Swali kwa wote

JS

JF-Expert Member
Sep 29, 2009
2,064
499
Wana JF za asubuhi/mchana/jioni!!!! Nimekuwa nikifuatilia ile hadithi ya Mwanakijiji ya Kisa cha Mjamaika ina mambo mengi visa mbalimbali vya kimapenzi. Sasa hadithi hiyo imenifanya nipate swali: Hivi suala la kunyimwa haki ya mwili (Unyumba) linakuaje?? na wanaume nao mnatoa adhabu hiyo kwa wasichana/wake zenu wanapowakosea au wanapowaudhi??? Maana inaonekana wanawake wanatumia zaidi hiyo kama silaha yao (sina uhakika wa statistics lakini hata kwenye mahusiano ya kawaida tu inatokeaga)

Clementina kamnyima Waziri unyumba kwa miezi 7/8 hivi na mnalala kitanda kimoja mnaamka wote mnaonana kila kitu lakini ndo hivyo miezi 7 Waziri hakuona ndani. Imenishtusha kidogo hali hii.
 
Wana JF za asubuhi/mchana/jioni!!!! Nimekuwa nikifuatilia ile hadithi ya Mwanakijiji ya Kisa cha Mjamaika ina mambo mengi visa mbalimbali vya kimapenzi. Sasa hadithi hiyo imenifanya nipate swali: Hivi suala la kunyimwa haki ya mwili (Unyumba) linakuaje?? na wanaume nao mnatoa adhabu hiyo kwa wasichana/wake zenu wanapowakosea au wanapowaudhi??? Maana inaonekana wanawake wanatumia zaidi hiyo kama kinga hiyo (sina uhakika wa statistics lakini hata kwenye mahusiano ya kawaida tu inatokeaga)

Clementina kamnyima Waziri unyumba kwa miezi 7/8 hivi na mnalala kitanda kimoja mnaamka wote mnaonana kila kitu lakini ndo hivyo miezi 7 Waziri hakuona ndani. Imenishtusha kidogo hali hii.

Swali lako zuri JS.

hapo kwenye nyekundu hapo mh..... kuna wengine analala na jeans, na akiamka anaingia bafuni kuoga akitoka keshavaa kila kitu anarudi chumbani kupaka tu mafuta na kuchana nywele ..unawezakta wiki hujaona hata rangi ya mgongo wake. Chezea yeye wewe.

Unajua sometimes huwa inakera mdogo wangu unadhani ni mara zote watu wanabania? sometimes inabidi maana unakuta mtu kakukosea umemwambia au kumlalamikia but bado hajirekebishi wala kuomba msamaha ukiamua kukasirika habembelezi. so unajenga kigruti ndani ya moyo.................sasa usiku anakuja kweli utakuwa na moyo wa kutoa?? ndio hapo waambiwa umemnyima.

Ila kwa kesi ya Mke wa Waziri mimi nafikiri ni tofauti- maana waziri ameonyesha kuwa mkewe hamfai- yaani hakitaki tena kitumbua chake ndo mana akaenda kwa binti Rehema------ hata ingekuwa mie nadhani ningebana bwana ah.
 
Unajua JS hata tamu ukinai ..na moyo ukishafedheheka na kuondoa amani..kila kitu kinakuwa ni kazi bure
Unaweza kumchukia mtu kwa matendo yake ,usmitamani hata kidogo akikugusa unaona kama adhabu .
Moyo ukikinai hata iweje ni ngumu kuurudisha..
Kwa miezi saba ya Clementina ni too much hiyo ndoa ilikuwa inaelekea kuvunjika..
Me bado ku- experience hiyo problem na siombei kabisa
 
mie nambaniaga japo wiki, kuna vijimambo akinifanyia hapo lazima nimbanie, akija late kanikuta nimeshalala hapo hakifanyiki kitu, na kesho yake maelezo yake yakipinda ya huko alikokuwa mbano unaendelea, kuna vijimambo mambo akivifanya anajua kabisa hapa hakuliki...hiyo miezi 7 kwa kweli ni mingi ila inategemeana na ishu yenyewe ilivyo.
 
mie nambaniaga japo wiki, kuna vijimambo akinifanyia hapo lazima nimbanie, akija late kanikuta nimeshalala hapo hakifanyiki kitu, na kesho yake maelezo yake yakipinda ya huko alikokuwa mbano unaendelea, kuna vijimambo mambo akivifanya anajua kabisa hapa hakuliki...hiyo miezi 7 kwa kweli ni mingi ila inategemeana na ishu yenyewe ilivyo.

Ha ha ha hapo hujambania mmepunzika japo wiki.
 
mie nambaniaga japo wiki, kuna vijimambo akinifanyia hapo lazima nimbanie, akija late kanikuta nimeshalala hapo hakifanyiki kitu, na kesho yake maelezo yake yakipinda ya huko alikokuwa mbano unaendelea, kuna vijimambo mambo akivifanya anajua kabisa hapa hakuliki...hiyo miezi 7 kwa kweli ni mingi ila inategemeana na ishu yenyewe ilivyo.

Ni kweli kabisa dada inategemea na ishu yenyewe ..........kusema ukweli Waziri alikosea na ile ban kwake ni naona ni sawa tu kwa sababu ninaamini angemkuta Mkewe na shamba boy ndani ya nyumba yao - ingekuwa habari nyingine. Unajua wenzetu hawa wamejaliwa kila kitu mwanaume anazo njia nyingi za kuadhibu
1. Kuna wanaopiga- mwanamke hawezimpiga mumewe kwa kumkosea (wengi wetu)
2. Anawezaamua kuchelewa kurudi nyumbani/ au kulala kabisa huko apendapo na akatoa sababu kuwa umemkosea .... na jamii ikamwelewa
3. Anawezaamua akaoa mwanamke mwingine bila kukupa talaka kwa kisingizio cha kukuadhibu na ikaeleweka
4. Anaweza akakuacha kabisa.

Hivyo vyote wanawake si rahisi kuvifanya na wakaeleweka katika jamii na hivyo kubakiwa na njia chache za kuadhibu pale anapokosewa na mwenzi wake ............na unfortunately hii ya ban ndio inaonekana kama inawork ----- ingawa wengi huwa hawajali kwa kuwa wana uwezo wa kupata nje....
 
Ha ha ha hapo hujambania mmepunzika japo wiki.


hamuwezi kupumzika wakati mwenzio anakuhitaji....ni mbano huo, anakuhitaji/humuhitaji kwa wakai huo mpaka anyooshe maelezo, mana nayo ukifanya wakati una mtima nyongo kwangu naona kaam adhabu vile.
 
Wana JF za asubuhi/mchana/jioni!!!! Nimekuwa nikifuatilia ile hadithi ya Mwanakijiji ya Kisa cha Mjamaika ina mambo mengi visa mbalimbali vya kimapenzi. Sasa hadithi hiyo imenifanya nipate swali: Hivi suala la kunyimwa haki ya mwili (Unyumba) linakuaje?? na wanaume nao mnatoa adhabu hiyo kwa wasichana/wake zenu wanapowakosea au wanapowaudhi??? Maana inaonekana wanawake wanatumia zaidi hiyo kama silaha yao (sina uhakika wa statistics lakini hata kwenye mahusiano ya kawaida tu inatokeaga)

Clementina kamnyima Waziri unyumba kwa miezi 7/8 hivi na mnalala kitanda kimoja mnaamka wote mnaonana kila kitu lakini ndo hivyo miezi 7 Waziri hakuona ndani. Imenishtusha kidogo hali hii.
labda ningeanzia kwako jeiesi na MAHUSIANO YAKO..............!
hii adhabu huwa unaitoa?????:drum:
 
Ni kweli kabisa dada inategemea na ishu yenyewe ..........kusema ukweli Waziri alikosea na ile ban kwake ni naona ni sawa tu kwa sababu ninaamini angemkuta Mkewe na shamba boy ndani ya nyumba yao - ingekuwa habari nyingine. Unajua wenzetu hawa wamejaliwa kila kitu mwanaume anazo njia nyingi za kuadhibu
1. Kuna wanaopiga- mwanamke hawezimpiga mumewe kwa kumkosea (wengi wetu)
2. Anawezaamua kuchelewa kurudi nyumbani/ au kulala kabisa huko apendapo na akatoa sababu kuwa umemkosea .... na jamii ikamwelewa
3. Anawezaamua akaoa mwanamke mwingine bila kukupa talaka kwa kisingizio cha kukuadhibu na ikaeleweka
4. Anaweza akakuacha kabisa.

Hivyo vyote wanawake si rahisi kuvifanya na wakaeleweka katika jamii na hivyo kubakiwa na njia chache za kuadhibu pale anapokosewa na mwenzi wake ............na unfortunately hii ya ban ndio inaonekana kama inawork ----- ingawa wengi huwa hawajali kwa kuwa wana uwezo wa kupata nje....

ya nje itabakia kuwa ya nje, na ukiona umembania na yeye hajali ujue hapo kuna walakini mwingine wa kukaa na kuuongelea kiundani, kuna zaidi ya tatizo hapo.
 
Wanawake bana eti unambania...Yaani hyo huwa haifanyi kazi hata kdogo kwangu maana ukijidai kubana mi pia naweza kusavaivu hata aka 2. Huwa nacheka tu nikisikia mwanamke eti amembania mumewe mademu wenyewe wako kwa mafungu mitaani.
 
Wanawake bana eti unambania...Yaani hyo huwa haifanyi kazi hata kdogo kwangu maana ukijidai kubana mi pia naweza kusavaivu hata aka 2. Huwa nacheka tu nikisikia mwanamke eti amembania mumewe mademu wenyewe wako kwa mafungu mitaani.

hiyo ni ya kwako, kuna baadhi ya wanaume japo wanajua wapo wa mafungu kama unavyowaita wewe lakini dhamani ya mke ipo pale pale, ataweka mambo nyumbani yaende sawa kama anafanya upuuzi wake wa nje ndio utakaofuata, wengine wanapenda tuwe na amani na wanajua tukiwa na amani na wao wanapata amani....
 
sababu kubwa sana ya kuwa na nyumba ndogo ni PAMOJA NA HII ya kubaniana.....................
 
mi akinibore sana hasa wa mambo ya infidelity lazima anyimwe hata miezi kadhaa!
 
Wanawake bana eti unambania...Yaani hyo huwa haifanyi kazi hata kdogo kwangu maana ukijidai kubana mi pia naweza kusavaivu hata aka 2. Huwa nacheka tu nikisikia mwanamke eti amembania mumewe mademu wenyewe wako kwa mafungu mitaani.
nenda mashariki magharibi na kaskazini ya ndani ni tamu tena ana uhakika nayo kuliko ya nje wa ulize uone
 
Wanawake bana eti unambania...Yaani hyo huwa haifanyi kazi hata kdogo kwangu maana ukijidai kubana mi pia naweza kusavaivu hata aka 2. Huwa nacheka tu nikisikia mwanamke eti amembania mumewe mademu wenyewe wako kwa mafungu mitaani.[/QUOTE]





hapo wameongelewa wana ndoa zaidi, sasa hiyo kwenye red inategemeana na umri na utashi wako kifikra juu ya kitu mke/mme
 
mie nambaniaga japo wiki, kuna vijimambo akinifanyia hapo lazima nimbanie, akija late kanikuta nimeshalala hapo hakifanyiki kitu, na kesho yake maelezo yake yakipinda ya huko alikokuwa mbano unaendelea, kuna vijimambo mambo akivifanya anajua kabisa hapa hakuliki...hiyo miezi 7 kwa kweli ni mingi ila inategemeana na ishu yenyewe ilivyo.
mie nikibaniwa wiki tu naenda Jolly Club kujipoza nikiona anaendelea kubana kama kawaida najenga kajumba, msitumie nyuchi kama silaha ya maangamizi kwa m/ume mie inaniboa sana hiyo kitu na ndio malalamiko ya w/ume wote mtaani mtu mmekorofishana mambo ya kawaida anakimbilia kukunyima unyumba hapo si unafungulia nyumba ndogo mwenyewe mmmh sijui lakini mna matatizo hapo
 
mie nambaniaga japo wiki, kuna vijimambo akinifanyia hapo lazima nimbanie, akija late kanikuta nimeshalala hapo hakifanyiki kitu, na kesho yake maelezo yake yakipinda ya huko alikokuwa mbano unaendelea, kuna vijimambo mambo akivifanya anajua kabisa hapa hakuliki...hiyo miezi 7 kwa kweli ni mingi ila inategemeana na ishu yenyewe ilivyo.

Unambania??!! it is good. Lakini kumbuka ikiwa kuna issue ni lazima muiongee na kusolve, kumbania is not a solution. Na katika kipindi unachobana akiamua kutoka nje na ukajua, ukajifanya kulalamika akasema ukweli kuwa umembania na alikuwa radhi kuzungumza kutatua tofauti zenu, jamii na hata rafiki zako watakuelewaje?
 
Mimi ningependa tu kuwauliza kina kaka mloisoma hadithi ya Mwanajamii opssssssssss Mwanakijiji. Je kama wewe ndie ungemfuma mkeo alilimwa na shamba boy kama Waziri alivyokuwa anafanya kwa housegirl. Na kama ungekuwa huna option ya kumwacha, kumpiga ungechukua uamuzi gani na hasira yako??
 
sababu kubwa sana ya kuwa na nyumba ndogo ni PAMOJA NA HII ya kubaniana.....................
True Shit....ukinibania tena kwa kiburi kabisa yaani umewasha moto na mie sikugusi mpk uniombe mwenyewe tena kipindi hicho nitakuwa narudi saa 6 daily na pia mpk uje kulegeza masharti ujue nyumba ndogo ishakamata ujauzito

kuna mzee mmoja alienda nje sasa aliporudi mkewe akapata habari kuwa kule alikuwa na m/mke mkenya yule mama akaamua kumnyima jamaa unyumba na walilala vyumba tofauti kama miaka miwili hivi yule mama alitegemea baada ya hapo jamaa angejirekebisha muda ukapita wakarudi kwenye mstari, kumbe kipindi kile jamaa alitafuta nyumba ndogo akazaa nayo mtoto mmoja ila mkewe hakujua mpk mtoto alipoanza form one ndio yule mama alimkuta mumewe Kariakoo anamfanyia shopping mwanae wanachagua magodoro na ile misanduku ya bati (ya boarding)
mama kuuliza huyu nani mzee akampasulia ukweli kuwa miaka ile ulivyohama chumba mm nilihamua kutafuta m/mke nikazaa nae mtoto. Yule mama alichanganyikiwa ingawa baadae mambo yalienda sawa ila nadhani alipata funzo na hasara za kulala vyumba tofauti na mumewe
 
mi akinibore sana hasa wa mambo ya infidelity lazima anyimwe hata miezi kadhaa!
ai wishi mke wangu angekuwa na akili kama zako......NINGEHAMIA TABATA-MAWENZI kwa nyumba ndogo yangu mtoto SALIMA....DAH!

mke wangu nikipiga infidelity ye ndo anaongeza manjonjo kwenye chakula cha usiku!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom