Swali la kizushi kwa Dr Slaa, Mbowe, Mnyika, Mkumbo na Wanachadema

Katiba inayotakiwa kubadilishwa ni katiba ya Jamhuri ya muunga wa Tanzania na si ya Zanzibar. Na hata ikibadilishwa hiyo ya Muungano na kuweka serikali tatu , ya znz ya muungano/shirikisho na ya tanganyika bado katiba ya znz itaendelea kusomeka kama inavyosomeka sasa.

Na hata hii katiba inayopigiwa ukunga haiandikiki ikaisha leo ni jambo ya muda 2,3,4,5 years pengine so meanwhile tunayo hii ya sasa "titi la mama tamu hataka kama la mbwa" tuiheshimu na kuheshimu maoni ya wananchi wa Zanzibar tusiwabeze na kuwajeli. Nadhani CDM inahitaji wanachama kule ili kiwe na sura ya kimuungano zaidi basi ushauri wangu ni kuwa wasiwadhihaki wazanzibar kwa maneno ya kejeli wao ndio waliopiga kura za maoni na si kama inavyozungumzwa na viongozi wa CDM kuwa CCM na CUF wao ndio wamepanga.

Mkuu hapa ujumbe wako uko wazi zaidi: hujafurahia bezo za CDM kwa muungano wa CUF na CCM huko Z'bar. Hilo ni jingine. Lakini ukirejea kuhusu CDM watafanya nini wakifanikiwa kufikia ushindi wa kwanza au wa pili huko Zanzibar basi hauna budi kujiuliza kwanza CDM wana visheni gani kuhusu ushiriki wao kwenye serikali ya Z'bar? Ndipo ninapojibu kuwa sioni kama CDM wana mpango wa dhati wa kushika uongozi wa serikali huko Zanzibar.

Nionavyo, kama mambo yakienda kama wanavyotaka (katiba mpya) basi Zanzibar inaweza kuongozwa na chama kingine na wao wakabakia bara (sitaki kusema Tanganyika) na kushirikiana kwenye serikali ya muungano kulingana na katiba mpya itakavyoainisha.
 
Mbowe alisema wakati wa mdahalo na Hamad Rashid kuwa Yeye (Mbowe) alienda kuzungumza na CUF (Hamad Rashid) kuwataka washirikiane kwenye kambi ya upinzani, alikuwa hajui kuwa CUF imeolewa na CCM?

Hujamalizia sentensi...walitaka washirikiane lakini akataka ufafanuzi wa CUF inasimamaje ikiwa ndani ya GNU.
Kimsingi reception ya CUF was negative in the first place.

Ila at day end we are discussing something whose end result is 0%
 
Ndugu Yangu mtoa Mada umeuliza maswali mazuri sana na umejaribu kutoa majibu mazuri sana katika baadhi ya hoja ulizozitoa. Umesimika hoja zako kwenye katiba, sheria na taratibu.

Tatizo ninaloliona kwako ni kuendeleza fikira zaidi ya hapo ulipofikia na kuona kuwa nchi ya Zanzibar ina Serikali ya Umoja wa Kitaifa inayoshirikisha vyama viwili tu vya siasa kwa sababu ya matakwa ya kikatiba then ukageuka kutizama sheria na kanuni za Bunge la Jamhuri ya Muungano zinasema nini kuhusu Kambi ya Upinzani Bungeni. Kwa kanuni hizo Chadema wanayo haki au hawana haki ya kuunda hivyo kambi?

Well, ni maswali magumu ila yanahitaji akili nying na Busara kidogo ila inaonesha wazi una akili nyingi ila umekosa Busara ndogo tu ya kuyaangalia mambo hayo kwa mapana yake katika misingi ya Katiba, Sheria, Kanuni na taratibu za nchi.
 
Kadhalika kanununi zinasema chama cha upinzani kitakachopata zaidi ya 12.5% ya viti ndicho kitakachounda kambi ya upinzani. Ndivyo kanuni zinavyoeleza
Mkuu,

Hili hakuna anayelipinga,lakini katika bunge hakuna kipengele kinachozuia pia Chama hicho kinachopata asilimia hizo kisishirikishe vyama vyengine...hii ndio tofauti..mimi ninaona wakiwashirikisha wengine,si lazima CUF ni kuupa nguvu upinzani na hivyo kusukuma mbele mabadiliko...itawafavour CDM kuonekana kuwa ni chama kinachopigania umoja, kuliko pekee pekee.

Wengi waCDM wanafikiri sisi wengine tunapigia debe CUF..ni kuwa tunaona ushirikiano wa upinzani ni kitu chema na kinawaleta wananchi wanaounga mkono vyama vya upinzani kujenga matumaini kuwa wanaelekea kuzuri.
Hakuna anaye-force CDM iwaingize wengine, sisi tunatoa rai kuwa ni jambo zuri kufanya hivyo. Pia ni kwa manufaa ya upinzani wote.
 
Mkuu,

Hili hakuna anayelipinga,lakini katika bunge hakuna kipengele kinachozuia pia Chama hicho kinachopata asilimia hizo kisishirikishe vyama vyengine...hii ndio tofauti..mimi ninaona wakiwashirikisha wengine,si lazima CUF ni kuupa nguvu upinzani na hivyo kusukuma mbele mabadiliko...itawafavour CDM kuonekana kuwa ni chama kinachopigania umoja, kuliko pekee pekee.

Wengi waCDM wanafikiri sisi wengine tunapigia debe CUF..ni kuwa tunaona ushirikiano wa upinzani ni kitu chema na kinawaleta wananchi wanaounga mkono vyama vya upinzani kujenga matumaini kuwa wanaelekea kuzuri.
Hakuna anaye-force CDM iwaingize wengine, sisi tunatoa rai kuwa ni jambo zuri kufanya hivyo. Pia ni kwa manufaa ya upinzani wote.

Lakini hata Dr Slaa alipokuwa anajibu hili alisema kimsingi hawana tatizo na kushirikisha vyama vingine endapo vitakuwa tayari kuvunja ndoa yao na cuf. Kimsingi, ccm wamewaowa cuf, cuf nao wamewaoa nccr+tlp, ambapo by imlication ccm imewaowa wote hao. Sasa wahamue kimoja. Haya mambo tulianza kuyaona tu baada ya kifo cha Wangwe wakati wa ule umoja wa vyama vinne, nadhani unakumbuka jinsi kila kiongozi alivyokimbilia tarime. Je, hawa kweli hawana balozi mmoja leo? Mimi nadhani tunahitaji kujenga upinzani wenye maana badala ya kushia kwenye upinzani wa kuchumia tumbo wakati taifa linayoyoma.
 
Kwa mtazamo wangu CDM hawawezi kufanya mambo yao nje(Bila kufuata) ya KATIBA ya jamhuri ya Muungano ya Tanzania, suala la Serikali ya mseto ZNZ halipo kwenye katiba yetu, kama wewe ni muungwana unawezaje kushirikiana na chama kinachovunja katiba ya nchi dhairi (bila kificho).
vyama vingine ambavyo vinafuata katiba ya nchi is ok.
CDM tunapenda amani iliyopo ZNZ iendelee ambayo imeletwa na serikali ya Mseto ndio maana tunapigania katiba mpya ili suala la mseto liingizwe kwenye katiba ili liwe kisheria zaidi.
Nashauri tupiganie katiba mpya ili pasiwepo na kupingana kwa vyama vya upinzani.
 
Kwa mtazamo wangu CDM hawawezi kufanya mambo yao nje(Bila kufuata) ya KATIBA ya jamhuri ya Muungano ya Tanzania, suala la Serikali ya mseto ZNZ halipo kwenye katiba yetu, kama wewe ni muungwana unawezaje kushirikiana na chama kinachovunja katiba ya nchi dhairi (bila kificho).
vyama vingine ambavyo vinafuata katiba ya nchi is ok.
CDM tunapenda amani iliyopo ZNZ iendelee ambayo imeletwa na serikali ya Mseto ndio maana tunapigania katiba mpya ili suala la mseto liingizwe kwenye katiba ili liwe kisheria zaidi.
Nashauri tupiganie katiba mpya ili pasiwepo na kupingana kwa vyama vya upinzani.

Mkuu,
Tunachanganya mambo mengi ...Hivi katiba ya Zanzibar ni sehemu inayojitegemea au ni ndani ya katiba ya Tanzania?
Well, mimi ninafahamu huu mchanganyiko, mkorogo lakini ni matatizo aliyotuundia mwalim kwa ujanja wake...
Vipi katiba ya Muungano iingize ndani katiba ya Tanganyika au Zanzibar?
Kuna jurisdictions 3 Tanzania, soma Chapisho, Shirikisho ndani ya shirikisho utaelewa nini nazungumza. Na kila moja inajitegemea, sio kwamba moja ni superior na nyengine ni subordinate.
kwa hiyo umezungumza point lakini umeichanganya...CDM pia wanafanya kosa hilo hilo.

NB
Kuna thread ya shirikisho ndani ya shirikisho hapa JF, ipitie.
 
CCM wanafedha nyingi ndio maana wamekinunua CUF..........kama ningekuwa na fedha kama mafisadi ningekinunua CCM na kukigeuza kuwa chama cha mchezo wa kuigiza na mazingaombwe kwani kimepoteza uelekeo ila kina vitega uchumi vizuri kama jengo la umoja wa vijana linalojengwa na fedha za BOT wanatudanganya eti Patel ndio mmiliki wake na uwanja aliotaka kuuza lau kule mwanza
 
Heshima zenu waheshimiwa ndugu Dr Slaa, Mbowe, Mnyika na Mkumbo, Najua nyie ni wana JF mpo katika hii himaya ya kina invisible na uwepo wenu hapa jamvini umeleta tija kubwa kwa kutujuza mambo mbalimbali ya kimapinduzi na kisiasa.

Sina uhakika kama wote mpo jamvini lakini nina uhakika kuwa Dr Slaa, Mnyika na Mkumbo tunao humu jamvini kwa maana nimeona post zao nyingi tu.


Nisiwachoshe na maelezo naomba niulize maswali mawili la pili likiwa na sehemu aa na be.

1.Kutokana na tamko lenu kuhusu KUB kuwa hamtawashirikisha CUF kwa kuwa imo ndani ya Serikali ya kitaifa je mtawashirikiasha UDP na NCCR - Mageuzi? na kama hamtawashirikisha ni kwanini?

2.Ninavyoona hamuwatendei haki Wazanzibari ambao miongoni mwao wapo wanaCDM kwa maana Serikali ya umoja wa kitaifa wao waliupigia kura za maoni na kura hizo ndizo zilizopelekea kubadilishwa katiba na kusomeka kama ilivyo sasa.

a) Je kwa katiba iliyopo Zanzibar ikitokea one day YES kwa CDM wakashinda wao na kufuatiwa na chama kingine cha pili mtaunda serikali ya zanzibar peke yenu?

b)Je ikitokea siku moja mkashika nafasi ya pili Zanzibar na katiba inasema kuna Serikali ya kitaifa mtakubali ku join hands na walioshinda ili kuwatumikia wananchi?

Nina maswali mengi lakini hayo ni yamsingi mengine ya nyongeza yatakuja baada ya kujibiwa hayo maswali.

Naomba kuwakisha na kutoa shukrani zangu za awali kwa majibu yenu mazuri na yenye kunifanya niwe huru na haya maswali yanayoniumiza kichwa tangu mlipotoa tamko kuhusu kuwashirikisha CUF na vyama vingine kwenye KUB.

Mohammed H. Shossi

Safarini Ngamiani,

Shossi maswali yako mazuri: Ningekuwa mimi ndio muulizwa swali ningejibu hivi;-
1. CDM ilishaweka wazi kwamba iko tayari kuwashirikisha wapinzani wasio wana CUF endapo watajitoa kwenye ndoa yao na CUF maana CUF tayari wameshaunda serikali kwa kushirikiana na chama tawala kwa hiyo wao ni sehemu ya chama tawala.
2. Kuhusu kutowatendea haki wana-CHADEMA wa zanzibar hiyo si kweli maana tulichofanya ni maamuzi ya chama. isitoshe kura ya maoni zanzibar ilipita kwa 61% maana yake ni kwamba huenda 39% ni wana- CHADEMA ambao hii leo wanataka pasiwe na ndoa ya aina hii! Kimsingi hayo Makubaliano si CCM na CUF bali Maalim na Karume kwani mwenye mamlaka ya kufanya makubaliano ya aina hiyo ni Mwenyekiti wa CCM/CUF kupitia kamati kuu tofauti na jinsi ilivyotokea zanzibar kwa Karume na Saif kukubaliana Chumbani. Kwa kuongezea hoja hiyo ilitakiwa vyama vyote vya siasa viingie kwenye majadiliano hayo ya siri!
3": kuhusu kushirikisha chama kinachofuatia lazima ifanyike hivo maana ni matakwa ya katiba. Kama sisi chadema tulitii kutoenda mahakamani au kuitisha maandamano ya nchi nzima kupinga matokea kutokana na zuio lililopo ndani ya katiba ya nchi, kwanini tusiheshimu katiba ya zanzibar?
Angalizo: kama CUF bara wameshindwa kuwa kambi rasmi ya upinzani na wanataka kubadili kanuni za bunge ili wengine wasivae kiatu walichofaidi kwa miaka 15, kwanini Zanzibar wasitumie mbinu hiyo mara watakaposhindwa kuwa washindi wa pili? na endapo wakiwa watawala completely kwa nini wasikifute hicho kipengele ili wabaki wenyewe?

NDUG YANGU MOHAMAD; Sipendi kuonyesha ushabiki but historia inaonyesha Lipumba na Seif ni Masultani and mark my word that, siku wakiondoka CUF ndo utakuwa mwisho wa hicho chama. Chunguza watu wot walowahi kuhoji utendaji wao katika chama jinsi walivyotimuliwa. Ninaamini siku CUF chini ya Lipumba na Seif wakichukua nchi fahamu papo hapo itakuwa ya ki-sultani ni bora hata CCM waendelee kuongoza kuliko hao jamaa wawili!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!11 they are the most dangerous Leader in our Country!!
 
CCM wanafedha nyingi ndio maana wamekinunua CUF..........kama ningekuwa na fedha kama mafisadi ningekinunua CCM na kukigeuza kuwa chama cha mchezo wa kuigiza na mazingaombwe....

Mkuu,
Wewe unasema CCM imenunua CUF, wengine wanasema CUF kaolewa na CCM, wengine CUF kafunga ndoa na CUF, wengine CUF wanalala kitanda kimoja na CUF...hii lugha inayotumika ndio hiyo mchezo wa kuigiza na mazingaombwe!

Mkuu, Siasa za TZ unazielewa vilivyo?
Kwa picha ya jana unaweza kusema kuwa Mbowe amenunuliwa na Kikwete? au Kikwete kanunuliwa na Mbowe? au wamekuwa "wapenzi"?
Tuache hizi siasa majitaka, hazitusaidii kama wanyonge, zinatugawa na wajanja wanaendelea kula nchi.
CDM imepata kura ngapi uchaguzi mkuu, CUF wamepata ngapi? Kama una jibu basi ujue upinzani una safari ndefu.... wabunge wangapi CDM, CUF, NCCR?
 

Utaona wanachadema wanaoulizwa wanaview na kusepa maana maswali yamesimama hasa yanabidi kujipanga ikiwezekana kuPM mwenye uelewa zaidi, napenda na kuwaheshimu hao wasoamao na kusepa nadhani watatafakari kwa kina maswali haya na Mungu atawafungua macho yao na kuona kilichojificha kwenye giza la upinzani Tanzania.
..ndoto kubwa kabisa! Kuota mtanzania wa sasa kukipa umakini kilichoandikwa!! Tunachohitaji tulio wengi wetu ni kusikia fulani amesema nini, iwe kwa kusikia wenyewe ama kunukuliwa na wengine wetu!! Bado hatujawa na mikakati maalumu ya kujua tunataka kwenda wapi na tunaendaje. Bado tunashabikia siasa ambazo nazo hatujazijua vema!

Mungu Ibariki Tanzania.
 
Swali la kizushi kwa Dr Slaa, Mbowe, Mnyika, Mkumbo na Wanachadema
Heshima zenu waheshimiwa ndugu Dr Slaa, Mbowe, Mnyika na Mkumbo, Najua nyie ni wana JF mpo katika hii himaya ya kina invisible na uwepo wenu hapa jamvini umeleta tija kubwa kwa kutujuza mambo mbalimbali ya kimapinduzi na kisiasa.

Sina uhakika kama wote mpo jamvini lakini nina uhakika kuwa Dr Slaa, Mnyika na Mkumbo tunao humu jamvini kwa maana nimeona post zao nyingi tu.


Nisiwachoshe na maelezo naomba niulize maswali mawili la pili likiwa na sehemu aa na be.

1.Kutokana na tamko lenu kuhusu KUB kuwa hamtawashirikisha CUF kwa kuwa imo ndani ya Serikali ya kitaifa je mtawashirikiasha UDP na NCCR - Mageuzi? na kama hamtawashirikisha ni kwanini?

2.Ninavyoona hamuwatendei haki Wazanzibari ambao miongoni mwao wapo wanaCDM kwa maana Serikali ya umoja wa kitaifa wao waliupigia kura za maoni na kura hizo ndizo zilizopelekea kubadilishwa katiba na kusomeka kama ilivyo sasa.

a) Je kwa katiba iliyopo Zanzibar ikitokea one day YES kwa CDM wakashinda wao na kufuatiwa na chama kingine cha pili mtaunda serikali ya zanzibar peke yenu?

b)Je ikitokea siku moja mkashika nafasi ya pili Zanzibar na katiba inasema kuna Serikali ya kitaifa mtakubali ku join hands na walioshinda ili kuwatumikia wananchi?

Nina maswali mengi lakini hayo ni yamsingi mengine ya nyongeza yatakuja baada ya kujibiwa hayo maswali.

Naomba kuwakisha na kutoa shukrani zangu za awali kwa majibu yenu mazuri na yenye kunifanya niwe huru na haya maswali yanayoniumiza kichwa tangu mlipotoa tamko kuhusu kuwashirikisha CUF na vyama vingine kwenye KUB.

Mohammed H. Shossi

kaka huwa nafatilia sana post zako za kisiasa na pale unapochangia coment kwa post za watu wengine.
Nimegunduwa kuwa wewe ni cuf damu kama tulivyo sisi wengine kwa CDM. Ila upendi kujionyesha kuwa
wewe ni mwana NGANGARI. Ila kuna msemo unasema WENGI WAPE,NA SAUTI YA WENGI NI SAUTI YA
MUNGU. kaka majority ya watanzania bara wote wameunga mkono chadema kuwakataa CUF na sababu
zote ushapewa hapa jamvini. Kaa na utulie tu mkuu! utaumiza ubongo wako tu.
 
Mohammedi Shossi,

Hongera mkuu,nina imani kuwa unao Moyo wa kizalendo wa kujenga Tanzania yenye nguvu Africa na duniani.

Hata hivyo nikujibu swali lako la pili kwa kifupi tu,CHADEMA Ina wafuasi Zanzibar,wangepata wabunge kupitia CHADEMA lazima wangewakuwa sehemu ya kambi ya Upinzani.Lakini kusema kuwa kwa kuwa ati hawana Mbunge Zanzibar,basi iwe heri kwa CUF kupitia mgongo wa CHADEMA,huo ni ufisadi,uvivu,kupoteza dira na kukosa msimamo wa kiitikadi!nikomee hapo kwa sasa.
 
I cant believe u if ur a Tanganyika guy kwa sababu ya maswali yako ya kutaka kuchokonoa chokonoa
Kwa hilo nakubaliana na wewe na ujue pia muungano tunaoujua mimi na wewe ni tofauti na wanaujua kina Seif Sharif na Mzee Aboud Jumbe na Mzee Karume. Mzee Karume kuna kipindi alipoona anabanwabanwa na Nyerere alinukuliwa kuwahi kusema "muungano ni kama koti likikubana unalivua"

Pia ikumbukwe kuwa ziliungana nchi mbili wazanzibari wana taifa lao na bado lina exist kwahiyo tusiwaonee choyo na wivu tumtafute mchawi wetu alieiuza nchi yetu ya Tanganyika ikaondoka kwenye uso wa dunia.

Kuhusu CCM (ASP) na CUF (HIZBU) kuna mikakati ya haja kuiweka mizizi ya CHADEMA (UMMA PART) zanzibar wale wa umma part ya Abdulrahman Babu wataingia hapa na mchezo utanoga na kuwa mkazi zaidi.

Ua unaonaje mzee?
 
Ahali yangu.

Chadema si chama cha kisiasa bali ni chama cha udugu, Ukabila na Udini.

Wao siku zote wanafakiri muafaka zanzibar ulitokea hivihivi tu bila CUF kufanya kazi ya ziada visiwani kwetu na matunda ndio haya tunayaona.

Nina imani Chadema hawawezi hata kidogo kuleta mabadiliko huku Bara peke yao bila kushirikiana na wenzao wa upi.nzani.

Chadema kidole kimoja hakivunji chawa. Unganeni mlete mabadiliko ya kweli.
CCM yako iliwahi kuungana na nani bara? mbona mnajifanya mmeleta tija? Naamini katika kuungana lakini siamini katika kuungana na kila chama. Kuungana kwatakiwa kuwe na uangalifu sana. Kama cuf wamefanya uangalifu huo ngoja tusubiri hizo tija. Lakini nawasihi Chadema kuwa waangalifu sana.
mwisho nakupa angalizo kwamba hapa huyu ndugu yetu kaleta mchango wa maana ambao tunasubiri walioulizwa waje na majibu na tusingetegemea pumba zako katika issues za taifa. Hatujadili mambo ya dini hapa. Wewe unadhani dini yako imesaidia nini katika nchi yetu maskini ya mwisho kwenye karne hii? badilika kichwani kwa kuweka ubongo badala ya uji.
 
Na wewe nijibu maswali haya:

1. Cuf wameunda "serikali ya umoja wa kitaifa" kwa kushirikiana na ccm huko zanzibar, je wameshirikisha vyama vingine zaidi ya wao na ccm? Au ndio vyama pekee vilivyoko huko? Na kama hawajashirikisha, ni kwa nini? Utasema katiba. Je wakati inaundwa/kufanyiwa marekebisho hiyo katiba hawakujua kuwa kuna vyama vingine vya siasa ambavyo vinastahili kuwepo kwenye "serikali ya umoja wa kitaifa"?

CUF wameingia kwenye Serikali ya umoja wa kitaifa baada ya wananchi kupiga kura na kuridhia marekebisho ya katiba kuwa vyama vitavyopata uwakilishi vitaingia kwenye serikali ya umoja wa kitaifa katiba inasema vyama vitakavyokuwa na uwakilishi haisemi CCM na CUF pekee ndio watakakuwa na uwakilishi kwahiyo ni jukumu la vyama vingine kama NCCR, UDP, PPT, DP, CMD na vinginevyo vijipenyeze Zanzibar na kuweza kuupata huo uwakilishi kwenye baraza la wawakilishi.

2. Kwenye chaguzi za spika, naibu spika, wabunge wa east africa na sadc; cuf kwa makusudi mazima walishirikiana na kuchaguana na ccm tena kwa mapatano eti nafasi hii mpeni huyu wa ccm na ile mpeni yule wa cuf. Hakuna mbunge hata mmoja wa cuf aliyepigia kura chadema kwenye chaguzi hizo alkadhalika kwenye chaguzi za mameya, hapakuwa na ushirikiano hapo. Je itawezekanaje cuf hao hao sasa washirikiane na chadema ambao mwanzo waliona hawafai (na ni watu wale wale), waliwatuhumu na kuwabeza na bado wanaendelea kuwabeza?

Mimi sipo pamoja na CUF kwa hayo waliyoyafanya na walikosea kwani waliwavunja mioyo wenzao wa upinzani hususan CDM, lakini sikubaliani na hoja za kuto washirikisha wapinzani wengine na sio lazima CUF waungane na CDM basi hao waliobakia yaani NCCR na UDP waingie kwenye Kambi ya Upinzani Bungeni "KUB" Lakini uchaguzi umeshaisha nadhani ingekuwa ni jambo la busara hawa watu yaani CDM,UDP,NCCR na CUF kuangalia mbele wakae waelezane wapi walipokosea na wawe na strategy ya ku move forward na sio kuangalia yaliyopita.


3. Kwa kutowashirikisha cuf au vyama vingine vya upinzani, chadema inavunja sheria/kanuni gani?

Hakuna sheria wala kanuni inayovunjwa ila watu waliopo kwenye upinzani wangefurahia vyama vya upinzani viwe na umoja ili kuweza kuwa na nguvu ya kukabiliana na CCM

4. Kama hawatakuwa kwenye hiyo kambi, wabunge wa cuf au vyama vingine vya upinzani hawataweza kutekeleza yale waliyowaahidi wapiga kura wao? Je wakati wanaomba kura waliweka sharti la kutekeleza ahadi zao kupitia "KUB"?

Jibu ni sawa na hilo hapo juu
.

Nina maswali mengi lakini kwanza nijibu hayo machache kabla sijaongeza mengine.

Ndimi, Mkeshaji
Nikiwa safarini kuelekea hapahapa.

Nimeona nikujibu chini ya maswali yako na kuyaweka bold nahisi itakuwa nimekutendea haki kwa kujibu kila swali.

Shukran.
 
I cant believe u if ur a Tanganyika guy kwa sababu ya maswali yako ya kutaka kuchokonoa chokonoa

Mimi huwa najiuliza mambo mengi tu sichukulii siasa kama wimbo wao waimbe mie nikariri kiitikio. Nina penda ku reason out nchi zote zilizoendelea watu hawakariri wasemayo viongozi kila neno likizungumzwa wanalipima kwanza hawalichukulii kama neno la Mungu.
 
Mohammedi Shossi,

Hongera mkuu,nina imani kuwa unao Moyo wa kizalendo wa kujenga Tanzania yenye nguvu Africa na duniani.

Hata hivyo nikujibu swali lako la pili kwa kifupi tu,CHADEMA Ina wafuasi Zanzibar,wangepata wabunge kupitia CHADEMA lazima wangewakuwa sehemu ya kambi ya Upinzani.Lakini kusema kuwa kwa kuwa ati hawana Mbunge Zanzibar,basi iwe heri kwa CUF kupitia mgongo wa CHADEMA,huo ni ufisadi,uvivu,kupoteza dira na kukosa msimamo wa kiitikadi!nikomee hapo kwa sasa.

Shukran mkuu,

Hapo kwenye nyekundu unaamanisha TLP, UDP na Chadema walifanya ufisadi kuingizwa kwenye kambi ya upinzani 2005 - 2010 wakati CUF ilikuwa na uwezo wa kuunda peke yao? au sijaelewa? Tafadhali nifahamishe.
 
Maswali yako ni muhimu na yanahitaji majibu kwani binafsi naamini kuna makosa yamefanyika katika reasoning ya kukataa ushirikiano lakini vilevile katika kukwepa practicality ya kushirikiana.
 
Back
Top Bottom