Swali la Udadisi: Sheria Gani Inasimamia Huduma za Uokoaji na EMS?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
GARI%2BSITA%2B.JPG


(Picha ya kwanza msaada wa gari lililotolewa na Prof. Muhongo jimboni kwake)

5.jpg


(Moja ya magari yaliyotolewa na Mbunge wa Chalinze Ridhiwani kusaidia wagonjwa)

1312.jpg

(Gari la wagonjwa, Marekani)

Chini video inayoonesha baadhi ya mambo yaliyomo katika magari ya kisasa ya wagonjwa; ukiondoa kitanda na ving'ora!



Nimejikuta najiuliza swali hili leo baada ya kutafakari mambo kadha wa kadha. Kuna magari ya kuzima moto (fire trucks) na tumeona mara kadhaa viongozi mbalimbali wakitoa zawadi au misaada ya magari ya kusafirisha wagonjwa (ambulance trucks) kwa ajili ya kusaidia huduma hiyo. Lakini mara kadhaa tumeona watu wanapata ajali au mtu anahitaji huduma hiyo lakini mara nyingi anategemea usafiri binafsi kuweza kuwahishwa hospitali. Na nina uhakika wa kutosha kuwa hatuna huduma ya air ambulance (helikopta zinawahi eneo la tukio la ajiri na kuwachukua wajeruhiwa ambao wanahitaji kuwahishwa zaidi hospitali kuliko kwa kutumia barabara).

Je, ni sheria gani inasimamia huduma hii? Je, huduma hii ni ya watu binafsi au ni vizuri kutegemea kampuni binafsi kufanya huduma hii ya kwanza ya dharura (EMS)? Je, wale wanaotoa huduma - kama wale wanaopewa magari ya wagonjwa) wana utaalamu gani au wamepata utaalamu wapi wa kutoa huduma hiyo? Je, ni taasisi gani inasimamia uandikishwaji na usahili wa watu wanaotoa huduma hii?

Chukulia kwa mfano wa kile kinachoitwa "gari la wagonjwa"; je, gari hilo lina vifaa gani vya kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa? Au linaitwa "gari la wagonjwa" kwa sababu lina kitanda tu na ving'ora? Na kama gari hilo linaweza kuwa na vifaa vya kisasa je, wanaolitumia wamepata mafunzo wapi ya kutumia vifaa hivyo?

Lakini swali jingine ni je, halmashauri na miji yetu ni ni mingapi imejaribu hata kuwa na dispatch unit inayoongoza magari ya wagonjwa; kwamba mtu akiita au kupiga simu nani anapokea ujumbe, na gari gani inaamuliwa kwenda wapi na nani? Je, ni kwa jinsi gani magari hayo yanahusiana na hospitali zilizoko karibu? Kuna mawasiliano yoyote?

Maswali yote haya yana umuhimu wake katika kufanikisha huduma ya dharura na uokoaji pale inapohitajika.

Au tumeamua kuendelea kuombea tu watu wasipatwe na majanga na kuwa yakitokea basi wasipate madhara makubwa? Lakini vipi wale ambao wanapata magonjwa ya ghafla wakiwa majumbani kwao, kazini au barabarani; vitu kama shinikizo la moyo au yabisi wanaweza kupatiwa msaada vipi?
 
ninavyojua mimi na uzoefu wangu ni kuwa wabongo wanazikuta ambulance hospitali,sijawahi kuona ambulance inamfata mtu mtaan au nyumbani,ni kwamba ukizidiwa hospitali ya chini unakimbizwa muhimbili au bugando na ambulance(kama una bahati hiyo).

mengine wataelezea wadau
 
Ambulance za Tanzania kazi yake ni kukumtoa mgonjwa hospitali moja kumpeleka hospitali nyingine yenye huduma zaidi.

Sijawahi kuona zikibeba wagonjwa toka majumbani.
 
Uko right.
Nimewahi kumpeleka mgonjwa mmoja hospital na ambulance fulani, ilikuwa ni majanga!
Safari ilianzia Moshi kwenda Arusha. Tulianza saa moja kamili na tulifika saa tano kasoro.
Njiani tuliishiwa mafuta mara mbili na tukalazimika kubadilisha gari, japo kampini ilikuwa ileile.
Nilijuta kwenda na yule muingereza, niliona aibu mpaka basi!

Kampuni jina Kubwa, Makao makuu south Afrika! Huduma ni ghali acha, malipo kwa dola mzee.
Bahati nzuri wazungu insuarance zao ziko vizuri sana. Japo kila wakati tukiwasiliana nilitamaani ardhi ipasuke niingie, all the time insurance wana keep contact na wao ndio wana initiate calls.
 
Mzee Mwanakijiji

Maswali mazuri sana
Je, wato huduma wanajua matumizi ya gari na vifaa na wanajua kwanini linaitwa gari la Wagonjwa?

Kwa kudokeza tu, gari la wagonjwa lina maana nyingi sana.
Kwanza, huduma ya kwanza ya mgonjwa akiwa eneo kutoka kwa watu wa 'dispatch'
Pili, huduma ya kwanza ya dharura ndani ya gari mgonjwa akielekea hospitali
tatu mawasiliano na kituo gari linapoelekea ili kuwajuza wataalam dharura inayokuja
nne, kuhakikisha hakuna uchelewashi wa safari kwa foleni za barabarani
n.k.

Pili, Je, kuna mahali katika halmashauri mtu anaweza kupiga simua na kupata huduma
Siku za nyuma ilikuwa ndiyo na tuliwahi kutumia baadhi. Huduma hiyo ikafa

Gari la wagonjwa halikai hospitali, linakaa maeneo ambayo likihitajika linapatikana kwa uharaka

Tatizo la gari la wagonjwa ni sehemu tu ya matatizo mengi yasiyoonekana kwasababu yamefunikwa na mambo ya siasa ya kutoa magari bila kujua yanatumikaje na ynasaidia vipi

Kwa mfano, utapiga wapi simu Tanzania kupata huduma ya dhararu kama 'poison control centre'
Matokeo ya hayo mtu akipata 'ajali' ya sumu watu wanashindilia maziwa ambayo kuna baadhi ya sumu ni kama vile unasaidia kuziingiza mwilini.

Ni hoja nzuri inayohitaji mjadala na hao viongozi wafungue macho
 
ninavyojua mimi na uzoefu wangu ni kuwa wabongo wanazikuta ambulance hospitali,sijawahi kuona ambulance inamfata mtu mtaan au nyumbani,ni kwamba ukizidiwa hospitali ya chini unakimbizwa muhimbili au bugando na ambulance(kama una bahati hiyo).

mengine wataelezea wadau

EEh.. yaani ambulance iko kwa ajili ya kukutoa hospitali moja kwenda hospitali nyingine? Sikuwahi kufikiria hili.
 
Uko right.
Nimewahi kumpeleka mgonjwa mmoja hospital na ambulance fulani, ilikuwa ni majanga!
Safari ilianzia Moshi kwenda Arusha. Tulianza saa moja kamili na tulifika saa tano kasoro.
Njiani tuliishiwa mafuta mara mbili na tukalazimika kubadilisha gari, japo kampini ilikuwa ileile.
Nilijuta kwenda na yule muingereza, niliona aibu mpaka basi!

Kampuni jina Kubwa, Makao makuu south Afrika! Huduma ni ghali acha, malipo kwa dola mzee.
Bahati nzuri wazungu insuarance zao ziko vizuri sana. Japo kila wakati tukiwasiliana nilitamaani ardhi ipasuke niingie, all the time insurance wana keep contact na wao ndio wana initiate calls.

Kwa hiyo kama mtu akipata emergency nyumbani kwake, kitu kama anapata stroke au amechomwa kisu mnafanyaje kuwahi hospitali au hili ndilo linaelezea ile tunayosikia mara nyingi "alifia njiani" si kwa sababu ya jeraha lenyewe au janga bali kwa sababu alikosa huduma ya kwanza kwa haraka?
 
Ambulance za Tanzania kazi yake ni kukumtoa mgonjwa hospitali moja kumpeleka hospitali nyingine yenye huduma zaidi.

Sijawahi kuona zikibeba wagonjwa toka majumbani.

Aisee yaani hapa mmenifanya nitetemeke kweli kweli duh.. sasa naogopa hata kuuliza swali liliko kichwani mwangu
 
Mzee Mwanakijiji

Maswali mazuri sana
Je, wato huduma wanajua matumizi ya gari na vifaa na wanajua kwanini linaitwa gari la Wagonjwa?

Kwa kudokeza tu, gari la wagonjwa lina maana nyingi sana.
Kwanza, huduma ya kwanza ya mgonjwa akiwa eneo kutoka kwa watu wa 'dispatch'
Pili, huduma ya kwanza ya dharura ndani ya gari mgonjwa akielekea hospitali
tatu mawasiliano na kituo gari linapoelekea ili kuwajuza wataalam dharura inayokuja
nne, kuhakikisha hakuna uchelewashi wa safari kwa foleni za barabarani
n.k.

Pili, Je, kuna mahali katika halmashauri mtu anaweza kupiga simua na kupata huduma
Siku za nyuma ilikuwa ndiyo na tuliwahi kutumia baadhi. Huduma hiyo ikafa

Gari la wagonjwa halikai hospitali, linakaa maeneo ambayo likihitajika linapatikana kwa uharaka

Tatizo la gari la wagonjwa ni sehemu tu ya matatizo mengi yasiyoonekana kwasababu yamefunikwa na mambo ya siasa ya kutoa magari bila kujua yanatumikaje na ynasaidia vipi

Kwa mfano, utapiga wapi simu Tanzania kupata huduma ya dhararu kama 'poison control centre'
Matokeo ya hayo mtu akipata 'ajali' ya sumu watu wanashindilia maziwa ambayo kuna baadhi ya sumu ni kama vile unasaidia kuziingiza mwilini.

Ni hoja nzuri inayohitaji mjadala na hao viongozi wafungue macho

Nimeuliza hili kwani wiki chache nyuma Rais naye alitoa msaada wa magari ya "wagonjwa" kiasi kwamba inashangaza kama alimaanisha kwa ajili ya kusaidia kuwaokoa watu wanaoopata dharura au kweli ni la kubeba wagonjwa - toka hospitali moja kwenda nyingine - na siyo kwa ajili ya kuwahisha watu hospitali.
 
Kwa hiyo kama mtu akipata emergency nyumbani kwake, kitu kama anapata stroke au amechomwa kisu mnafanyaje kuwahi hospitali au hili ndilo linaelezea ile tunayosikia mara nyingi "alifia njiani" si kwa sababu ya jeraha lenyewe au janga bali kwa sababu alikosa huduma ya kwanza kwa haraka?
Ukipata dharura nyumbani kwako unatakiwa kuita Bajaji au Bodaboda ikuwahishe kwenye a Near by Health Centre (Mungu jalia iwe na Ambulance)
Bajaj ama Bodaboda zinaweza ku Manuva vizuri na Follen,au kama una gari lako basi unawasha Hazard halafu unapita kulia kwa barabara na kutanua kama kuna Follen,traffic akikukamata akimuona Mgonjwa atazidi kukusaidia kukukwamua kutoka kwenye follen na kuwahi Kituo cha Afya.
Ova.
 
Emergence Medicine ni somo jipya sana nchini ...nadhani hadi sasa ni Muhimbili pekee yenye kitengo chenye wataalamu waliosomea emergency medicine.

Kiukweli somo la dharura kwa ujumla wake hapa Tanzania ni tatizo.
 
Nimeuliza hili kwani wiki chache nyuma Rais naye alitoa msaada wa magari ya "wagonjwa" kiasi kwamba inashangaza kama alimaanisha kwa ajili ya kusaidia kuwaokoa watu wanaoopata dharura

au kweli ni la kubeba wagonjwa - toka hospitali moja kwenda nyingine -

na siyo kwa ajili ya kuwahisha watu hospitali.
Mkuu hii mada ni muhimu sana kwa Taifa.
Kuna misconception kubwa sana katika suala zima la dharura. Maana ya gari la wagonjwa haijulikani kabisa.

Ningependa huu mjadala uwe endelevu, ni muhimu sana kwakweli
 
Vipi kuhusu CPR?

Inafundishwa mashuleni siku hizi?

Mimi sikumbuki kabisa kama ilikuwa inafundishwa enzi nikiwa bado mwanafunzi wa msingi na upili.

Na hata hao wato huduma ya dharura wanao huo ujuzi kweli?
 
ninavyojua mimi na uzoefu wangu ni kuwa wabongo wanazikuta ambulance hospitali,sijawahi kuona ambulance inamfata mtu mtaan au nyumbani,ni kwamba ukizidiwa hospitali ya chini unakimbizwa muhimbili au bugando na ambulance(kama una bahati hiyo).

mengine wataelezea wadau
Yaani ni kinyume kabisa.

Mgonjwa aliyeko Mwanayamala yupo katika uangalizi. Kuhamishiwa Muhimbi inaweza kuwa si dharura bali uangalizi wa karibu kwa wataalam wa juu. Huyu anaweza kusafirishwa na gari lolote kwasababu 'stability' yake inajulikana

Mgonjwa aliyegongwa na piki piki nahitaji Ambulance kwasababu , kwanza, ni dharura na pili hana uangalizi wowote
Huyu anahitaji Ambulance ya kumpeleka Mwananyamala au Muhimbili akipatiwa huduma njiani kuokoa maisha

Hapa ndipo suala la watumishi wa Ambulance linapokuja. Kwamba, wanaweza kufanya assessment on spot na kubaini dhurura husika inahitaji Hospitali gani.

Kwa mfano, mtu aliyepata ajali ya gari hawezi kuhema, solution si kumkimbiza Muhimbili.
Ni kumpeleka hospitali kubwa ya karibu ili kuokoa maisha na si kufikisha 'marehemu' Muhimbi kwa dharura

Katika mazingira hayo hayo, assessment inaweza kuonyesha mtu kavunjika mguu.
Hakuna dharura nyingine inayoweza kusababisha kifo lakini ukubwa wa jereha unahitaji utaalam wa MOI.
Huyu anakimbizwa MOI

Gari la Wagonjwa linakaa katika maeneo mkakati ili kufikia dharura.

Hapa suala si gari tu, ni je, watumishi wanajua kukabiliana na dharura?

Vifaa vya Ambulance kama mawasiliano na hopsitali zingine vina connections au ni ving'ora tu

Think about this, mtoto ameingiwa na harage sikioni. Mwananyamala hawana vifaa vya kulitoa na wanafanya referral Muhimbili kwasababu tu hawana vifaa na wala si hatari ya maisha. Hawa wanatumia Ambulance kama unavyosema

Kuna mzazi yupo kimara, mtoto ameshindwa kutoka, mama anavuja damu. Halafu hakuna Ambulance kwasababu tu imepeleka muhimbi mtoto aliyeingiwa na harage sikioni!

Ambulance ina maana kubwa sana, kuanzia position inapotakiwa iwepo, vifaa vyake, watumishi wake wakiwemo madereva n.k. Si suala la kuhamisha wagonjwa na kama ni hivyo tununue bajaji nyingi tu
 
Vipi kuhusu CPR?

Inafundishwa mashuleni siku hizi?

Mimi sikumbuki kabisa kama ilikuwa inafundishwa enzi nikiwa bado mwanafunzi wa msingi na upili.

Na hata hao wato huduma ya dharura wanao huo ujuzi kweli?
Yaani ni tatizo kubwa kweli.
Nawashangaa wanasiasa wanamwaga Ambulance tu. Kwa mazingira ninayoona ni afadhali wapeleke Bajaji
Maan nzima ya Ambulance haipo
 
Vipi kuhusu CPR?

Inafundishwa mashuleni siku hizi?

Mimi sikumbuki kabisa kama ilikuwa inafundishwa enzi nikiwa bado mwanafunzi wa msingi na upili.

Na hata hao wato huduma ya dharura wanao huo ujuzi kweli?
hata huko marekani ukiondoa Madaktari wachache wengi hawajui CPR....CPR sio neno tu ni kazi nzito.
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom