Swali la Hoja: Wabaguzi ni Wazanzibari au Watanganyika...?

Status
Not open for further replies.
Ukiangalia ushahidi wote uliopo utaona kuwa wenye hisia za kujitenga na kujiweka kiupekee ni watu wa Zanzibar siyo watu wa Tanganyika. Karibu mambo yote ya kujibagua wamefanya wao... si kweli?

Wao wanasema "nchi yao" tukisema "nchi yao" wanasema tunawabagua?

Hapo kwa RED ni tabia ya mtoto "aliyedekezwa"
 
Muungano umekosewa, ilitakiwa uwe muundo wa serikali moja. serikali mbili hazitekelezeki hasa kwa taifa masikini kama letu. serikali mbili haziashirii uniform bali zinaashiria 'semi' half uniform and half different.

ukiwa na muungano huu ambao kuna mambo ya muungano na yale yasiyo na muungano.cha kwanza kujiuliza ni Je kwa yale yasiyo ya muungano huyu aliye jiondoa power/sovereght atayaendesha vipi? Je raia watakuwa wamoja. mfano znz wanayo mahakama ya kadhi huko bara hakuna maana yake ukitoka dodoma kwenda znz unaenda sehemu yenye sheria zake na mfumo wa mahakama tofauti kabisa.elimu ya msingi znz inaishia kidato cha pili huku bara inaishia lasaba hapo utaona hii sio nchi moja kiutawala wala kwa raia wenyewe.

MUUNGANO UMEKOSEWA. serikali moja ya ingeanza mwanzo ingekuwa nzuri, hata serikali 3 za warioba nazo ni nzuri maana zinaondoa kero nyingi hasa ukiangalia haki za raia zilizoainishwa.
 
kwa hiyo muundo wa muungano ndio unawafanya wazanzibar kuwa wabaguzi. wakijaribu kulinda kile chao kwa ajili ya kuongeza ufanisi kwa yale yasiyo ya muungano. ndio maana unasikia serikali ya znz inawalipa kidogo watu wa znz. ukiwa na degree mshahara unaanzia laki na nusu. katika mazingira hayo sidhani kama utaona viongozi wakichekeana. znz igekuwa kanda au jimbo au jiji na ihudumiwe na serikali ya tz ndio hali ingekuwa sawa huku raia wakiruhusiwa kuishi popote.
 
ukiangalia mfano south afrika ingekuwa inaendeleza serikali za maeneo ambayo yameungana tangu mwanzo kuna uwezekano mkubwa kelele za kujitenga zingekuwa kubwa sana na cape town wangetumia kila wawezalo wajitenge.Lakini kwa kuwa ni nchi moja na serikali moja. hilo halipo na sio rahisi.
 
Nashukuru umeandika kifupi sana!!!!!
Sababu majibu na matakwa yao yako wazi sana na humu watakuja na kwa sababu ni tabia yao basi itaonekana tu!!!!!!

Tujipe muda kidogo!!!!!!!!!!
 
Wagaguzi ni serikali 2 wanazong'ang'ania CCM na Tanganyika kuvaa koti la muungano.
 
Tanganyika haijawahi kuchangia gharama za Muungano.......kwani haipo na haina akaunti........sasa Zanzibar wamechoka kubeba Gharama za Muungano wenyewe ....

Tanganyika iwepo ili iweze kuchangia .........ubaguzi utaisha........
 
naweashauri ukifika mjadala wa wizara zisizo za muungano watoke nje, itaonyesha ukomavu wa kisiasa.
 
Tanganyika haijawahi kuchangia gharama za Muungano.......kwani haipo na haina akaunti........sasa Zanzibar wamechoka kubeba Gharama za Muungano wenyewe ....

Tanganyika iwepo ili iweze kuchangia .........ubaguzi utaisha........
Naam.
Ndiyo maana ninakubaliana na aliyesema kuwa Ally Keissy amewasaidia (amewarahisishia kazi) Wazanzibar.

Wazanzibar wanatakiwa sasa washikilie hapo kuwa Tanganyika haichangii kitu kwenye muungano.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom