgonjwa.
 
Jamani jamani hali sasa ni tete kabisa. Hivyo ikitokea watu wanabisha hodi usiku hakuna kufungua mlango, wasubiri hadi kuche. Maana sasa ukiingia mikononi mwa wasiojulikana halafu ukaachwa hai basi utakuwa na mzimu mkali.
 
Salaam,
Juzi usiku, wafanyakazi wa TANESCO wakijitambulisha kama maafisa wa jeshi la polisi, walifika nyumbani kwa mwandishi wa habari, Emmanuel Kibiki na kumpekua nje ya muda uliowekwa kisheria na kisha kuondoka naye halafu wakamkabishi polisi baada ya zaidi ya masaa kumi na mbili.

Hapa Mkurugenzi wa TANESCO amevuka mipaka. Amepata wapi mamlaka ya kuwatuma vijana wake kupekua na kukamata bila kulishirikisha jeshi la polisi?

Kama TANESCO wana malalamiko, vyombo vya kutoa haki si vinajulikana? Kwanini hawakwenda kama wamechafuliwa??

Kwa waandishi wa habari, wanaharakati na wadau wa demokrasia, je hakuna haja ya kumfikisha mahakamani huyu Mkurugenzi wa TANESCO ? Jeshi la polisi nalo, je wameridhia TANESCO kuwasaidia kupekua na kukamata??

Kwanini Jeshi la Polisi halijalaani kitendo cha wafanyakazi wa TANESCO kujitambulisha kama maafisa wa polisi?.

Wito kwa wanahabari, ukifuatwa na TANESCO kabla hujafungua ita wenzako. Kama TANESCO watataka kuondoka na wewe basi wenzako wakusindikize hadi kituoni..haya mambo ya TANESCO kukupeleka wanapojua kwanza bila hata polisi kujua ni hatari.

Ni vizuri kuanza na huyu Mkurugenzi

Nawasilisha

Mods nisaidieni kuweka alama ya kuuliza kwenye title
Mamlaka anayapata kwa Boss yake aliyemteua....
 
Huyo mwandishi wa habari nasikia pia ni mwanasheria... naamini ataenda mahakamani kwa tafsiri zaidi za kisheria.
 
Hiyo mwandishi wa habari nasikia pia ni mwanasheria... naamini ataenda mahakamani kwa tafsiri zaidi za kisheria.
Na aungwe mkono....sema tatizo ni kuwa aliambiwa aripoti polisi asubuhi ya kesho yake. Itakuwa kama Roma tu
 
Jamani jamani hali sasa ni tete kabisa. Hivyo ikitokea watu wanabisha hodi usiku hakuna kufungua mlango, wasubiri hadi kuche. Maana sasa ukiingia mikononi mwa wasiojulikana halafu ukaachwa hai basi utakuwa na mzimu mkali.

Ukiwa na mashaka na watu wasiojulikana wako kwako usiku ..piga mbiu ya mwizi tu raia tutawakomesha pumbavu vibaraka na wajinga sana hawa..wanacheza na maisha yetu kama wanachezea doli....hakuna namna tena tumezidi kuchekeana na kuoneana kijingajinga. Woga nao ukizidi ni dhambi mbele ya Muumba wa vyote hapendi huu ujinga wa kuogopana hakuna cha wasiojukikana wala ***** mkurugenz... tutamalizana mtaana tu. Na nao waliowatuma watasikia wasiopenda kuyasikia.
 
Miongoni mwa skills muhimu kujifunza ni namna ya kutumia bunduki, na kama unauwezo jitahidi uimiliki (kihalali). Ukiwa na cha moto kunakua na "mutual respect"
 
Back
Top Bottom