Swali la Ugomvi kwa Watangaza Nia: Mafanikio Yote Mliyotuhubiria Leo Yamepeperuka?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Swali la Ugomvi: Miaka hii tisa wametuhubiria sana "mafanikio" yao, wametuonesha vyuo, barabara, mahospitali n.k ambavyo wamevifanya na wanajivunia. Ghafla kila mmoja anayetaka kugombea anasema "mabadiliko"; oo "ntabadilisha x,y". Najiuliza mbona hawasimamii 'maendeleo' yao wenyewe kila mmoja ni kama anayaruka?

Mara kadhaa tumewasikia wakitamba Bungeni "Serikali sikivu ya CCM imefanya a, b, c, na d" na tena kwa kejeli wengine walidai "hawa wapenzi hawayaoni?". Sasa leo, watangaza nia wetu ambao wengi ni mawaziri, manaibu au wabunge wote wanajaribu kutuaminisha kuwa nchi inaelekea kubaya kiasi kwamba inahitaji "mabadiliko". Kulikoni wenzetu? Yale mafanikio yamepeperuka au yalikuwa yakuzuga au sasa na nyie mmeamua kudandia treni la "mabadiliko"?

Obama alipotangaza "Change" alikuwa anamaanisha mabadiliko hasa kutoka chama na utawala wa Rais George Bush. Alikuwa analipeleka Taifa lake upande mwingine - kwa uzuri au kwa ubaya. Wananchi walioamuamini na kumpigia kura walifanya hivyo kwa sababu waliamini katika "mabadiliko". Sasa hawa wenzetu, chama chao, serikali yao na asilimia 99 wamewahi kutumikia serikali hiyo hiyo kwa nyadhifa mbalimbali; sasa iweje leo watuambie na kutuimbia "mabadiliko" na baadhi yetu kama tuliolishwa limbwata la kisiasa tunashabikia kweli kutakuwa na "mabadiliko".

Unaweza vipi kubadilisha kitu ambacho hakijabadilika isipokuwa kukibadilisha bila kukibadilisha; kama kubadilisha duara?


Picha hii haiko sawa. Nini tatizo?
 
Kwanini wasiruke kauli zao ikiwa aliyesema maisha bora kwa kila mtanzania, juzi kasema , anasikitika anaondoka na kuacha wakulima masikini! Hata yeye anaruka kauli ya maisha bora kwa kila mtanzania

Tena si kuruka kauli zao, wameenda mbali na ‘kuinyanyapaa'serikali yao.
Leo wanasema watapambana na rushwa na ufisadi uliokithiri!


Nahodha akitosa jahazi, waliobaki wafanye nini?
 
Kwanini wasiruke kauli zao ikiwa aliyesema maisha bora kwa kila mtanzania, juzi kasema , anasikitika anaondoka na kuacha wakulima masikini! Hata yeye anaruka kauli ya maisha bora kwa kila mtanzania

Tena si kuruka kauli zao, wameenda mbali na ‘kuinyanyapaa'serikali yao.
Leo wanasema watapambana na rushwa na ufisadi uliokithiri!


Nahodha akitosa jahazi, waliobaki wafanye nini?

Yaani, hawa siyo tu wanalitosa jahazi yaani wao wenyewe wamelitoboa matundu wakiwa ndani halafu leo wanatoka nje kusema "linazama linazama"!!
 
Watia NIA wa ccm wote walikuwa wajumbe wa BMK kupitia ccm na waliipondaponda rasimu ya Jaji Warioba na kutuletea what they call Katiba Pendekezwa!
Je ahadi hizi zinatekelezeka kwenye Katiba Pendekezwa ama Rasumu ya Warioba?
Ama wataendesha kwa katiba binafsi za mfukoni? Yaani watakuiuka utawala wa sheria mama(Katiba)?
[MENTION=126812][/MENTION]
 
Cha kushangaza ni kwamba, watangaza nia wetu, hata wale wenye tuhuma rushwa, leo hii, bila hata kusafishwa na chombo chochote kile (takukuru au mahakama) nao wanasimama majukwaani wakihubiri kuichukia rushwa huku wakiwalipa posho wale wadanganyika wanaokwenda kuwasikiliza kwa kukubali kwao kuwasikiliza. "Asante kwa kunisikiliza!" Tukiwapeleka hawa magogoni tutajuta kuliko majuto tunayojutia sasa kutokana na sanaa za msanii wa 'maisha bora kwa kila mdanganyika'. Anasikitika kuwaacha wakulima bado maskini huku anatabasamu?
 
Swali la Ugomvi: Miaka hii tisa wametuhubiria sana "mafanikio" yao, wametuonesha vyuo, barabara, mahospitali n.k ambavyo wamevifanya na wanajivunia. Ghafla kila mmoja anayetaka kugombea anasema "mabadiliko"; oo "ntabadilisha x,y". Najiuliza mbona hawasimamii 'maendeleo' yao wenyewe kila mmoja ni kama anayaruka?

Mara kadhaa tumewasikia wakitamba Bungeni "Serikali sikivu ya CCM imefanya a, b, c, na d" na tena kwa kejeli wengine walidai "hawa wapenzi hawayaoni?". Sasa leo, watangaza nia wetu ambao wengi ni mawaziri, manaibu au wabunge wote wanajaribu kutuaminisha kuwa nchi inaelekea kubaya kiasi kwamba inahitaji "mabadiliko". Kulikoni wenzetu? Yale mafanikio yamepeperuka au yalikuwa yakuzuga au sasa na nyie mmeamua kudandia treni la "mabadiliko"?

Obama alipotangaza "Change" alikuwa anamaanisha mabadiliko hasa kutoka chama na utawala wa Rais George Bush. Alikuwa analipeleka Taifa lake upande mwingine - kwa uzuri au kwa ubaya. Wananchi walioamuamini na kumpigia kura walifanya hivyo kwa sababu waliamini katika "mabadiliko". Sasa hawa wenzetu, chama chao, serikali yao na asilimia 99 wamewahi kutumikia serikali hiyo hiyo kwa nyadhifa mbalimbali; sasa iweje leo watuambie na kutuimbia "mabadiliko" na baadhi yetu kama tuliolishwa limbwata la kisiasa tunashabikia kweli kutakuwa na "mabadiliko".

Unaweza vipi kubadilisha kitu ambacho hakijabadilika isipokuwa kukibadilisha bila kukibadilisha; kama kubadilisha duara?


Picha hii haiko sawa. Nini tatizo?
Kwanini hukutumia mfano wa republican candidates ambao walikuwa kwenye serikali ya Bush kama vile McCain?
 
Kwanini hukutumia mfano wa republican candidates ambao walikuwa kwenye serikali ya Bush kama vile McCain?


Ambao walikuwa wanahubiri "mabadiliko" kutoka mwelekeo wa utawala wa Bush? Unafikiri kwanini McCain alishindwa? si hakutaka kujihusisha na Bush na "mafanikio" yake? Sasa upande mmoja McCain mwingine Obama unafikiri wananchi waliona ni nani kweli anamaanisha "Mabadiliko" of course not McCain. Hoja yangu basi kwa CCM inasimama. Sivyo?
 
Uchaguzi umefika na ni kipindi kingine cha wanasiasa kujiweka karibu kwa wananchi...yaani huu ni muda wa kusherehekea pamoja,kuzika pamoja,kucheza pamoja,kufikiri na kutafakari pamoja,kulia na kuimba pamoja.

Ni muda wa wanasiasa kuwa wananchi!

Tatizo ni wananchi ambao hutoa wanasiasa kwa hiyo usishangazwe sana mzee mwanakijiji.
 
we naye badala ujibu swali la mwana kijiji VIP safari ya maisha bora kwa kila mtanzania na hizi tambo za watangaza nia IPI nzuri?

Naona tatizo kwako ni lugha, soma tena:

quote_icon.png
By FaizaFoxy
Hilo swali la uchokozi au swali la kipunguani?

There is always space for improvement. No matter how long you've been in the business - Oscar De La Hoya.
 
Ambao walikuwa wanahubiri "mabadiliko" kutoka mwelekeo wa utawala wa Bush? Unafikiri kwanini McCain alishindwa? si hakutaka kujihusisha na Bush na "mafanikio" yake? Sasa upande mmoja McCain mwingine Obama unafikiri wananchi waliona ni nani kweli anamaanisha "Mabadiliko" of course not McCain. Hoja yangu basi kwa CCM inasimama. Sivyo?
Kama ni kwenye mpira wa kikapu, hapo umeteremsha goli mpaka kwenye sakafu.

Kama angetaka kujihusisha na mafanikio yake, angepata urais?
Kwenye politics kuna kitu kinaitwa "Collecive action dilemma" na " Window of opportunity for Change" (multiple stream model proposed by John Kingdon). Ndipo Obama alipowapiga bao.

It's not just about change, he was selling hope!
 
Mafanikio yote ya serekali waliokuwa wana yaeleza na kuyatetea yalikuwa ni kanya boya na sasa wako kuandaa kanyaboya lingine ili wawaingize mkinge wananchi.
 
Kama ni kwenye mpira wa kikapu, hapo umeteremsha goli mpaka kwenye sakafu.

Kama angetaka kujihusisha na mafanikio yake, angepata urais?
Kwenye politics kuna kitu kinaitwa "Collecive action dilemma" na " Window of opportunity for Change" (multiple stream model proposed by John Kingdon). Ndipo Obama alipowapiga bao.

It's not just about change, he was selling hope!

Well... hope inatoka wapi? si kwa watu waliokata tamaa? na hapa si ndiyo "mabadiliko" yenyewe? au hope comes for those who not in despair? Unafikiri hawa wanaohubiri"change" leo wanahubiri "hope"? kwamba sasa wao wanaleta matumaini? kutoka kwenye kitu gani "mafanikio"?
 
wanaendeleza madharau yaleyale kwa watanzania wakifikiri watanzania bado wamelala,wanasahau tulisha fungua macho na tunajua kutofautisha nuru na giza,Lowassa na mafisadi wenzake wamekaa serikalini zaidi ya miaka 40 walishindwa kufanya hayo mabadiliko wanayotaka kuyafanya miaka mitano?
 
Ninashangaa na nitazidi kushangaa, eti serikali inaelekea kubaya, mara wataboresha hiki mara kile. Wote wanaosema haya wamekuwemo serikalini kwa kipindi kirefu, tena kwenye nafasi kubwa kabisa. Asilimia kubwa walishiriki vikao vya baraza la mawaziri kwa miaka nenda rudi. Walishindwa vipi kuleta hayo mabadiliko?

Very low!
 
Naona tatizo kwako ni lugha, soma tena:

quote_icon.png
By FaizaFoxy
Hilo swali la uchokozi au swali la kipunguani?

There is always space for improvement. No matter how long you've been in the business - Oscar De La Hoya.


quote_icon.png
By FaizaFoxy
Hilo swali la uchokozi au swali la kipunguani?

There is always space for improvement. No matter how long you've been in the business - Oscar De La Hoya.


Bahati nzuri hata Majibu ya kipunguani kama hayo ya Kwako nayo yanasaidia kumjua punguani ni mtu wa aina gani.
Big up Mkuu Mwanakijiji hiyo like imeipenda.Hawa wasomi wetu wa aina ya Dr FaizaFoxy wanaosubiri Uprofesa wa Kimajimarefu hata kwenye vijiwe vya Kahawa hakustahili hata kukaa na kujadili na watu.
 
Last edited by a moderator:
Kwa mtu aliyetimamu wa akili anaweza kuona ni jinsi gani serikali ya CCM imefeli katika kila Nyanja labda walichofanikiwa kutuongezea UMASIKINI tu kwa kutuongezea deni la taifa...Ukitumia fikra zako vizuri utaweza kuona ni jinsi gani nchi yetu tangu kupata uhuru bado inashughulika na kero zile zile tena zikishughulikiwa na watu wale wale....Kitu ambacho bado wananchi hawajashtuka ni kuwa hakuna mabadiliko ndani ya nchi hii yatakayoletwa na serikali ya CCM kwa ajili ya kuwaneemesha wananchi , hilo kamwe halitatokea.....kungoja mabadiliko ndani ya nchi hii chni ya CCM ni sawa na kungoja usafiri wa boti TAZARA au AIRPORT.....Ukiwatazama kwa makini watangaza nia wa chama tawala kwenye hoja zao ,hakuna mwenye jibu au tiba ya matatizo ya WATANZANIA kwa kuwa wote wametokea katika mfumo huo huo uliolifanya taifa hili liendelee kuyumba kimaendeleo huku TAKWIMU zao za kutunga wakituaminisha kuwa UCHUMI unapaa...Karibia watangaza nia wote walikuwamo au bado wapo kwenye serikali hii ya CCM iliyoshindwa kuwapatia wananchi kile ambacho waliwaahidi....swali jepesi la kujiuliza je hawa watangaza nia kama walishindwa kuziongoza wizara na hatimaye kuvurunda, watawezaje kuliongoza taifa...??.....Baadhi yao wana tuhuma nzito za UFISADI mkubwa....Lakini wanatuambia kuwa wakipata nafasi ya kuliongoza taifa hili watapambana na UFISADI, kweli hoja hii inaingia akilini mwa mtu timamua au ndio kutugeuza WATANZANIA mazuzu....Wengine wanatuhumiwa kwa matumizi mabaya ya ofisi za umma na kwa amri zao wamewasababishia wananchi vidonda visivyotibika, lakini wanakuja kutuambia kuwa tukiwachagua watakuwa waadilifu, ama kweli ni kichekesho cha karne...Jibu rahisi kwa watangaza nia wote wa chama tawala hawana nia ya dhati ya kuutaka URAISI kwa maana ya URAISI bali nia yao kuutaka URAHISI ili wakafanyie uchafu wao ikulu...wengine wanasema kuwa wao sio matajiri na bado wana usaka utajiri...Hapo utagundua kuwa URAISI wa nchi hii hautafutwi kwa ajili ya kuwatumikia wananchi bali kwa ajili ya kujineemesha ndio maana haishangazi kusikia mtu anayewania nafasi ya kuteuliwa kugombea urais akitamka kuwa bado anautafuta UTAJIRI....sasa mwenyewe utajiuliza kuwa huko IKULU anapotaka kwenda atautafuta vipi utajiri..??.....Jawabu utalipata kwa kuwaangalia marafiki zao wanaowachangia ili kuzunguka kutangaza nia zao......Nawakumbusha ndugu zangu WATANZANIA wa bara na VISIWANI tuliokuwa tukilalamikia ubovu wa huduma za afya huku tukiwashudia wenzetu wakipishana angani kwenda kucheki afya zao na za familia zao huko ughaibuni , huku sisi wanyonge tukifia sakafuni mwa hospitali zisizokuwa na vifaa tiba wala dawa za kutoka chini ya uangalizi wa daktari mwenye stress za malalamiko kibao ya mishahara, Tuliokuwa tukilalamika kuhusu miundombinu mibovu ya barabara huku tukishudia misafara ya waheshimiwa wakitupita kwa kasi ya umeme kwenye mashangingi yao yalioyotokana na kodi zetu wakielekea kwenye vikao vyao vyenye posho lukuki ,huku walalahoi tukichelewa sehemu za kutafutia ridhiki kutokana ufinyu wa barabara na ubovu wa barabara ambazo marekebisho yake ni mpaka apite kiongozi mkubwa wa nje ya nchi, Wale tuliokuwa tukilalamikia UFISADI na wizi wa mali za umma, HUU NDIO WAKATI WENU WA KUFANYA MAAMUZI....MAMBO YOTE YAPO BAYANA......
 
Bahati nzuri hata Majibu ya kipunguani kama hayo ya Kwako nayo yanasaidia kumjua punguani ni mtu wa aina gani.
Big up Mkuu Mwanakijiji hiyo like imeipenda.Hawa wasomi wetu wa aina ya Dr FaizaFoxy wanaosubiri Uprofesa wa Kimajimarefu hata kwenye vijiwe vya Kahawa hakustahili hata kukaa na kujadili na watu.
Dr. Mp Kalix2, huyo anaejiita Mzee Mwanakijiji ananiogopa kupita kiasi, hawezi kujibu, anajuwa kwanini. Huwa nnampa kavu kavu za uso.
 
Back
Top Bottom