Swali la kizushi: Intelijensia haijafanya kazi Zanzibar?

Status
Not open for further replies.
Nadhani watu wengi akiwemo mwanakijiji bado awajatambua ukweli na chimbuko la matatizo na kuwa lawama zinaenda kwa wasiostahili.

Tatizo linalotokea sasa ni kosa lililopitishwa na bunge letu mwaka 1992 baada ya kupitisha mswada wa TISS act 1992 ambayo iligeuza usalama wa taifa toka chombo cha utendaji na kuwa chombo cha ushauri. kabla ya hapo usalama wa taifa walihusika moja kwa moja katika kugundua na kuzuia jambo lolote lenye madhara kwa taifa lakini kwa sasa wao kazi yao ni kuchunguza na kutoa mapendekezo kwa serikali na si kazi yao kuona kwamba yamefanyiwa kazi au lah kwani wao si watendaji.

kwa sheria hii ya TISS act ya 1992 inamaanisha ata usalama wa taifa wakigundua kuna meli imebeba mabomu inakuja katika nchi yetu wao kazi yao si kuizuia bali ni kutoa taarifa ya ujio wa meli hiyo na kama vyombo husika vikishindwa kuizuia wao wataacha iingie na ata ilipue taifa letu kwani ni nje ya kazi yao.

Godwine, Mwanakijiji ametumia neno 'overhaul' meaning unajenga upya - kama ni sheria, mabati, ukuta, zege whatever.... overhaul. Kwa hiyo kama tatizo ni sheria basi exercise ya overhaul ndiyo itamaliza.
 
Last edited by a moderator:
After so many missteps and a myriad of events that expose the incompetence and mediocrty of our intelligence service isn't this the time to call for major overhaul of TISS? the changes that will include the removal of RO and his deputies?

Mwanakijiji huwa na mawazo mazuri sana as far as I know, what I don't understand ni nini kimempata kuanzisha topic inayohusu secret societies za jamii yetu ambazo kwa mujibu wa utendaji wao hawawezi kujitetea, unanafasi ya kutoa criticism zako bila kuwa challenged na wahusika. To me that looks VERY UNFAIR judgment for an educated child of this land.
Haitusaidii sana sisi wananchi kupata habari ya upande mmoja, If I were you I would focus on constitutional weaknesses that makes this important institution seem not to deliver to our expectations. There are constitutional WEAKNESSES MWANAKIJIJI KNOWS About that but he pretends not to know !! Too sad My friend, you and me can help these guys build a better Tanzania of Today and Tommorrow unless you have a hidden Agenda!
 
Mwanakijiji huwa na mawazo mazuri sana as far as I know, what I don't understand ni nini kimempata kuanzisha topic inayohusu secret societies za jamii yetu ambazo kwa mujibu wa utendaji wao hawawezi kujitetea, unanafasi ya kutoa criticism zako bila kuwa challenged na wahusika. To me that looks VERY UNFAIR judgment for an educated child of this land.
Haitusaidii sana sisi wananchi kupata habari ya upande mmoja, If I were you I would focus on constitutional weaknesses that makes this important institution seem not to deliver to our expectations. There are constitutional WEAKNESSES MWANAKIJIJI KNOWS About that but he pretends not to know !! Too sad My friend, you and me can help these guys build a better Tanzania of Today and Tommorrow unless you have a hidden Agenda!

Good post!!!!! Like like like like!!!
 
Vurugu za Zanzibar zilitabirika na nafikiri vyombo vya usalama vilikuwa na nafasi kubwa ya kuzuia machafuko hayo. Mimi nina wasiwasi kuwa labda vyombo hivi vilitaka yaliyotokea yatokee labda ndo maana wakaamua kutofanya kitu kuzuia funjo au walifanya hivyo kulinda maslahi ya watu wachache au vikundi vya watu.

Wakati tukiwa wadogo, usalama wa taifa wa nchi yetu ulisifiwa sana duniani kote maana walijulikana kwa utendaji kazi wao mzuri. Watu walikuwa wanaogopa kuropoka vitu hovyo hovyo kwa kuhofia wa usalama wa taifa wangesikia na labda kukutia mbaroni. Wengi wao hatukuwajua, tulikuwa tukisikia tetesi kuwa fulani anafanya kazi usalama n.k

Lakini siku hizi wanajitambulisha baa, wanaonesha bastola zao waziwazi, kutoa vitisho hadharani n.k. Siku hizi mtu anajua fulani ni usalama jambo ambalo mimi binafsi nafikiri ni hatari kwa taifa.

Tatizo la Zanzibar nafikiri limesababishwa na wanasiasa wanaotaka ku-serve interests zao zisizofahamika.

Watu wengi wanawaulumu baadhi ya viongozi wa CUF hasa Ismail Jussa kuwa wamechangia kutokea kwa matatizo haya.
Sina ushahidi na tuhuma hizi lakini kauli ya Jussa mwezi wa pili kuwa CUF walipoteza jimbo la Uzini kutokana na kuongezeka kwa wakristo wengi na makanisa mengi si kauli iliyotakiwa kutolewa na kiongozi wa kitaifa kama yeye.

Pia CUF si chama cha waislamu wala wakristo bali ni chama cha watanzania wote.
Kama damu ikimwagika Zanzibar na uvunjifu wa amani zaidi kutokea, nafikiri viongozi kama hawa ni lazima wawajibishwe. Ocampo aandae majalada ya mashitaka yao kabisa.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom