cheupe sr
Senior Member
- Aug 18, 2012
- 102
- 34
Habari zenu wana JF,
Nimekua mara nyingi najiuliza bila kupata majibu , na leo nimeona nirudi jamvini pengine nipate mawazo tofauti kutoka kwa wadau. Hivi ni kwanini wanaume kwa asilimia kubwa walio kwenye ndoa huongea kwa ukali/hawana lugha za kimahaba wanavyoongea na wake zao kwenye simu?
Hili jambo huwa linanisikitisha sana, yaani mwanamke hata ujitaidi vipi lakini mwenzio mkavuu kama kauzu..
Labda niwakumbushe tu ndugu zangu wanaume, mapenzi ni kwa pande zote mbili huwa mara nyingi mnajisahau mnafikiri ni nyie peke yenu ndo mnastaili kupendwa na kupewa mahaba 24-7, but unasahau nawe unajukumu la kumpenda mkeo na si tu kumpenda bila matendo hayo yanakua si mapenzi bali ni maigizo..
Nashangaa sana, unataka mkeo akapate wapi mapenzi zaidi ya kwako?? Na ndio hapo mimi ninasema mara zote,wanaume ndio hasa chanzo cha wanawake kutoka nje ya ndoa na hasa ukikuta mwanamke si mvumilivu..
Sawa maisha yanaenda yanabadilika kuanzia mlivyokua girlfriend na boyfriend mpaka sasa labda mnafamilia ya watoto kadhaa, ila mapenzi lazima yaendelee.
Ninafahamu familia kama mbili hivi ambazo tangu nakua mpaka sasa wale wazee wana wajukuu, lakini ukimsikia yule baba anavyo msemesha yule mama ambaye anaweza akafika miaka kama 65 hivi, kwa kweli utawa admire sana, ni wanaume wachache sana wenye karama hizo.
Nadhani pia mmesahau kuwa mapenzi yanajengwa na vikitu vidogo vidogo, sio mpaka umnunulie mkeo mercedece benz ndo atajua unampenda NO NO NO, kauli tu na matendo hicho ndicho haswa tunachokihitaji wanawake ili nasi tujisikie burudani..
Karibuni wadau nanyi mtoe michango yenu..
Nimekua mara nyingi najiuliza bila kupata majibu , na leo nimeona nirudi jamvini pengine nipate mawazo tofauti kutoka kwa wadau. Hivi ni kwanini wanaume kwa asilimia kubwa walio kwenye ndoa huongea kwa ukali/hawana lugha za kimahaba wanavyoongea na wake zao kwenye simu?
Hili jambo huwa linanisikitisha sana, yaani mwanamke hata ujitaidi vipi lakini mwenzio mkavuu kama kauzu..
Labda niwakumbushe tu ndugu zangu wanaume, mapenzi ni kwa pande zote mbili huwa mara nyingi mnajisahau mnafikiri ni nyie peke yenu ndo mnastaili kupendwa na kupewa mahaba 24-7, but unasahau nawe unajukumu la kumpenda mkeo na si tu kumpenda bila matendo hayo yanakua si mapenzi bali ni maigizo..
Nashangaa sana, unataka mkeo akapate wapi mapenzi zaidi ya kwako?? Na ndio hapo mimi ninasema mara zote,wanaume ndio hasa chanzo cha wanawake kutoka nje ya ndoa na hasa ukikuta mwanamke si mvumilivu..
Sawa maisha yanaenda yanabadilika kuanzia mlivyokua girlfriend na boyfriend mpaka sasa labda mnafamilia ya watoto kadhaa, ila mapenzi lazima yaendelee.
Ninafahamu familia kama mbili hivi ambazo tangu nakua mpaka sasa wale wazee wana wajukuu, lakini ukimsikia yule baba anavyo msemesha yule mama ambaye anaweza akafika miaka kama 65 hivi, kwa kweli utawa admire sana, ni wanaume wachache sana wenye karama hizo.
Nadhani pia mmesahau kuwa mapenzi yanajengwa na vikitu vidogo vidogo, sio mpaka umnunulie mkeo mercedece benz ndo atajua unampenda NO NO NO, kauli tu na matendo hicho ndicho haswa tunachokihitaji wanawake ili nasi tujisikie burudani..
Karibuni wadau nanyi mtoe michango yenu..