SWALI: Mkoa gani Tanzania ni mzuri kwa kuishi?

Mandla Jr.

JF-Expert Member
Dec 15, 2013
3,099
630
Wadau wa JF!
Ningependa kupata mawazo yenu, ni Mkoa gani ni mzuri wa kuishi hapa kwetu au ni Wilaya gani ni nzuri kwa kuishi??

Naomba tujadiliane.
 
Ukweli mie naona mkao mzuri kuishi ni morogoro!! Kwanza sio mbali na dar ambako Ndio Tz ilipo pili Hali ya hewa si ya joto Kama dar, bei ya chakula sio ghali Sana na ardhi unaweza kununua kwa bei poa pia!! Sijazaliwa hapo wala kusoma ila nimefanya upembuzi yakinifu! Moro ze best
 
Dar still the best.....hakuna kulaza akili. Ukilaza tu akili kidogo inakula kwako mazima. No hustling no food! Unaweza kufa huku watu wanakutazama tu, hawana time na wewe. Kila mtu yupo na stress za maisha yake. Anawaza vipi atapiga dili liwe la wizi ama la kawaida. Dar the best. Unakuwa challenged kila leo!
 
Mkoa wa dodoma
wilaya ya dodoma mjini
kata ya mnadani
eneo la maili mbili

JIJI LA KITOVU CHA ELIMU TANZANIA

KUNA
1. CHUO CHA UDOM
2. ST.JOHN
3. CHUO MIPANGO
4. CBE
5. CHUO CHA MADINI
6. ASSEKI CHUO CHA BIASHARA
7. VETA KANDA YA KATI
9. CAPITAL CHUO CHA UALIMU
10. CHUO CHA MAFUNZO YA KIJESHI MAKUTUPORA

KUNA
¡ú BUNGE
¡ú KIWANDA CHA NYAMA CHA TAIFA TMC

KUNA
CHAKO NI CHAKO
MNADA MSALATO
MASTER PUB

LOL
KARIBU DODOMA
HOME OF THE BRAVE
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom