Swali kwa wataalamu wa sheria, katiba, vyama na siasa

Zakumi

JF-Expert Member
Sep 24, 2008
5,063
2,471
Nitaanza kwa utani tu. Katika nchi mmoja ya Ulaya watu wameruhusiwa kutembea na bangi lakini kwa matumizi ya binafsi (personal use). Hivyo kuna jamaa akahamua ku-import container nzima la bangi. Alipokamatwa na polisi, jamaa akajitetea kuwa ni kwa personal use, ingawaje ilikuwa ni ya biashara. Akaachiwa huru na sheria ikabidi ibadilishe hili kuonyesha kiwango gani mtu anaruhusiwa kubeba kwa personal use. Kwa mtaji huu kitu kisichoandikwa kisheria sio kosa.

Nikirudi kwenye mada: Najaribu kuisoma katiba ya serikali ya Tanzania na sioni sehemu inayosema kuwa ni lazima mgombeaji wa cheo cha kisiasa awe mwanachama wa chama kimoja tu cha siasa. Hivyo basi kwa mtaji huu, mtanzania anaweza kuwa mwanachama wa vyama vingi vya kisiasa na kugombea nafasi moja au nyingi kwa kutumia tiketi ya vyama vingi.

Kwa maoni yangu uanachama wa chama cha siasa is not mutually exclusive. 2015 ninaweza kugombea udiwani kwa kutumia uachama wa CUF na wakati huo huo kugombea ubunge kwa kupitia TLP na CHADEMA au CCM. Sheria ya nchi haikatazi mtu kushikilia udiwani na ubunge kwa wakati mmoja.

Naomba ufafanuzi wenu
 
dah, am not gud in LAW bt kwa mtazamo uliopo na sheria za UCHAGUZI, Mgombea yoyote anae taka kugombea nafasi iwe ya Ubunge, ama udiwani or katika serikari za mitaa (mwenyekiti wa mtaa). Sharti la kwanza ni lazima uwe mwana chama wa chama kinacho tambulika.

Na kwa mtazamo wako Tanzania hairuhusu mgombea au mwana chama wa chama chochote kuwa na udhamini/kadi ya chama zaidi ya kimoja. So bwana mkubwa hyo haipo, ningepata sheria ya vyama vya siasa toka kwa msajili wa vyama ningekusomea vifungu zaidi.
 
Nitaanza kwa utani tu. Katika nchi mmoja ya Ulaya watu wameruhusiwa kutembea na bangi lakini kwa matumizi ya binafsi (personal use). Hivyo kuna jamaa akahamua ku-import container nzima la bangi. Alipokamatwa na polisi, jamaa akajitetea kuwa ni kwa personal use, ingawaje ilikuwa ni ya biashara. Akaachiwa huru na sheria ikabidi ibadilishe hili kuonyesha kiwango gani mtu anaruhusiwa kubeba kwa personal use. Kwa mtaji huu kitu kisichoandikwa kisheria sio kosa.

Nikirudi kwenye mada: Najaribu kuisoma katiba ya serikali ya Tanzania na sioni sehemu inayosema kuwa ni lazima mgombeaji wa cheo cha kisiasa awe mwanachama wa chama kimoja tu cha siasa. Hivyo basi kwa mtaji huu, mtanzania anaweza kuwa mwanachama wa vyama vingi vya kisiasa na kugombea nafasi moja au nyingi kwa kutumia tiketi ya vyama vingi.

Kwa maoni yangu uanachama wa chama cha siasa is not mutually exclusive. 2015 ninaweza kugombea udiwani kwa kutumia uachama wa CUF na wakati huo huo kugombea ubunge kwa kupitia TLP na CHADEMA au CCM. Sheria ya nchi haikatazi mtu kushikilia udiwani na ubunge kwa wakati mmoja.

Naomba ufafanuzi wenu


This is where I tend to say no. Naomba ukarudie kusoma upya katiba ya jamhuri ya muungano wa kinafiki wa Tanzania.
 
Kwa maoni yangu uanachama wa chama cha siasa is not mutually exclusive. 2015 ninaweza kugombea udiwani kwa kutumia uachama wa CUF na wakati huo huo kugombea ubunge kwa kupitia TLP na CHADEMA au CCM. Sheria ya nchi haikatazi mtu kushikilia udiwani na ubunge kwa wakati mmoja.

Naomba ufafanuzi wenu

Kabla ya kutoa ufafanuzi, hivyo vyama vyenyewe vitakuelewa kwamba uvae shati yenye rangi nyekundu, kijani, bluu, njano, nyeupe, nk?
 
Nitaanza kwa utani tu. Katika nchi mmoja ya Ulaya watu wameruhusiwa kutembea na bangi lakini kwa matumizi ya binafsi (personal use). Hivyo kuna jamaa akahamua ku-import container nzima la bangi. Alipokamatwa na polisi, jamaa akajitetea kuwa ni kwa personal use, ingawaje ilikuwa ni ya biashara. Akaachiwa huru na sheria ikabidi ibadilishe hili kuonyesha kiwango gani mtu anaruhusiwa kubeba kwa personal use. Kwa mtaji huu kitu kisichoandikwa kisheria sio kosa.

Nikirudi kwenye mada: Najaribu kuisoma katiba ya serikali ya Tanzania na sioni sehemu inayosema kuwa ni lazima mgombeaji wa cheo cha kisiasa awe mwanachama wa chama kimoja tu cha siasa. Hivyo basi kwa mtaji huu, mtanzania anaweza kuwa mwanachama wa vyama vingi vya kisiasa na kugombea nafasi moja au nyingi kwa kutumia tiketi ya vyama vingi.

Kwa maoni yangu uanachama wa chama cha siasa is not mutually exclusive. 2015 ninaweza kugombea udiwani kwa kutumia uachama wa CUF na wakati huo huo kugombea ubunge kwa kupitia TLP na CHADEMA au CCM. Sheria ya nchi haikatazi mtu kushikilia udiwani na ubunge kwa wakati mmoja.

Naomba ufafanuzi wenu

Utata huu umeshajadiliwa katika kesi ya mgombea binafsi iliyofunguliwa na mtikila,hakuna chama ambacho kitaruhusu mwanachama wake awe na uanachama na chama kingine,huwezi kuwa mwanachama cuf ukiifuata katiba na itikadi ya cuf wakati huohuo uko chadema.Use common sense
 
dah, am not gud in LAW bt kwa mtazamo uliopo na sheria za UCHAGUZI, Mgombea yoyote anae taka kugombea nafasi iwe ya Ubunge, ama udiwani or katika serikari za mitaa (mwenyekiti wa mtaa). Sharti la kwanza ni lazima uwe mwana chama wa chama kinacho tambulika.

Na kwa mtazamo wako Tanzania hairuhusu mgombea au mwana chama wa chama chochote kuwa na udhamini/kadi ya chama zaidi ya kimoja. So bwana mkubwa hyo haipo, ningepata sheria ya vyama vya siasa toka kwa msajili wa vyama ningekusomea vifungu zaidi.

Real2Man:

Natafuta website ya msajili wa vyama vya siasa lakini sina mafanikio yoyote hivyo natumia katiba ya nchi. Na katiba ya nchi haijasema kuwa ni makosa kwa mtanzania kuwa mwanachama wa vyama vingi vya siasa.

Na kama katiba inavyonyesha chini, sifa ya mgombeaji wa ubunge, kwa mfano, anatikiwa kuwa mwanachama chama cha siasa na amependekezwa na chama cha siasa. Kipengere hiki hakisemi kuwa mgombeaji awe mwanachama wa chama cha siasa na apendekezwe na chama chake. Kwa mtaji huu mtu anaweza kuwa na mwanachama wa CUF lakini akapendekezwa kuwa mgombeaji wa CHADEMA.

67.-(1) Bila ya kuathiri masharti yaliyomo katika ibara hii, mtu yeyote atakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge endapo-
(a) ni raia wa Jamhuri ya Muungano aliyetimiza umri wa miaka ishirini na moja, na ambaye anajua kusoma na kuandika katika Kiswahili au Kiingereza;
(b) ni mwanachama na ni mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa;
(c) katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya Uchaguzi hakuwahi kutiwa hatiani katika mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali.
(2) Mtu hatakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge-
(a) ikiwa mtu huyo anao au kwa hiari yake amejipatia uraia wa nchi nyingine yote; au
(b) ikiwa kwa mujibu wa sheria inayotumika katika Jamhuri ya Muungano imethibitishwa rasmi kwamba mtu huyo ana ugonjwa wa akili; au
(c) ikiwa mtu huyo amehukumiwa na Mahakama yoyote katika Jamhuri ya Muungano na kupewa adhabu ya kifo au ya kufungwa gerezani kwa muda unaozidi miezi sita kwa kukutwa na hatia ya kosa lolote, vyovyote linavyoitwa, linaloambatana na utovu wa uaminifu; au
(d) ikiwa katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya Uchaguzi Mkuu amepata kuhukumiwa na kupewa adhabu ya kifungo kwa kosa linaloambatana na utovu wa uaminifu au kwa kuvunja sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma;
(e) bila ya kuingilia haki na uhuru wa mtu kuwa na maoniyake, kuamini dini atakayo, kushirikiana na wengine na kushiriki shughuli za umma kwa mujibu wa sheria za nchi, ikiwa mtu huyo si mwanachama na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa;
(f) ikiwa mtu huyo ana masilahi yoyote katika mkataba wa Serikali wa aina yoyote aliyowekewa miiko maalum kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge, na iwapo amekiuka miiko hiyo;
(g) ikiwa mtu huyo ameshika madaraka ya afisa mwandamizi katika utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano, isipokuwa madaraka ambayo Rais aweza au anatakiwa kukabidhi kwa Mbunge kwa mujibu wa Katiba hii au sheria iliyotungwa na Bunge;
(h) ikiwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoshughulikia makosa yanayohusika na uchaguziwa aina yoyote mtu huyo amezuiliwa kujiandikisha kama mpiga kura au kupiga kura katika uchaguzi waWabunge.
 
This is where I tend to say no. Naomba ukarudie kusoma upya katiba ya jamhuri ya muungano wa kinafiki wa Tanzania.

Mungi:

Katiba ya JMT hipo mbele yangu hapa. Hakuna hata sehemu moja inayosema ni makosa kwa mgombeaji wa uchaguzi or for that matter mtanzania kuwa mwanachama wa vyama vingi.

Hapa chini ni sifa za mgombeaji wa ubunge. Kipengere b kinasema mwanachama na apendekezwe na chama cha siasa. Kipengere hiki akijasema kuwa awe mwanachama wa chama kimoja cha siasa na apendekezwe na chama chake.

67.-(1) Bila ya kuathiri masharti yaliyomo katika ibara hii, mtu yeyote atakuwa na sifa za kustahili kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge endapo-
(a) ni raia wa Jamhuri ya Muungano aliyetimiza umri wa miaka ishirini na moja, na ambaye anajua kusoma na kuandika katika Kiswahili au Kiingereza;
(b) ni mwanachama na ni mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa;
(c) katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya Uchaguzi hakuwahi kutiwa hatiani katika mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali.
 
Utata huu umeshajadiliwa katika kesi ya mgombea binafsi iliyofunguliwa na mtikila,hakuna chama ambacho kitaruhusu mwanachama wake awe na uanachama na chama kingine,huwezi kuwa mwanachama cuf ukiifuata katiba na itikadi ya cuf wakati huohuo uko chadema.Use common sense

Mwaipaja:

As a matter of fact I use common sense. Kama mimi ni mwanachama wa kijani na mazingira naweza kuwa mwanachama wa chama cha maendeleo ya jamii. Political pluralism haikatazi mtu kuwa na itkadi zaidi ya moja.

kukubali yale yaliotolewa katika kesi ya Mtikila, ni kuwa receptive wakati political semantic indicates the opposite. Kuwa mwanachama wa vyama vingi sio kitu kigeni dunia. Chukua mfano wa South Africa. Joe Slovo, Chris Hani walikuwa ni wanachama wa South African communist Party na wakati huo huo ni wanachama wa ANC.
 
Unayo practical concern hata kama watu hawataki kuona. Kama kweli sheria inaishia kusema uwe mwanachama wa chama fulani basi kitu pekee cha kuzuia kugombea kwa tiketi mbili ni kama chama kingine kitakataa kukuidhinisha au chama chako kitafuta uanachama. Kama hili halijatokea basi nafikiri unaweza kugombea udiwani kwa tiketi ya CCM na ubunge kwa tiketi ya CUF!
 
Kuna Sheria ya vyama vyenyewe vya siasa nchini. Kwa mfano, ukiwa mwanachama wa CCM huwezi kuwa na uanachama wa chama chingine. Kwa hiyo, hata kama Katiba ya nchi inakuruhusu bado umevunja ktk ya CCM. Inabidi ujitoe kwenye CCM kwanza kabla ujaamua kugombea ktk chama chingine. Ninaamini vyama vingine vya upinzani vina sheria kama hiyo.
 
Kuna Sheria ya vyama vyenyewe vya siasa nchini. Kwa mfano, ukiwa mwanachama wa CCM huwezi kuwa na uanachama wa chama chingine. Kwa hiyo, hata kama Katiba ya nchi inakuruhusu bado umevunja ktk ya CCM. Inabidi ujitoe kwenye CCM kwanza kabla ujaamua kugombea ktk chama chingine. Ninaamini vyama vingine vya upinzani vina sheria kama hiyo.

Nimesoma kanuni za uanachama za CCM na CHADEMA. Zinakataza kuwa mwanachama wa vyama vingine. Lakini kama kuna vyama ambavyo havina vigezo hivyo, basi utata utakuwepo.
 
Unayo practical concern hata kama watu hawataki kuona. Kama kweli sheria inaishia kusema uwe mwanachama wa chama fulani basi kitu pekee cha kuzuia kugombea kwa tiketi mbili ni kama chama kingine kitakataa kukuidhinisha au chama chako kitafuta uanachama. Kama hili halijatokea basi nafikiri unaweza kugombea udiwani kwa tiketi ya CCM na ubunge kwa tiketi ya CUF!

The Dreamer:

Unaweza kuleta mabadiliko makubwa kwa kufanya explotation ya vipengere vya katiba na sheria. Mpaka sasa ni vyama vyenyewe vinavyozuia uanachama wa vyama vingine lakini sio katiba ya nchi.

Hivyo basi kama hakuna sheria ya nchi inayokataza uanachama wa vyama vingi, kuna uwezekano wa kuwa na vyama vitavyokubali dual membership.
 
Mwaipaja:

As a matter of fact I use common sense. Kama mimi ni mwanachama wa kijani na mazingira naweza kuwa mwanachama wa chama cha maendeleo ya jamii. Political pluralism haikatazi mtu kuwa na itkadi zaidi ya moja.

kukubali yale yaliotolewa katika kesi ya Mtikila, ni kuwa receptive wakati political semantic indicates the opposite. Kuwa mwanachama wa vyama vingi sio kitu kigeni dunia. Chukua mfano wa South Africa. Joe Slovo, Chris Hani walikuwa ni wanachama wa South African communist Party na wakati huo huo ni wanachama wa ANC.
Zakumi,
Tunazungumzia siasa ya tanzania na mfumo wake,ni vizuri ukafuatilia mambo ili kubaini ukweli.Katika kesi ya mtikila hakuna mahali popote ulipoondolewa utata wa suala unaloliuza.Katika kujivua na lawama mahakama ya rufaa iliisukumia hoja ya mgombea binafsi bungeni ambalo bado halijakaa kuijadili hoja hiyo.
Ni vema ikaeleweka kuwa katiba ya Tanzania ina viraka na utapiamlo wa kutisha,ilitungwa wakati wa mfumo wa chama kimoja na hii ndio sababu tunadai katiba mpya.
Kuhusu suala la mgombea kupitia vyama vingi ni vizuri ukaelewa kwamba vyama vinaweza kuungana na kusimamisha mgombea mmoja,hii inategemeana na makubaliano ya vyama.
Kuchanganya itikadi,falsafa na malengo ya vyama kwa hoja kuhitaji uwe mfuasi wa vyama vingi ni dalili nzuri ya kutokujua maana ya ufuasi na kukosa msimamo.Vyama au mtu anaweza kuwa rafiki wa chama hata kama kina itikadi na malengo tofauti lakini cha msingi lazima ujulikane upo upande gani.
Kukubali mtu mmoja kuwa mfuasi wa chama zaidi ya kimoja ni kukaribisha wanafiki na mamluki ndani ya vyama.Asante ndugu yangu
 
Zakumi,
Tunazungumzia siasa ya tanzania na mfumo wake,ni vizuri ukafuatilia mambo ili kubaini ukweli.Katika kesi ya mtikila hakuna mahali popote ulipoondolewa utata wa suala unaloliuza.Katika kujivua na lawama mahakama ya rufaa iliisukumia hoja ya mgombea binafsi bungeni ambalo bado halijakaa kuijadili hoja hiyo.
Ni vema ikaeleweka kuwa katiba ya Tanzania ina viraka na utapiamlo wa kutisha,ilitungwa wakati wa mfumo wa chama kimoja na hii ndio sababu tunadai katiba mpya.
Kuhusu suala la mgombea kupitia vyama vingi ni vizuri ukaelewa kwamba vyama vinaweza kuungana na kusimamisha mgombea mmoja,hii inategemeana na makubaliano ya vyama.
Kuchanganya itikadi,falsafa na malengo ya vyama kwa hoja kuhitaji uwe mfuasi wa vyama vingi ni dalili nzuri ya kutokujua maana ya ufuasi na kukosa msimamo.Vyama au mtu anaweza kuwa rafiki wa chama hata kama kina itikadi na malengo tofauti lakini cha msingi lazima ujulikane upo upande gani.
Kukubali mtu mmoja kuwa mfuasi wa chama zaidi ya kimoja ni kukaribisha wanafiki na mamluki ndani ya vyama.Asante ndugu yangu

Hujamuelewa au unakwepa swali ili ukwepe na jibu?
Yeye nadhani wasi wasi wake ni kuwa kama vyama kwa sababu moja au nyingine vikikubali kumsimamisha mgombea (ikimaanisha wote wameona hakuna tatizo) kwenye nafasi tofauti tofauti za ngazi za ugombea kwa vyama tofauti itakuwaje?
Usiishie tu kusema haiwezekani. Jiulize pia ikiwezekana itakuwaje? Kwa hili unahitaji kushughulisha kichwa sio kujibu juu juu tu. Kuna mantiki fulani katika swali lake!
 
Kabla ya kutoa ufafanuzi, hivyo vyama vyenyewe vitakuelewa kwamba uvae shati yenye rangi nyekundu, kijani, bluu, njano, nyeupe, nk?

Buchanan:

Kimiundo na kiutandaji, vyama vya siasa vya Tanzania vinafuata muundo wa CCM na havina Itikadi ambavyo vinaweza kufanya mwanachama kuwa mwanachama wa zaidi ya chama kimoja.

Nimetoa mfano kuwa kama kutakuwepo na chama cha kijani (Green Party) basi mwanachama wa chama hiki anaweza kuwa mwanachama CHADEMA, CUF au CCM. Hii ni kwa sababu itikadi ya Green Parties ni kulinda na kuboresha mazingira. Itikadi ya Mazingira inaweza kuishi katika zizi moja na itikadi ya kijamaa bila kuingiliana kimaslahi.

Vilevile katika kambi za kijamaa kuna wasoshalisti na wakomunisti, mtu anaweza kuwa mwanachama wa wasoshalisti na vilevile wakomunisti. Hivyo kuwa na dual membership ni kitu kinachowezekana na kinafanyika.
 
Hii ni observation nzuri sana. Sijui kama pia sheria inazuia mtu mmoja kugombea kiti kimoja mara mbili kwa kutumia vyama viwili tofauti.

I have no idea
 
Zakumi,
Tunazungumzia siasa ya tanzania na mfumo wake,ni vizuri ukafuatilia mambo ili kubaini ukweli.Katika kesi ya mtikila hakuna mahali popote ulipoondolewa utata wa suala unaloliuza.Katika kujivua na lawama mahakama ya rufaa iliisukumia hoja ya mgombea binafsi bungeni ambalo bado halijakaa kuijadili hoja hiyo.
Ni vema ikaeleweka kuwa katiba ya Tanzania ina viraka na utapiamlo wa kutisha,ilitungwa wakati wa mfumo wa chama kimoja na hii ndio sababu tunadai katiba mpya.
Kuhusu suala la mgombea kupitia vyama vingi ni vizuri ukaelewa kwamba vyama vinaweza kuungana na kusimamisha mgombea mmoja,hii inategemeana na makubaliano ya vyama.
Kuchanganya itikadi,falsafa na malengo ya vyama kwa hoja kuhitaji uwe mfuasi wa vyama vingi ni dalili nzuri ya kutokujua maana ya ufuasi na kukosa msimamo.Vyama au mtu anaweza kuwa rafiki wa chama hata kama kina itikadi na malengo tofauti lakini cha msingi lazima ujulikane upo upande gani.
Kukubali mtu mmoja kuwa mfuasi wa chama zaidi ya kimoja ni kukaribisha wanafiki na mamluki ndani ya vyama.Asante ndugu yangu

Mwaipaja:

Kabla ya kuendelea ni lazima tuweke sawa mambo ya itikadi na falsafa. Uwezi kuwa na Itkadi ya kisiasa mpaka uwe na political spectrum. Na huwezi kuwa na political spectrum bila kuwa na interest groups zinazo-define spectrum yenyewe. Those interest groups should be real and genuine.

Vyama vya siasa vya Tanzania vinashindana katika mambo ya ethics: wewe fisadi, mimi sio fisadi, wewe fisadi, mimi sio fisadi. Ethics and Political Spectrum ni vitu viwil tofauti. Kwa hiyo ukiondoa ufisadi na maslahi ya viongozi wa vyama vya siasa, mtanzania anaweza kuwa mwanachama wa TLP na CCM bila kuwa mamluki. Kama TLP ni Tanzania Labour Party na CCM ni chama cha wakulima na wafanyakazi, what is the difference? Nothing. Vyote ni vya mkondo wa kushoto.

Tukirudi kwenye katiba ni kweli katiba ilikuwa ni ya chama kimoja. Hivyo kasoro nyingi zipo. Pili kuna ndoto kuwa hili tuwe na demokrasia ya kweli ni lazima tuwe na vyama vikubwa viwili kama vile Marekani. Hivyo katiba ya sasa inatumika kulazimisha two party system kama ilivyo Marekani.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom