Swali la kizushi; Kwa nini umtendee mwenzako mabaya?

Equation x

JF-Expert Member
Sep 3, 2017
29,189
39,954
Kama miaka 10 iliyopita hivi nilipata safari ya kikazi kwenda huko mbali kwa muda wa miezi sita. Kwa sababu ndoa yangu ilikuwa bado ni changa, nikaona nimtafutie majukumu mazito mama watoto wangu ili nitakapokuwa huko nje, asiweze kushawishika na mabaharia wa mjini.

Nikampa kazi ya kwenda kusimamia ujenzi wa nyumba ya kufikia huko kijijini; siku ilipofika ya kuondoka, niliondoka na yeye akaenda kijijini kwa ajili ya kutekeleza majukumu niliyomuachia. Nikiwa huko ugenini, nilikuwa nafanya mawasiliano ili kujua kinachoendelea nyumbani, pamoja na kazini.

Baada ya kumaliza kilichonipeleka huko ugenini, nilirudi nyumbani na familia ilinipokea vizuri; ingawa nilikuwa na kama wiki mbili hivi za kupumzika kabla ya kuripoti kazini. Kwa muda ule niliutumia kuwa karibu na familia, pamoja na kupunguza uchovu wote niliotoka nao safari.

Ndipo mama watoto, akanishawishi twende kijijini ukaone kazi uliyoniachia; nami nikamkubalia nikamwambia twende na familia angalau tukaone alichokifanya. Kwa ujumla alifanya kazi nzuri, nami nikamwambia inabidi tuizindue kwa kulala humo angalau kwa siku tatu.

Kesho yake jioni majira ya saa 11 jioni, niliamua kujilaza kwenye veranda hapo nje ili kupata upepo wa nje, pamoja na kunyoosha mgongo vizuri. Baada ya kama nusu saa hivi, nilihisi kitu kimenipiga shingoni, najaribu kugeuza shingo hivi, inakataa na kuwa ngumu huku inauma, nainua mkono wa kushoto unakata, mguu wa kushoto unakataa, kichwa kinagoma; daa nililia kama mtoto mdogo ,ndipo watu wakaja kwa ajili ya kunipa msaada. Wakajaribu kunikanda na aina fulani ya majani, nafuu haikupatikana; ikabidi wanipeleke hospitali ya wilaya, baada ya dokta kunicheki haoni tatizo, zaidi ya kunipa dawa za kutuliza maumivu.

Ndipo baba mmoja akawa na wazo, hebu mpelekeni kwenye tiba ya asili; Kule na wenyewe wakafanya yao, wakasema kama ningecheleweshwa kuna uwezekano nisingemaliza wiki. Ila wakasema changamoto ni huko kazini, na hata ukirudi huko watakushangaa kwa kusalimika. Kesho yake ilipofika maumivu hakuna na nikawa niko powa,tukalipia gharama, na tiba nyingine nikaondoka nazo kwa ajili ya kutumia.

Safari ya kurudi kazini ilipowadia, nilipanda basi na kwenda huko mkoani; tunakaribia kufika huko mkoani, basi nililokuwemo likapoteza uelekeo na kuingia kichakani na kupinduka; bahati nzuri lililala kiubavu na hakuna mtu aliyefariki zaidi ya majeraha tu; mi niliumia vidole vya mikononi kwa sababu nilikuwa napiga ngumi ili nipasue kioo. Ndipo tukapata usafiri mwingine na kuondoka.

Nilipofika kazini, kila mmoja ananitazama; umefikaje fikaje huku; mi nikawa nawauliza kwa nini mnaniuliza hivyo? Wakawa wanacheka tu, basi tukaendelea na maisha ya mzigoni, ila kuna wengine waliomba kuhama kutokana na sababu zao wanazozijua. Ilinibidi nisiwe nasafiri safiri kwa muda mpaka ile kumbukumbu ya ajali itakapoisha. Na nilifanikisha hilo.

Swali la kizushi; Kwa nini umtendee mwenzako mabaya?

NB: Ishi na wenzako kwa akili, 'co-workers are not your friends'
 
Kama miaka 10 iliyopita hivi nilipata safari ya kikazi kwenda huko mbali kwa muda wa miezi sita. Kwa sababu ndoa yangu ilikuwa bado ni changa, nikaona nimtafutie majukumu mazito mama watoto wangu ili nitakapokuwa huko nje, asiweze kushawishika na mabaharia wa mjini.

Nikampa kazi ya kwenda kusimamia ujenzi wa nyumba ya kufikia huko kijijini; siku ilipofika ya kuondoka, niliondoka na yeye akaenda kijijini kwa ajili ya
Umechelewa kuwafaham binadam
 
Kama miaka 10 iliyopita hivi nilipata safari ya kikazi kwenda huko mbali kwa muda wa miezi sita. Kwa sababu ndoa yangu ilikuwa bado ni changa, nikaona nimtafutie majukumu mazito mama watoto wangu ili nitakapokuwa huko nje, asiweze kushawishika na mabaharia wa mjini.
Hizi kazi za kua jiliwa ni ushirkina mtupu tena wewe una bahati rafiki yangu baada ya kupandishwa cheo alibadilisha na hao hao co-workers akawa anawika kama jogo kila baada ya lisaa, alishauliwa ache kazi, paka leo iko nyumbani..........pesa sio kitu bora afya na amani
 
Hizi kazi za kua jiliwa ni ushirkina mtupu tena wewe una bahati rafiki yangu baada ya kupandishwa cheo alibadilisha na hao hao co-workers akawa anawika kama jogo kila baada ya lisaa, alishauliwa ache kazi, paka leo iko nyumbani..........pesa sio kitu bora afya na amani
Kweli mkuu
 
Aliyekuwa rafiki yangu (classmate) alipoteza maisha kwasababu ya kazi. Baada ya kumaliza masomo aliomba kazi mkoa fulani akapata. Aliteuliwa kuwa mkuu wa idara fulani nyeti kwasababu ya elimu yake, hivyo Mzee aliyekuwa mkuu wa idara hiyo alilazimika kushushwa kwakuwa elimu yake ilikuwa ni ndogo.

Mzee akamkabidhi gari kijana japo kwa shingo upande. Kilichofuata ni kijana kupooza na hospital kila wakipima vipimo hakuonekana kuwa na ugonjwa wowote. Mwaka mmoja jamaa akatangulizwa mbele ya haki. Iligundulika ni Mzee aliyeshushwa cheo baada ya kuropoka yeye mwenyewe huko walikokuwa wakilewa pombe.
 
Wafanyakazi wenzako maisha yote sio marafiki zako, cha kukushauri ni kwamba "Fanya kazi, pata ujira wako endelea na mambo yako" anaekupiga mpige usimuache maana amekusudia kukuumiza ama kukuua kabisa!
Ukiangalia wengi makazini mwao ni uadui mtupu ndio unaendelea!!

Wakishastaafu hawa wazee mambo hayo yatakuwa hamna!!!! Sina hakika km vijana wanalogana labda uko ccm..... vijana wapo smart wazee ndo wana uwoga wakupoteza nafasi zao kwenda kwa vijana ndo sababu wanawamaliza
 
Ukifanyiwa jambo huwezi jua tatizo mpaka umefanyiwa hivyo ni kwa nini ?

Jitazame kuburi chako kwa wengine, hujawagi kushiriki wenzako wapate adhabu au kutaka kuvunja mahusiano ya watu wewe ukaona n haki ufanye hivyo.

Mara nyingi mnaologwa huwa mnanguvu kuzidi walio chini yenu wanakosa cha kuwafanya zaidi ya ndumba.

Ukiwa juu usishiriki kuharibu ndoa ya mtu,kazi au jambo lolote kwa nafasi yako hata umbea na ichonganishi.

kikubwa jitathimini kama watu wote walikua wanajua hutorudi huenda unatatizo pia .

Mshukuru Mungu kwa kila jambo.
 
Wakishastaafu hawa wazee mambo hayo yatakuwa hamna!!!! Sina hakika km vijana wanalogana labda uko ccm..... vijana wapo smart wazee ndo wana uwoga wakupoteza nafasi zao kwenda kwa vijana ndo sababu wanawamaliza
Mzee uchawi hauna sura, siku hizi hata vijana wanayo hayo mambo! Ukimkuta nje yuko smart kachomekea huwezi amini! Ila kwenye anga zake ni gwiji kuliko Chriss Katembo kwenye fani yake ya uchoraji!
 
ukifanyiwa jambo huwezi jua tatizo mpaka umefanyiwa hivyo ni kwa nini ?

jitazame kuburi chako kwa wengine, hujawagi kushiriki wenzako wapate adhabu au kutaka kuvunja mahusiano ya watu wewe ukaona n haki ufanye hivyo.

Mara nyingi mnaologwa huwa mnanguvu kuzidi walio chini yenu wanakosa cha kuwafanya zaidi ya ndumba.

ukiwa juu usishiriki kuharibu ndoa ya mtu,kazi au jambo lolote kwa nafasi yako hata umbea na ichonganishi.

kikubwa jitathimini kama watu wote walikua wanajua hutorudi huenda unatatizo pia .

Mshukuru Mungu kwa kila jambo.
Hayajakukuta bado, watu wanatenda wema na bado wanaumizwa
 
Ukifanyiwa jambo huwezi jua tatizo mpaka umefanyiwa hivyo ni kwa nini ?

Jitazame kuburi chako kwa wengine, hujawagi kushiriki wenzako wapate adhabu au kutaka kuvunja mahusiano ya watu wewe ukaona n haki ufanye hivyo.

Mara nyingi mnaologwa huwa mnanguvu kuzidi walio chini yenu wanakosa cha kuwafanya zaidi ya ndumba.

Ukiwa juu usishiriki kuharibu ndoa ya mtu,kazi au jambo lolote kwa nafasi yako hata umbea na ichonganishi.

kikubwa jitathimini kama watu wote walikua wanajua hutorudi huenda unatatizo pia .

Mshukuru Mungu kwa kila jambo.
Mkuu naona ww nimgeni wahaya mambo mtu anakuroga bila sababu yoyote,
 
Hizi kazi za kua jiliwa ni ushirkina mtupu tena wewe una bahati rafiki yangu baada ya kupandishwa cheo alibadilisha na hao hao co-workers akawa anawika kama jogo kila baada ya lisaa, alishauliwa ache kazi, paka leo iko nyumbani..........pesa sio kitu bora afya na amani
🤣🤣🤣🤣🤣🤣Sivuti picha yupo kwenye daladala siti ya nyuma anaanza kuwika.
Binadamu sio viumbe wazuri kwa kweli.

Ile ningependa kumjua huyo mtaalam wa kuwikisha. Ningeanza kuwaroga wabunge, wakiwa mjengoni ni mwendo wa kuwika tu. Wanapokezana🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom