Kwa nini mnakubali chama chenu kuchafuliwa na kukejeliwa kama ni Chama Cha Mafisadi. Je, katika kanuni zenu hakuna kanuni (au kipengele cha katiba yenu) inayosimamia integrity wa wanachama wenu? Nauliza kwa sababu wengi wa viongozi wa juu wa chama chenu wanatuhumiwa kwa kufanya ufisadi mkubwa sana katika nchi hii. Je mmechukua hatua gani kuwashughulikia wanaCCM walio ndani ya serikali na waliojiuzulu kwa ajili ya tuhuma za ufisadi. Kama hakuna hatua zozote zilizochukuliwa naomba mtangaze rasmi kuwa CCM haisimami kama kifupi cha Chama Cha Mapinduzi na bali Chama Cha Mafisadi.