Swali kwa Wanawake wa kileo: Nini kilichowatoa majumbani na kuanza kuingia mitaani na maofisini kutafuta hela?

Kisai

JF-Expert Member
Apr 6, 2018
27,982
28,100
Masikio yameumbiwa kusikia, moyo kutafakari na kuamua, akili kung'amua na kutambua lipi baya na lipi zuri, nafsi ndiyo wewe na mimi, ila Roho ndiyo uhai sasa, vinne hivi vipo ndani yetu, yaani kwenye miili yetu na ndiyo mimi na wewe sasa.

Wanawake wa leo ujuaji umewaponza sana na mbeleni mwao ni giza totoro,wengi wao hawalijui hili isipokuwa wachache walio rehemewa, huku wakisahau ya kuwa kila jambo lina chanzo na historia imeaandika.

Nikawa najiuliza hivi, hili kweli wanawake wa leo ambao wamewezeshwa hawalioni ? Mbona wanayo yadai ni madogo sana kuliko matokeo ya kile wanachokidai ? Leo mwanamke amefanywa kama bidhaa, lakini wao muda huo huo wakijinadi ya kuwa wamewezeshwa na wametolewa gizani, na huku wakijinadi ya kuwa zama zimebadilika ? Sasa mbona wao ndiyo wako gizani zaidi kuliko zama zote ? Hivi leo hii hakuna upuuzi wowote unaofanyika isipokuwa mwanamke amewekwa kama chambo, mwanamke amekuwa mtu wa kuvutia bisashara,wanawake wa kileo heshima kwao si lolote. Mwanamke gani aliwahi kutoka na kulikemea hili na kuzilinda heshima zao na thamani zao ? Wao wamefundishwa ya kuwa adui yako namba moja duniani ni Mwanaume na lazima ushindane nae, na uhakikishe unamshinda (Huwa nacheka sana).

Nikaja kuhitimisha ya kuwa Wanawake wa leo yule aliyewatoa majumbani aliwaficha lengo la kwanini aliwatoa majumbani na kuwaleta mtaani kwa jina zuri la "HAKI" ila ukweli ni kuwadhalilisha. Lakini alifanikiwa sana kwa kondoo kumvisha sanamu la Ng'ombe na kisha wenyewe wakaambiana yule ni Ng'ombe na siyo kondoo, huoni pua ile, huoni pembe zile ? Yaani akawa anaona mambo mazuri mazuri tu,kuwa na mahela, kumiliki mali na mfano wake.

Nina mengi ya kuandika, ila nakumbuka maneno mazuri yaliyotoka kwenye kinywa Twahara yasemayo "Bora ya maneno ni maneno machache na yenye faida".

Nahitimisha kwa nukuu maridhawa ya Will Durant, mwanafalsafa anayejulikana vyema, na mwandishi wa kitabu kiitwacho ‘History of Civilization’ anasema, “Tukijaalia kuwa tunaishi katika mwaka wa 2000 A.D na tunataka kujua tukio lililokuwa muhimu kabisa katika robo ya kwanza ya karne ya 20, tutaona kuwa haikuwa vita ya kwanza ya Dunia wala Mapinduzi ya Urusi. Lilikuwa ni badiliko la nafasi ya mwanamke. Historia haikuwahi kushuhudia badiliko la kusisimua kiasi hicho ndani ya muda mfupi kiasi hicho. Nyumbani, ambapo ndio ulikuwa msingi wa kiuendeshaji wetu wa kijamii, mfumo wa unyumba (ndoa), ambao ulizuia ufisadi na zinaa na kuleta utengamano wa maisha ya familia, na sheria madhubuti ya maadili iliyotusaidia kuondoka katika ushenzi kwenda katika utamaduni na tabia inayokubalika ya kijamii, yote haya yalisukumiziwa mbali na badiliko hili la kimapinduzi.”

Angalizo

1. Wanawake wa humu wana rauka sana kama wametoka usingizini, ombi langu mkija katika huu uzi mje na hoja za kielimu na sisi kutuonyesha uanamke wenu na kutia kwenu huruma. Bali mje na hoja za kielimu na mtuambie ilikuwaje mpaka mkatolewa majumbini na kuingia mtaani.

2. Siyo lazima tufikie muafaka sababu muafaka si lengo katika mijadala ya kielimu, bali lengo ni kuuweka wazi ukweli, bila kuangalia nani atachukia wala nani atalaumu.

3. Lazima tuheshimiane na tusivunjiane heshima. Hapa ni hoja kwa hoja.

4. Wanawake mkiulizwa maswali mjibu siyo mnakimbia.

5. Nachukua fursa hii kuwaita wanawake wote humu, huku nikiwaambia ya kuwa "Huu uzi ni wenu, karibuni mjimwaye mwaye" ila mje na hoja kama nyinyi ni wa kweli. Kwa uchache naomba ni waite kadhaa : Rowin cariha Paula Paul SIERA

Ni mimi kijana mtiifu Zurri
 
Mada imekaa kimashambulizi sana. Why explain anything wkt tyr uko biased kimtizamo?
Hakuna shambulizi hapo, nimeandika kile ambacho tunakiona na tunaishi nacho, kwani ni uongo bibie hamfanywi kaa bidhaa?

Kwani ni uongo huko kwenye semina zenu na makangomano hamuambiwi na kujazwa upepo ya kuwa sisi ndiyo maadui zenu na msiwe chini yetu?

Kwani ni uongo ya kuwa hakuna upuuzi ambao mbele ya upuuzi huo amewekwa mwanamke kama kivutio? Hili sijawahi kusikia mkilisema kwani kina athari hasi sana kwenu, na linawavunjia heshima pakubwa mno.
 
Hakuna shambulizi hapo bibie,nimeandika kile ambacho tunakiaona na tunaishi nacho, kwani ni uongo bibie hamfanywi kaa bidhaa?

Kwani ni uongo huko kwenye semina zeno na makangomano hamuambiwi na kujazwa upepo ya kuwa sisi ndiyo maadui zenu na msiwe chini yetu?

Kwani ni uongo ya kuwa hakuna upuuzi ambao mbele ya upuuzi huo amewekwa mwanamke kama kivutio ? Hili sijawahi kusikia mkilisema kwani kina athari hasi sana kwenu, na linawavunjia heshima pakubwa mno.
Eti bidhaa duhh😅
Wanauzwa wapi hao haha?.wanawake wote wako hivyo?

Ushaenda hizo kongamano?

Una wasiwasi gani km wanawake ndio wanapata athari?.si uwaache wahangaike wenyewe
 
Eti bidhaa duhh😅
Wanauzwa wapi hao haha?.wanawake wote wako hivyo?
Sehemu za biashara bibie.
ushaenda hizo kongamano?
Huwa habari zinatufikia. Kama ni uongo nibainishie tu kwamba ni uongi, hakuna kuminyana bibie.
una wasiwasi gani km wanawake ndio wanapata athari?.si uwaache wahangaike wenyewe
Haoana akili iliyo salama inalikataa hili, tumeumbiwa huruma sisi, halafu nyinyi ndiyo dada zetu, wadogo zetu, wake zetu na mama zetu pia, nafasi yenu kwetu ni kubwa mno na umuhimu wenu kwenye jamii hauna mfano, kwahiyo lazima tuwazindue.

Si huwa mnatuambia "Ukimuelimisha mwanamke mmoja ni sawa na umeelimisha jamii nzima". Sasa embu chukulia ukimuelimisha mwanamke mmoja elimu iliyo sahihi na akawa na msimamo huoni kama tunakuwa tumepiga hatua kubwa sana katika kuijenga jamii imara ?
 
Sehemu za biashara bibie.

Huwa habari zinatufikia. Kama ni uongo nibainishie tu kwamba ni uongi, hakuna kuminyana bibie.

Haoana akili iliyo salama inalikataa hili, tumeumbiwa huruma sisi, halafu nyinyi ndiyo dada zetu, wadogo zetu, wake zetu na mama zetu pia, nafasi yenu kwetu ni kubwa mno na umuhimu wenu kwenye jamii hauna mfano, kwahiyo lazima tuwazindue. Si huwa mnatuambia "Ukimuelimisha mwanamke mmoja ni sawa na umeelimisha jamii nzima". Sasa embu chukulia ukimuelimisha mwanamke mmoja elimu iliyo sahihi na akawa na msimamo huoni kama tunakuwa tumepiga hatua kubwa sana katika kuijenga jamii imara ?
Kwanini unahisi wanawake wote wamepotoka? Au umeandika sehemu baadhi?
 
Hivi kwanini uumizwe na Mambo ya wanawake, dunia imechange you have to accept it mengine wewe Kama mwanaume huwezi kuelewa mpaka uwe mwanamke, usiwe Kama wasaudia wanaume wazima Wana discuss Mambo ya hedhi ya wanawake bila wanawake wenyewe kuwepo na kuelezea Mambo yao ya hedhi.

In short wanaume insecure tuacheni wanawake na Mambo yetu nyie Nani wakutupangia mtukome kabisa.
 
Hakuna sehemu niliyo maanisha hivyo, soma vizuri utaona nini nimekusudia humo.
Anhaaa kwaiyo wanawake wenye wanajishughulisha na shughuli za kimaendeleo ikiwemo biashara pamoja na kujichanganya kijamii katika mishe zingine umewahesabu kama mfano wa kuigwa kwa wanawake wengine au ni wanawake wasiofaa kufatwa kulingana na vitu hivyo nilivyo vi-orodhesha?
 
Kwanini unahisi wanawake wote wamepotoka?
Au umeandika sehemu baadhi?.
Wapi nimeandika wote wamepotoka. Ndiyo maana nikatoa angalizo, umakini unatakiwa ili usikosee katika kujenga hoja au kujibu hoja. Naomba usome tena huko juu nilicho kiandika, samahani lakini mrembo.
 
Anhaaa kwaiyo wanawake wenye wanajishughulisha na shughuli za kimaendeleo ikiwemo biashara pamoja na kujichanganya kijamii katika mishe zingine umewahesabu kama mfano wa kuigwa kwa wanawake wengine au ni wanawake wasiofaa kufatwa kulingana na vitu hivyo nilivyo vi-orodhesha?
Soma nilichokiandika mzee, kinajieleza wazi, usiwe na haraka, hii mada nyepesi sana na nimeiandika kwa kuangalia hali za watu humu ndani.
 
Anhaaa kwaiyo wanawake wenye wanajishughulisha na shughuli za kimaendeleo ikiwemo biashara pamoja na kujichanganya kijamii katika mishe zingine umewahesabu kama mfano wa kuigwa kwa wanawake wengine au ni wanawake wasiofaa kufatwa kulingana na vitu hivyo nilivyo vi-orodhesha?
Mleta mada hapendi wanawake wafanye kazi na wanaofanya eti hawafai.
 
Hivi kwanini uumizwe na Mambo ya wanawake
Hivi unamuulizaje mwanaume swali hili, wakati kwa vyovyote wanawake wananihusu. Wanawake ndiyo wake zetu, watoto wetu, dada zetu na mfano wake.

Kwa nafasi adhimu ya mwanamke na majukumu, ni muhali mimi kutoumizwa kwa kuona anavyo chezewa na kuvunjiwa heshima yake, huku yeye mwenyewe akiona ya kuwa amekombolewa.
dunia imechange you have to accept it mengine wewe Kama mwanaume huwezi kuelewa mpaka uwe mwanamke,
Dunia imebadilika katika nini bibie ? Kwahiyo nyinyi mmekuwa ni bendera fata upepo siyo ? Kuna mabadiliko ambayo hayabadilishi asili hata kwa bahati mbaya, hakuna mabadiliko ambayo hubadilisha majukumu ya mwanaume kwa mwanamke au mwanamke kwa mwanaume na familia, hili halipo bibie.

Dunia ni ile ile na watu ni wale wale, ila iliyo badilika ni fikra na mitazamo tu na maendeleo ya kiteknolojia.

Nisilo lielewa bibie labda ule uchungu wenu mnapo zaa au hali zenu mnapoingia katika ada(hedhi) zenu ila hata hizo huwa mnatupa habari.
usiwe Kama wasaudia wanaume wazima Wana discuss Mambo ya hedhi ya wanawake bila wanawake wenyewe kuwepo na kuelezea Mambo yao ya hedhi.
Hakuna siku umeandika ujinga kama haya maneno yako. Hedhi ni zaidi ya unavyoijua wewe kama ni damu chafu,ila hedhi ina tuhusu sisi pia wanaume kwa ukaribu kwa ajili ya kuwafanyia wema wake zetu na kuwapa stahiki zao.

Wewe mpaka unakufa huwezi kuiongelea hedhi katika hakika yake na hukumu zake.
In short wanaume insecure tuacheni wanawake na Mambo yetu nyie Nani wakutupangia mtukome
Bibie usikate tamaa, hatukupangii ila tunawaonyesha wapi mlipo kosea.
 
Rudi kujisoma

labda uweke 'baadhi ya wanawake'ndio italeta uhalisia
Labda lugha yangu itakuwa ngumu sana hukuelewa au una umakini mdogo sana katika hili, hilo unalo litaka nimeliandika humo.

Ngoja nikuonyeshe hilo unalo taka ulione ambalo hukuliona huko lakini lipo :

".....wengi wao hawalijui hili isipokuwa wachache walio rehemewa,....."
 
Back
Top Bottom