Swali la Ukorofi: Vigogo wa CHADEMA Wanaomuuza Lowassa Wakianguka Bunge Iweje?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
1.png

Baadhi ya viongozi wakuu wa CDM (wengi wajumbe wa Kamati Kuu) wanagombea Ubunge sehemu mbalimbali nchini. Baadhi ya hawa ndio wamekuwa waimbaji wakubwa wa sifa za Lowassa kama mgombea wao na wameamua kuweka heshima na hatima yao na ushindi wa Lowassa. Hili limenifanya nijiuliza maswali yafuatayo hasa kama wakianguka - kama wakishinda sidhani kama itakuwa shida mambo mengine. Ngoma itakuwa kwenye kama wakishindwa.

Lowassa Akishinda: Kama Lowassa akishinda (kinadharia tu japo haitotokea) na viongozi hawa wa CDM wakakataliwa majimboni mwao, Lowassa awakumbuka nafasi mbalimbali au aheshimu maamuzi ya watu na kuwaacha wajifikirie wenyewe? Au afanye kama marais wa CCM ambao mtu hata akikataliwa na wananchi anapewa nafasi nyingine ambazo zinaitwa za "ulaji"?

Lowassa akishindwa: Na wao wakashindwa, waendelee kuongoza chama hasa kama Lowassa ataamua baada ya kushinda kujiuzulu siasa au hata kuamua kurudi CCM (hata kimya kimya)?

Maswali haya ni muhimu kwa sababu zipo dalili za baadhi ya viongozi maarufu kujikuta wanakataliwa na wao majimboni na tusije kushangaa baadhi ya majina maarufu hayarudi Bungeni hasa kwa sababu wapo wanachama ambao kutokana na hili la Lowassa na dubwasha la UKAWA wataona kuwa viongozi wao wamewaingiza mjini na kukivuruga chama bila sababu ya msingi wakati ushindi ulikuwa uko njiani.
 
Wasiwasi wako nini, muda wa kampeni haujakwisha, kama walitumikia vizuri wananchi watashinda tu.

CCMout, CCJ woyee.
 
Kwanini kushinda kwa Lowasa kuwe nadharia?!

Nani anachagua kiongozi!?
Kwa utaratibu gani?!

Kama ni kura na wananchi wakaamua kumpigia Lowasa kwa wingi haiwezi kuwa nadharia, labda kama kuna utaratibu mwingine utatumika kumpata kiongozi wa JMT
 
"Lowassa Akishinda: Kama Lowassa akishinda (kinadharia tu japo haitotokea)"
Hapa ndipo huwa natofautiana na Dr. Slaa pamoja na wewe, mengine mengi huwa nawasupport...
 
mm ningemshauri Mh. Lowassa kuwa hata kama anapenda kampeni za kistaarabu ajaribu mapigo cose anajua madudu mengi ya serikali zilizopita/na ya jk.hivyo ajue asipotibua baadhi ya mambo ukimya wake unatumika kama kete ya kummaliza/angalizo:hakuna mtu hapendi utajiri lakini wa lowassa imekuwa fimbo kwake.kuna watoto wa juzi ni mabilionea lkn wamefichwa nyuma ya pazia.tahadhari lowassa ukimya wako unatuangusha.
 
chagua rais lowassa

chagua mbunge wa ukawa

chagua diwani wa ukawa

kataa ulaghai wa ccm na vibaraka wake kama huyu mleta thread

ulofa mwisho october 25

chagua mabadiliko

wasipoyapata ndani ya ccm watayapata nje ya ccm - mwalimu nyerere

nguvu ya umma ndio itaamua na sio propaganda za vibaraka

peoples' power
Kama huna hoja ni vema ukakaa kimya ukabakia kuwa msomaji tu.

Huu ujinga wa kuchafua mada za watu ndio unaowafanya watu washindwe kuwatofautisha na Nyumbu.

Wewe unaonekana ndio kile kinyesi kilicholetwa Chumbani Matokeo yake Chumba kinanuka kuliko choo chenyewe.
 
Huyu mzee Mwanakijiji zamani alikuwa anaandika mambo mhimu na mazuri, ila siku hizi ameishiwa kabisa! Cjui ndio uzee unamnyemelea!

Ukweli ni kwamba hata km Lowassa asiposhinda Urais basi atakuwa amewekwa kwny historia mhimu sana ya kuibadili Tanzania toka mfumo dhalimu wa chama.kimoja chenye nguvuu na kuwa na upinzani wenye nguvu kubwa kabisa!

Nina uhakika mwaka huu waziri mkuu au spika wa bunge lazima atatoka chama pinzani...hii itakuwa ni mara ya kwanza kutokea tangu nchi ipate uhuru kwa mhimili wa dola kuongozwa na upinzani!
 
Lowasa Ni Mgombea wa CHADEMA.....Viongozi wa CHADEMA watamnadi mgombea wa CHADEMA

Lowasa amepitishwa na majority katika vikao vya chama.....Sasa wewe kama hujaridhika hustahili hata kuwaona wanaosimamia maamuzi ya vikao vya chama kama wanakose.......UBINAFSI....CHUKI...Ni dhambi

Matokeo yakitoka chama kitaendelea kama kawaida.....Aidha kimeshinda au kimesindwa.....CHAMA HIKI SIO CHA SLAA NI CHA WANANCHI
 
Huyu mzee Mwanakijiji zamani alikuwa anaandika mambo mhimu na mazuri, ila siku hizi ameishiwa kabisa! Cjui ndio uzee unamnyemelea!

Ukweli ni kwamba hata km Lowassa asiposhinda Urais basi atakuwa amewekwa kwny historia mhimu sana ya kuibadili Tanzania toka mfumo dhalimu wa chama.kimoja chenye nguvuu na kuwa na upinzani wenye nguvu kubwa kabisa!

Nina uhakika mwaka huu waziri mkuu au spika wa bunge lazima atatoka chama pinzani...hii itakuwa ni mara ya kwanza kutokea tangu nchi ipate uhuru kwa mhimili wa dola kuongozwa na upinzani!

Mbona swali ni rahisi tu; kuna mambo yanahitaji tafakari kabla hayajatokea, yatakapotokea watu wawe angalau wamefikiria nini cha kufanya. Sasa wewe unaonaje? hufikirii kuna vigogo wa CDM wanaweza kupoteza viti vyao vya ubunge ambavyo vinagombaniwa sasa?
 
Nilishasema tanzania ina type ya watu kama huyu mwanakijiji, slaa ni wazee ambao wanazungumza mabadiliko ambayo hayaamini, ni watu ambao hawawezi kutake risk,ni watu ambao wanafunction mazingira yakiwa mazuri tu, ilaikitokea challange kidogo ni watu wa kukata tamaa kwenye maisha japo unaweza usijue ukiangalia juju, ni watu ambao kwa nje wanaonesha ccm inatakiwa iondoke madarakani lakini kwa ndani hawamini hilo wamejaa uoga .Ni COWARDS
ukisoma uzi kama huu kwa umakini unaona UNAFKI na UOGA wa hali ya juu, unaona mtu anayejidai KUUMA na KUPULIZA. Na kutoa viangalizo vya kinafki ili baadae aje kusema nlisema.
watu wa aina hii wamezorotesha taifa la tanzania sana, wamezalisha watoto ambao wamekuwa ni kizazi cha watu waoga WALIOKOSA uthubutu, hata wa kusakanya maisha.
Embu soma huo uzi hapo juu ulivyojaa UNAFKI na WOGA it's COWARDNESS. Ni hasara.
 
Mbona swali ni rahisi tu; kuna mambo yanahitaji tafakari kabla hayajatokea, yatakapotokea watu wawe angalau wamefikiria nini cha kufanya. Sasa wewe unaonaje? hufikirii kuna vigogo wa CDM wanaweza kupoteza viti vyao vya ubunge ambavyo vinagombaniwa sasa?

Unaposhindana huwa kuna mambo mawili tu unayotegemea, either winning or lose....ukishinda basi lengo linatimia, ukipoteza then lazima uwe na plan B!

Walau ungezungumzia vyama ndanj ya UKAWA vilivyomezwa na CHADEMA ningekuelewa mjadala ungekuwa hot zaidi!
 
Kinadhari tu japo....? Hakika na wewe nilikuwa nadhani una uwezo wa kufikiri kumbe bora hata polepole! Mtanunuliwa sana lakini wananchi wamekwisha kuamua.
 
Sipati picha mtu kama Mch.Msigwa akianguka itakuaje.

Kwanza alisema mtu atakaempigia kura Lowassa akapimwe akili.

Siku chache baadae akageuka na kuanza kumsifia na kumsafisha mbele ya camera za TV bila aibu.

Tena akaongeza kuwa "Watanzania hawana uelewa kuhusu ufisadi hivyo hoja ya ufisadi haina mashiko" Sasa mtu kama huyu akipigwa chini lazima tumsahau kwenye jukwaa la siasa.
 
Tuanze na Ukawa ni nini? Hawa viongozi waliobaki Chadema hawajielewi. Leo kuna ilani ya Ukawa hakuna ilani ya Chadema.
Sasa majibu kwa maswali yako ni kuwa
1. Lowassa atawakumbuka akina Chenge na Serukamba kabla ya akina Mbatia na Mbowe.
2. Viongozi wa CDM wajiuzulu au wabaki haijalishi kwa sababu Chadema imefikia expiration date yake.
Na kwa kumalizia mpango wa Lowassa ni kwenda kupumzika London baada ya uchaguzi na ni 100% atashindwa na ameshalitambua hilo. Rostam baada ya kujaribu kumjibu Dr Slaa kaamua kutimuka zake na wafadhili wengine wa Lowassa wamempotezea hata wanafamilia hawajitolei mabasi na misaada midogomidogo. Reality is setting in.
Sasa last attempt yao ni kujaribu kuchangisha kwa jina la Ukawa (sijui ni nini) na Chadema. Na wale watakaonaswa na hawamjui Lowassa watachangia. Ila ndiyo ujue they are scrapping the bottom of the barrel now. This is like a pyramid scheme, the latecomers who are the majority get screwed.
 
mm ningemshauri Mh. Lowassa kuwa hata kama anapenda kampeni za kistaarabu ajaribu mapigo cose anajua madudu mengi ya serikali zilizopita/na ya jk.hivyo ajue asipotibua baadhi ya mambo ukimya wake unatumika kama kete ya kummaliza/angalizo:hakuna mtu hapendi utajiri lakini wa lowassa imekuwa fimbo kwake.kuna watoto wa juzi ni mabilionea lkn wamefichwa nyuma ya pazia.tahadhari lowassa ukimya wako unatuangusha.

Huyu Lowassa hafanyi kampeni ya kistaarabu kwa kupenda. Ni lazima maana akianza tu kitakachofuata kitakuwa chungu sana kwake. Ana madudu mengi tokea miaka ya 1990.
Pili ana mpango wa kuishi London na anataka vizazi vyake visinyang'anywe mali walizopora so he is playing it safe.
Ukimya wake ni wa maksudi. It is not by coincidence but by design.
 
1.png

Baadhi ya viongozi wakuu wa CDM (wengi wajumbe wa Kamati Kuu) wanagombea Ubunge sehemu mbalimbali nchini. Baadhi ya hawa ndio wamekuwa waimbaji wakubwa wa sifa za Lowassa kama mgombea wao na wameamua kuweka heshima na hatima yao na ushindi wa Lowassa. Hili limenifanya nijiuliza maswali yafuatayo hasa kama wakianguka - kama wakishinda sidhani kama itakuwa shida mambo mengine. Ngoma itakuwa kwenye kama wakishindwa.

Lowassa Akishinda: Kama Lowassa akishinda (kinadharia tu japo haitotokea) na viongozi hawa wa CDM wakakataliwa majimboni mwao, Lowassa awakumbuka nafasi mbalimbali au aheshimu maamuzi ya watu na kuwaacha wajifikirie wenyewe? Au afanye kama marais wa CCM ambao mtu hata akikataliwa na wananchi anapewa nafasi nyingine ambazo zinaitwa za "ulaji"?

Lowassa akishindwa: Na wao wakashindwa, waendelee kuongoza chama hasa kama Lowassa ataamua baada ya kushinda kujiuzulu siasa au hata kuamua kurudi CCM (hata kimya kimya)?

Maswali haya ni muhimu kwa sababu zipo dalili za baadhi ya viongozi maarufu kujikuta wanakataliwa na wao majimboni na tusije kushangaa baadhi ya majina maarufu hayarudi Bungeni hasa kwa sababu wapo wanachama ambao kutokana na hili la Lowassa na dubwasha la UKAWA wataona kuwa viongozi wao wamewaingiza mjini na kukivuruga chama bila sababu ya msingi wakati ushindi ulikuwa uko njiani.

Ati huyu nfio mshauri wa padre mzinzi monsinyori Slaa.

Mambo ya UKAWA tuachie wenyewe, ninachokuahidi leo ndanivya kipindi hiki nitakutaja jina lako halisi nitatoa picha zako halisi hili upigane vita hii kiuhalisia.

Hakuna mwanajeshi mwoga wewe ni coward ndio maana sehemu zote umejificha utambulisho wako, lakini finaly i got you na nitakusambaza.
 
Back
Top Bottom