Swali Muhimu kwa MHE WAZIRI MKUU PINDA Leo

BEHOLD

JF-Expert Member
Nov 17, 2013
5,057
10,715
Mheshimiwa WAZIRI MKUU,

Kumekuwepo malalamiko mengi kwa muda mrefu ndani na nje ya Bunge juu ya Utendaji usio ridhisha wa baadhi ya wizara na mawaziri wake,

Kwa bahati mbaya mawaziri waliochini ya ofisi yako wamekuwa ndio vinara kwa kulalamikiwa jambo lililopelekea Bunge hili kupitisha azimio la kutaka wajitathmini kama wanafaa kuendelea na nyadhifa hizo.

Lakini wewe kama Waziri Mkuu ni dhahiri kuwa sio tu unashindwa kuzisimamia wizara zilizo ndani ya ofisi yako bali hata nyinginezo kwa mujibu wa madaraka na wajibu wako kikatiba,

Je? Huu Si Muda Muafaka wa Wewe KUJIUZULU?
 
Ntalia jaman hata kama muda kalikobaki si mniache nimalize, mbona. Na nyie huko majimboni kwenu mmeshindwa je mmeshajiuzuru? Au shida ni uwaziri mkuu
 
Mheshimiwa WAZIRI MKUU,

Kumekuwepo malalamiko mengi kwa muda mrefu ndani na nje ya Bunge juu ya Utendaji usio ridhisha wa baadhi ya wizara na mawaziri wake,

Kwa bahati mbaya mawaziri waliochini ya ofisi yako wamekuwa ndio vinara kwa kulalamikiwa jambo lililopelekea Bunge hili kupitisha azimio la kutaka wajitathmini kama wanafaa kuendelea na nyadhifa hizo.

Lakini wewe kama Waziri Mkuu ni dhahiri kuwa sio tu unashindwa kuzisimamia wizara zilizo ndani ya ofisi yako bali hata nyinginezo kwa mujibu wa madaraka na wajibu wako kikatiba,

Je? Huu Si Muda Muafaka wa Wewe KUJIUZULU?
CC: john Mnyika TUMAINI Makene freeman MBOWE
 
Last edited by a moderator:
Wewe tatizo lako lipo wapi hii ndio nchi yetu hata mawaziri wanafanya kazi kwa mujibu wa vichwa vyetu vibovu vilivyo kuwa havina elimu hata ya kujua haki zetu!unatarajia nini afanye waziri mkuu?hii ndio nchi yetu kila mtu ataishi kwa mujibu wa njia zake anazo weza kupata chakula ilimradi mambo yanakwenda siku zinakwenda stop complaing like baby
 
ikitokea hyo najiuwa mie pm ajiuzulu?kisa utendajiwake mbovu?kama alishindwa ile ya liwalo na liwe na ulimboka akawashwa ,wauwaji wa albino wauwawe ,kula za zito?
 
Mheshimiwa WAZIRI MKUU,

Kumekuwepo malalamiko mengi kwa muda mrefu ndani na nje ya Bunge juu ya Utendaji usio ridhisha wa baadhi ya wizara na mawaziri wake,

Kwa bahati mbaya mawaziri waliochini ya ofisi yako wamekuwa ndio vinara kwa kulalamikiwa jambo lililopelekea Bunge hili kupitisha azimio la kutaka wajitathmini kama wanafaa kuendelea na nyadhifa hizo.

Lakini wewe kama Waziri Mkuu ni dhahiri kuwa sio tu unashindwa kuzisimamia wizara zilizo ndani ya ofisi yako bali hata nyinginezo kwa mujibu wa madaraka na wajibu wako kikatiba,

Je? Huu Si Muda Muafaka wa Wewe KUJIUZULU?

Nugu yangu BEHOLD kwanza nashukuru sana kwa swali lako zuri sana, mimi kama waziri mkuu sioni kama ipo haja ya mimi kujitathimini kwa sababu ifike mahali tuseme ule ukweli kabisa,ukiangalia mawaziri wanaopigiwa kelelele na waheshimiwa wabunge si kweli kabisa eti wameshindwa kudeliver hapana kabisa,wamefanya kazi kwa weledi na katika mazingira magumu sana nadhani wewe huwezi kuliona.

Kwa sasa mfono tumeongeza mikoa na halmashauri mpya za wilaya na miji midogo, mheshimiwa Hawa Ghasia kama waziri wa TAMISEMI amejitahidi sana kunisaidia katika utendaji wangu wa kila siku,changamoto hazikosekani cha msingi tusaidiane ili tusonge mbele, na wa kutusaidia ni ninyi wabunge wenyewe.Sasa mnapokuja hapa na kutoa kasoro ambazo mheshimiwa waziri hakuzipata mapema nyie mnazifanya kama tuhuma.

Nikija kwa mheshimiwa Engineer Chiza waziri wangu wa kilimo, jamani mnataka kusema kweli hajafanya lolote? Jamani ifike mahali tuweke na ubinadamu, namfahamu sana mheshimiwa Engineer Chiza ni mchapakazi na mnyenyekevu sana, kisa cha kusema eti hajatembelea mkoa fulani si haki kabisa kwa sababu wizara ya kilimo na chakula ina katibu mkuu na naibu katibu mkuu, hao ni watendaji wa wizara na wameshafika kwenye mkoa husika zaidi ya mara 5 sasa jamani mnataka yeye afike mwenyewe mumuone kwa macho ndiyo mridhike.

Nikija kwa mheshimiwa Prof wangu Jumanne Maghembe nae mnajua kabisa changamoto za maji mfano katika jini la Dar es salaam hayawezi kuyamaliza kwa mpigo tunafanya kwa awamu lakini huku tukiangalia na ukubwa wa tatizo lenyewe,tumepata wahisani wameahidi kutuongezea nguvu na nina imani kufikia mwaka 2015 ahadi zote za mheshimiwa rais zitakuwa zimetekelezwa.Jamani mnataka tufanye nini zaidi ya hilo, nadhani tufike mahali penye sifa pasemwe siyo kila kitu kupinga tu. Hayo ndiyo maneno ya waziri mkuu anajibu huku akishika shika miwani na mwisho wabunge wote wa CMM wanagonga meza na kazi inakuwa imekwisha
 
Na wapigwe tu, maana tumechoka sasa! Na watanzania tutakoma kuchagua waliochoka maana tunajitakia wenyewe.....
 
Kapiga chenga Swali!

Kweli Pinda kachoka. Anasema Rais au Bunge wanaweza kumuamulia hatima yake na atakuwa happy tu!

Labda ndio principle ya "LIWALO,......"
 
pinda apewe heshima yake anafaa sana amekuwa kioo cha uvumilivu na utendaji uliotukuka.
 
Kapiga chenga Swali!

Kweli Pinda kachoka. Anasema Rais au Bunge wanaweza kumuamulia hatima yake na atakuwa happy tu!

Labda ndio principle ya "LIWALO,......"
hapo kapiga chenga kivipi sasa wakati swali kalijubu na majibu yake umeyabainisha wewe mwenyewe.
 
Mheshimiwa WAZIRI MKUU,

Kumekuwepo malalamiko mengi kwa muda mrefu ndani na nje ya Bunge juu ya Utendaji usio ridhisha wa baadhi ya wizara na mawaziri wake,

Kwa bahati mbaya mawaziri waliochini ya ofisi yako wamekuwa ndio vinara kwa kulalamikiwa jambo lililopelekea Bunge hili kupitisha azimio la kutaka wajitathmini kama wanafaa kuendelea na nyadhifa hizo.

Lakini wewe kama Waziri Mkuu ni dhahiri kuwa sio tu unashindwa kuzisimamia wizara zilizo ndani ya ofisi yako bali hata nyinginezo kwa mujibu wa madaraka na wajibu wako kikatiba,

Je? Huu Si Muda Muafaka wa Wewe KUJIUZULU?

muuliza swali mwenyewe ni mzigo amejaa kwenye kiti lakini hakuna anachofanya nenda kwa wananchi wake hakuna cha maana alichofanya.
 
Pinda kasema yupo tayari kuondolewa ktk nafasi yake,kasema bunge linao uwezo huo na kama wabunge wanaona hafai watumie utaratibu uliopo kumuondoa na yeye atafurahi kwa kuwa kazi ya uwaziri mkuu ni 'nzito'sana. My take:kama kweli mh.Pinda anaona kazi ya uwaziri mkuu ni ngumu ngumu kwa nini asijiuzulu mwenyewe?
 
Back
Top Bottom