Kapyepye Mfyambuzi
JF-Expert Member
- Jun 18, 2020
- 542
- 918
Kweli kabisa mkuu ✓ 100%Hyo inaitwa "dejavu" ni neno la kifaransa linamaanisha "pre existed" yaan sisi binadamu kabla ya maisha haya, tushawahi ishi kabla. Kilichofanyika ni kitendo cha kupewa miili mipya tu lakn nafsi zetu zilikuepogo kabla ya sisi kuwa na hii miili"
Watu wengi hawalijui hilo, dini zetu zimetuaminisha tofauti sana. Ndio maana mtu akifa tunamlilia, na wakati kilichofanyika ni nafsi/ roho tu ndio imerudi kwenye u-milele wake na baadae itarudi tena duniani ikipata (fresh body) mwili mpya (Yaani utazaliwa tena upya kama mtoto mchanga na haijalishi ni taifa gani au nchi gani na ni wazazi gani), sema ufahamu na kumbukumbu zitakuwa zimefungwa na Ego isipokuwa tu kwa wanaofanya meditation mpaka kufikia Enlightenment (spiritutal awakening) ndio huwa wanakumbuka experience ya maisha yao ya zamani waliyowahi kuyaishi.
Jamani meditation ni kitu kizuri sana,, sana,, sana tu yaani,, hasa ukiwa na juhudi ya kufanya mpaka ukafikia mwangaza wa kiroho, mtayajua mengi bila kufundishwa na mtu, utayaona maisha ni rahisi sana maana hauta tegemea vitu tena ili uwe na furaha na amani bali furaha unayo ndani mwako muda wote.
Ndio maana kwa wanaojitambua huwa wanasema, siku nikifa msinililie bali sherehekeeni maisha yangu niliyoishi duniani.