Swali: Mliofanikiwa kutumia mifuko mipya, inafaa kwa kubebea mboga yenye majimaji?(nyama au samaki) au unga wa kula?

Mzee Mapenzi

Senior Member
Jan 9, 2019
122
439
Binafsi sijaitumia ila nimefanikiwa kuiona sehemu mbalimbali ikiuzwa kwa wingi sana.
Nilipojaribu kuichunguza kwa makini nilipata walakini kama inaweza kuhifadhi mboga kwa usalama na isiwe na matokeo mabaya kwa mbebaji. Niliona pia kutakuwa kuna tatizo kwa wale wanapima unga wa kula kwa kilo, sioni kama mifuko ile ni rafiki kwa kuhifadhi ili utoke nao dukani hadi nyumbani (mliofanikiwa kuiona nadhani mlijiuliza swali hilo pia) lakini nikajiuliza wamama wanaobeba mchele toka sokoni hadi nyumbani pia kutakuwa kuna hitilafu kidogo kwenye chakula chao.

Mifuko ile ni ya nyuzinyuzi na sio karatasi (japo sijui kama imethibitiswa au ni watu wanatumia fursa).

Kwa haraka haraka nimeona ile inafaa kubebea nguo ukitoka dukani ila si mboga ama chakula cha kupima.(mliotumia nisahihisheni kama nipo tofauti).


Hili swala lisichuliwe kirahisi, linahitaji umakini sana kuendelea kulinda afya za watu na mazingira kiujumla.

Tusijekuwa tunamwita Dulla badala ya Abdalah.
 
hapa dawa ni kwenda na sufuria kbsa kwa mangi, walianza na viroba, sasa rambo hawa jamaa wanaturudisha kwenye ujima, washatuona sisi ma zinjatropous, sasa na watapikaji nao watembee na masemosiii?, tukikubali watahamia kwenye condom watatuletea za bati.
 
Wahenga wenzangu nadhani hawato pata tabu kukubaliana na mabadiliko haya ya kurudi kwenye matumizi ya vifungashio vya zamani kabla ya plastic bags.
Sikuzile tulitumia vikapu, magazeti pamoja na mifuko ya kaki kwaajili ya kubebea mahitaji yote ya dukani na sokoni.
 
Binafsi sijaitumia ila nimefanikiwa kuiona sehemu mbalimbali ikiuzwa kwa wingi sana.
Nilipojaribu kuichunguza kwa makini nilipata walakini kama inaweza kuhifadhi mboga kwa usalama na isiwe na matokeo mabaya kwa mbebaji. Niliona pia kutakuwa kuna tatizo kwa wale wanapima unga wa kula kwa kilo, sioni kama mifuko ile ni rafiki kwa kuhifadhi ili utoke nao dukani hadi nyumbani (mliofanikiwa kuiona nadhani mlijiuliza swali hilo pia) lakini nikajiuliza wamama wanaobeba mchele toka sokoni hadi nyumbani pia kutakuwa kuna hitilafu kidogo kwenye chakula chao.

Mifuko ile ni ya nyuzinyuzi na sio karatasi (japo sijui kama imethibitiswa au ni watu wanatumia fursa).

Kwa haraka haraka nimeona ile inafaa kubebea nguo ukitoka dukani ila si mboga ama chakula cha kupima.(mliotumia nisahihisheni kama nipo tofauti).


Hili swala lisichuliwe kirahisi, linahitaji umakini sana kuendelea kulinda afya za watu na mazingira kiujumla.

Tusijekuwa tunamwita Dulla badala ya Abdalah.
Kwa wale tunaosafiri barabara Dar to mikoa ya Lindi na Mtwara tutakuwa mashahid pale Nangurukuru kuna bahasha tunauziwa kuwekea samak tunaonunua pale hotelin nadhani zile bahasha ni nzur zaid na salama maana ni ngumu na imara sana,sijajua zinatengenezewa wapi,nikipita sik za hiv karibun nitawauliza wale vijana.
 
Kwa wale tunaosafiri barabara Dar to mikoa ya Lindi na Mtwara tutakuwa mashahid pale Nangurukuru kuna bahasha tunauziwa kuwekea samak tunaonunua pale hotelin nadhani zile bahasha ni nzur zaid na salama maana ni ngumu na imara sana,sijajua zinatengenezewa wapi,nikipita sik za hiv karibun nitawauliza wale vijana.
Yah kweli pale kuna bahasha nzuri sana na imara na unazipata kuanzia hotelini hadi kule chini kwa wanauouza samaki na pia kule mzani. Pale waliwahi kustarabika naona
 
Back
Top Bottom