Swali la umakini; Baada ya African Barrick Gold kubadili jina kuwa ACACIA Gold, usajili ulikufa?

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Ninaiheshimu sana kamati ya pili ya Magufuli kuhusu suala la makanikia, na mapendekezo waliyotoa.

Hata hivyo, nimesikia Kamati ya Magufuli wakisema Acasia haipo nchini kisheria, kwamba haijawahi kusajiriwa kama kampuni inayofanya biashara nchini Tanzania. Nina swali ambalo linalenga kupima umakini wa wasomi wetu katika kuchambua mambo. Lengo sio kukosoa kamati, lengo ni kuangalia umakini wetu katika kuchambua mambo.

Nakumbuka kwamba Acasia ni matokeo ya kubadili jina toka African Barrick Gold kuwa Acasia Gold. Sasa, hivi kutosajiriwa kwa Acasia ndio kosa lao au kosa ni kwamba African Barrick Gold walipobadili jina kuwa Acasia Gold hawakutoa taarifa kwa Msajiri wa Makampuni Tanzania? Hivi nikiwa na kampuni nikaibadili jina, nahitaji kufanya usajiri mpya kwa kutumia jina jipya la kampuni?

Je, ilibidi African Barrick Gold wafute usajiri wa mwanzo walipobadili jina, au watoe tu taarifa? Na kama ni usajiri mpya, haitamaanisha lesseni itabidi zitolewe upya? Kama Acasia haipo nchini kisheria, bado tunaitambua African Barrick Gold kuwa mmiliki wa hii migodi?

Wasiwasi wangu ni kwamba, pamoja na udanganyifu na dhambi zote za Acasia, kama kamati hii haijaliwakilisha suala la uwepo wa Acasia nchini inavyotakiwa, kuwa ni suala la kutokuwapo kwa taarifa kwamba African Barrick Gold imebadilisha jina, basi ukweli ni kwamba Tanzania tuna tatizo kubwa sana la wataalamu wetu kutokuwa makini katika mambo mengi, na jambo la kutisha na kisababshi kikubwa kuwa hata wale tunaowaamini wanashindwa kuona mapungufu katika mikataba ya kitaifa kwa kuwa hawako makini, vigilant, katika kutathmini (assess and review) mambo.
 
Toka huo muda walipobadilisha jina kodi walikuwa hawalipi? Kama walikuwa wanalipa walikuwa wanalipa kwa jina gani, na kama walikuwa hawalipi wahusika walikuwa wapi?
Hivi vitu vinaumiza sana hawa viongozi na wote waliokuwa kwenye mamlaka ya kusaini mikataba, kutoa leseni na kukusanya kodi watuambie tu.
 
Toka huo muda walipobadilisha jina kodi walikuwa hawalipi? Kama walikuwa wanalipa walikuwa wanalipa kwa jina gani, na kama walikuwa hawalipi wahusika walikuwa wapi?
Hivi vitu vinaumiza sana hawa viongozi na wote waliokuwa kwenye mamlaka ya kusaini mikataba, kutoa leseni na kukusanya kodi watuambie tu.

Kweli Mkuu. Ndio maana kuna zaidi ya Acasia inabidi wawajibike kwa hili. Nadhani hata watu wa TRA wanapaswa kuigizwa katika hili. Wanatusumbua pale airport na kukagua begi zetu na kudai ushuru tunapowasili toka nchi za nje wakati wanaacha mabilioni ya kujenga SGR yanaibiwa
 
Ninaiheshimu sana kamati ya pili ya Magufuli kuhusu suala la makanikia, na mapendekezo waliyotoa.

Hata hivyo, nimesikia Kamati ya Magufuli wakisema Acasia haipo nchini kisheria, kwamba haijawahi kusajiriwa kama kampuni inayofanya biashara nchini Tanzania. Nina swali ambalo linalenga kupima umakini wa wasomi wetu katika kuchambua mambo. Lengo sio kukosoa kamati, lengo ni kuangalia umakini wetu katika kuchambua mambo.

Nakumbuka kwamba Acasia ni matokeo ya kubadili jina toka African Barrick Gold kuwa Acasia Gold. Sasa, hivi kutosajiriwa kwa Acasia ndio kosa lao au kosa ni kwamba African Barrick Gold walipobadili jina kuwa Acasia Gold hawakutoa taarifa kwa Msajiri wa Makampuni Tanzania? Hivi nikiwa na kampuni nikaibadili jina, nahitaji kufanya usajiri mpya kwa kutumia jina jipya la kampuni?

Je, ilibidi African Barrick Gold wafute usajiri wa mwanzo walipobadili jina, au watoe tu taarifa? Na kama ni usajiri mpya, haitamaanisha lesseni itabidi zitolewe upya? Kama Acasia haipo nchini kisheria, bado tunaitambua African Barrick Gold kuwa mmiliki wa hii migodi?

Wasiwasi wangu ni kwamba, pamoja na udanganyifu na dhambi zote za Acasia, kama kamati hii haijaliwakilisha suala la uwepo wa Acasia nchini inavyotakiwa, kuwa ni suala la kutokuwapo kwa taarifa kwamba African Barrick Gold imebadilisha jina, basi ukweli ni kwamba Tanzania tuna tatizo kubwa sana la wataalamu wetu kutokuwa makini katika mambo mengi, na jambo la kutisha na kisababshi kikubwa kuwa hata wale tunaowaamini wanashindwa kuona mapungufu katika mikataba ya kitaifa kwa kuwa hawako makini, vigilant, katika kutathmini (assess and review) mambo.


Mkuu jaribu kutafuta Companies Act 2002 na Companies Ordinance.Utaratibu wa kubadili jina umeelezwa vizuri.Na Brela wanazo instruments za ku-accomodate hayo mabadiliko.Hata Board ya Wakurugenzi wakiazimia kubadili lakini mabadiliko hayo yasifanyike BRELA mabadilko hayo yanakuwa Null and Void.

Na jambo lolote litakalofanywa chini ya jina jipya ambalo halijatambuliwa kisheria linakuwa halitambuliki kisheria.Na ndicho inachokisema Kamati.

Na cheti cha kuonyesha jina jipya huambata na jina la Zamani.Na ukishabadilisha jina vitu vyote ulivyokuwa ukifanya kwa jina la zamani lazima sasa visomeke kwa jina jipya.Sio tu jina hadi anuani ya Biashara ikibadilika lazima Msajili ajulishwe.Uki-ignore siku ukikamatwa utachukuliwa wewe ni trespasser na mzuraraji tu.

Jambo la kujiuliza ni kwa nini ABG waliamua ku-ignore kitu muhimu kama hiki? Ilikuwaje walikuwa wanakumbuka kuweka seal kwenye makontena ya Makanikia wakasahau kuweka seal muhimu kama hii ya kisheria?Wakati utatuambia

Lakini zaidi ya yote,Wahenga walituhusia: Sungura pamoja na ujanja wake wote alionao alinaswa kwenye gundi tu.ABG (calling themselves ACACIA) wana mitaji mikubwa.Wana Wataalamu wabobezi katika nyanja mbalimbali lakini wamenaswa kwa Ulimbo tu.Wao walitunasa kwa kupitia kwa akina Team Chenge kwa pesa lakini wao wamenaswa kwa Ulimbo wa jjna.
 
Haya mambo inabidi tuhusishe na waganga mkuu maana tunao wengi wanaweza hata badili maandishi ya mikataba feki tuliyoingizwa chaka
 
Mkuu jaribu kutafuta Companies Act 2002 na Companies Ordinance.Utaratibu wa kubadili jina umeelezwa vizuri.Na Brela wanazo instruments za ku-accomodate hayo mabadiliko.Hata Board ya Wakurugenzi wakiazimia kubadili lakini mabadiliko hayo yasifanyike BRELA mabadilko hayo yanakuwa Null and Void.Na jambo lolote litakalofanywa chini ya jina jipya ambalo halijatambuliwa kisheria linakuwa halitambuliki kisheria.Na ndicho inachokisema Kamati.Na cheti cha kuonyesha jina jipya huambata na jina la Zamani.Na ukishabadilisha jina vitu vyote ulivyokuwa ukifanya kwa jina la zamani lazima sasa visomeke kwa jina jipya.Sio tu jina hadi anuani ya Biashara ikibadilika lazima Msajili ajulishwe.Uki-ignore siku ukikamatwa utachukuliwa wewe ni trespaser na mzuraraji tu.

Jambo la kujiuliza ni kwa nini ABG waliamua ku-ignore kitu muhimu kama hiki? Ilikuwaje walikuwa wanakumbuka kuweka seal kwenye makontena ya Makanikia wakasahau kuweka seal muhimu kama hii ya kisheria?Wakati utatuambia

Lakini zaidi ya yote,Wahenga walituhusia: Sungura pamoja na ujanja wake wote alionao alinaswa kwenye gundi tu.ABG (calling themselves ACACIA) wana mitaji mikubwa.Wana Wataalamu wabobezi katika nyanja mbalimbali lakini wamenaswa kwa Ulimbo tu.Wao walitunasa kwa kupitia kwa akina Team Chenge kwa pesa lakini wao wamenaswa kwa Ulimbo wa jjna.

Umenipa ufafanuzi mzuri sana Mkuu. Ndio maana nikasema ni kweli kabisa mambo mengi sana yanayotuathiri hapa nchini ni kwa sababu ya uzembe wetu wenyewe. Yaani Watanzania tuna shida sana ya kutokuwa serious katika kazi zetu, ili mradi tumenufaika kibinafsi. Uzalendo na m,aslahi ya nchi ni vitu ambavyo havipo kabisa kichwani, kwa hiyo hata tukionwa utaratibu unakiukwa wala hatujali.

Hili tu la kubadili jina kutoka ABG kuwa Acasia ukitafakari kwa makini, watu wengi sana wanatakiwa kutumbuliwa!
 
Umenipa ufafanuzi mzuri sana Mkuu. Ndio maana nikasema ni kweli kabisa mambo mengi sana yanayotuathiri hapa nchini ni kwa sababu ya uzembe wetu wenyewe. Yaani Watanzania tuna shida sana ya kutokuwa serious katika kazi zetu, ili mradi tumenufaika kibinafsi. Uzalendo na m,aslahi ya nchi ni vitu ambavyo havipo kabisa kichwani, kwa hiyo hata tukionwa utaratibu unakiukwa wala hatujali.

Hili tu la kubadili jina kutoka ABG kuwa Acasia ukitafakari kwa makini, watu wengi sana wanatakiwa kutumbuliwa!


Mkuu hii ndo unasikia inaitwa "A blessing in disguise".Kufa kufaana.Ni kosa lenye heri Wakatoliki wanasema hivyo.Watu walizembea na sasa imekuwa ndio tool ya kuokokea.Nakuambia hili la jina pekee ni nyundo ya kuwabinyia *ACACIA" korodani.Hawafurukuti.Lazima wakae chini tu.Umesoma statement yao baada ya Kamati kuwasilisha Report yao? Isome utaelewa jinsi walivyobanwa korodani na maumivu wanayoyasikia.
 
Mkuu hii ndo unasikia inaitwa "A blessing in disguise".Kufa kufaana.Ni kosa lenye heri Wakatoliki wanasema hivyo.Watu walizembea na sasa imekuwa ndio tool ya kuokokea.Nakuambia hili la jina pekee ni nyundo ya kuwabinyia *ACACIA" korodani.Hawafurukuti.Lazima wakae chini tu.Umesoma statement yao baada ya Kamati kuwasilisha Report yao? Isome utaelewa jinsi walivyobanwa korodani na maumivu wanayoyasikia.

Naanza kuona mwanga mwisho wa tunnel, and thanks to Magufuli.

Nadhani wengi wamesema sana kuwa ni heri hili lingetokea miaka ya nyuma tungefaidika sana. NI kweli - ni kama tumekumbuka shuka wakati kumekucha. Hata hivyo, hili linatoa precedent nzuri sana kwa kampuni nyingine zitakazokuja nchi baadae kujua kuwa Tanzania sio shamba la bibi.

Na hili la kuwashitaki maraisi na viongozi waliopita ni muhimu sana, hasa kwa kuwa Magufuli tunaye kwa miak 10 tu. Tukimuwajibisha Mkapa kwa hili la Bulyankulu na mengine kama Kiwira, basi tutaweka precedent na raisi atakekuja baada ya Magufuli atajua asipokuwa makini yatampata yaliyowapata maraisi waliopita, ikiwa watawajibishwa. Tukiacha kina Mkapa wanusurike na hili, basi baada ya Magufuli tunaweza kuwa na Raisi akaturudisha kule kule kwenye mikataba mibovu na maagizo kwa mawaziri wupunguze hisa za Tanzania kwa kuwa tumepewa zawadi ya hoteli ya kifahari kule Johannesburg, South Africa!
 
Mkuu hii ndo unasikia inaitwa "A blessing in disguise".Kufa kufaana.Ni kosa lenye heri Wakatoliki wanasema hivyo.Watu walizembea na sasa imekuwa ndio tool ya kuokokea.Nakuambia hili la jina pekee ni nyundo ya kuwabinyia *ACACIA" korodani.Hawafurukuti.Lazima wakae chini tu.Umesoma statement yao baada ya Kamati kuwasilisha Report yao? Isome utaelewa jinsi walivyobanwa korodani na maumivu wanayoyasikia.

Mkuu nimeiona hii kwenye thread nyingine. Angalia hapa chini. Kumbe sisi ndio wazembe. Kuna kamchezo kamefanyika. Angalia hizo tarehe.

upload_2017-6-13_14-25-39.png
upload_2017-6-13_14-26-28.png
 
Back
Top Bottom